OFISAUhusiano wa Mfuko wa Pencheni (PPF) Edward Kyungu akitowa maelezo kwa mwananchi katika banda la Wizara ya Fedha, akitaka kujua muhimu wa mfuko huo katika maonesho ya wakulima ya nane nane yanayoendelea mjini Dodoma.(Picha kwa hisani ya Hazina.)
Thursday, 4 August 2011
KARAFUU ZAPANDA BEI TENA
Karafuu zapanda bei tena
Na Mwandishi Wetu
IKIWA siku chache kupita tangu serikali kutangaza bei mpya ya karafuu, bei imepandishwa tena ambapo katika bei hiyo mpya kilo moja ya daraja la kwanza itauzwa kwa bei ya shilingi 15,000 huku pishi ikiuzwa kwa shilingi 22,000.
Bei hiyo mpya, kwa kiasi kikubwa itawanufaisha wakulima na kuacha kuzisafisrisha kwa njia ya magengo kuzipeleka nchi jirani.
Taarifa iliyotolewa na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Bishara ya Taifa Zanzibar (ZSTC), Suleiman Juma Jongo amesema bei mpya ya kilo moja ya daraja la kwanza itapanda kutoka shilingi 10,000 hadi 15, huku pishi moja ikiuzwa shilingi 22,000 badala ya shilingi 15,000 za awali.
Alisema kuwa daraja la pili la karafuu kilo moja itauzwa shilingi 14,500 badala ya 9,500, huku pishi moja ya daraja hilo ikipanda kutoka kutoka shilingi 14,250 hadi 21,500.
Aidha Jongo alisema kilo moja ya karafuu daraja la tatu itauzwa shilingi 14,000 kutoka shilingi 9,000 na pishi moja ya daraja hilo itauzwa shilingi 21,000 kutoka shilingi 13,500.
Katika tangazo hilo jipya, bei ya makonyo itauzwa kilo moja shilingi 1,500 huku kila mwenye shamba la karafuu akitakiwa kumlipa shilingi 2,000 mchumaji kwa kila pishi moja.
Mkurugenzi huyo alisema kupandishwa kwa bei hiyo mpya kunafuatia ahadi iliyowekwa na Rais wa Zanzibar kupandisha bei ya zao hilo ili liweze kuleta tija kwa wakulima.
"Katika kutekeleza ahadi ya Rais, serikali inatangaza mabadiliko ya bei ya karafuu itakayotumika hivi sasa badala ya zile zilizotangazwa hapo awali”, ilieleza sehemu ya taarifa hiyo.
Alisema kupandishwa huko sio mwisho wa safari kwani, serikali itapandisha bei ya zao hilo kulingana na kupanda bei katika soko la dunia.
Mkurugenzi huyo aliwaomba wananchi watoe ushirikiano kwa kuhakikisha kuwa karafuu zao zote wanaziuza kupitia shirika la ZSTC na kuacha kabisa kuzisafirisha kwa njia ya magendo ambayo yanaangusha uchumi wa Zanzibar.
Kenya inatajwa kuwa imekuwa ikipokea karafuu za Zanzibar kwa njia ya magendo na kuziuza katika soko la dunia pamoja na kwamba nchi hiyo haizalishi karafuu.
Nchi nyengine maarufu zinazozalisha karafuu ukiachilia Zanzibar ni pamoja na Indonesia, India, Madagascar, Brazil, Comoro na Sri Lanka.
Na Mwandishi Wetu
IKIWA siku chache kupita tangu serikali kutangaza bei mpya ya karafuu, bei imepandishwa tena ambapo katika bei hiyo mpya kilo moja ya daraja la kwanza itauzwa kwa bei ya shilingi 15,000 huku pishi ikiuzwa kwa shilingi 22,000.
Bei hiyo mpya, kwa kiasi kikubwa itawanufaisha wakulima na kuacha kuzisafisrisha kwa njia ya magengo kuzipeleka nchi jirani.
Taarifa iliyotolewa na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Bishara ya Taifa Zanzibar (ZSTC), Suleiman Juma Jongo amesema bei mpya ya kilo moja ya daraja la kwanza itapanda kutoka shilingi 10,000 hadi 15, huku pishi moja ikiuzwa shilingi 22,000 badala ya shilingi 15,000 za awali.
Alisema kuwa daraja la pili la karafuu kilo moja itauzwa shilingi 14,500 badala ya 9,500, huku pishi moja ya daraja hilo ikipanda kutoka kutoka shilingi 14,250 hadi 21,500.
Aidha Jongo alisema kilo moja ya karafuu daraja la tatu itauzwa shilingi 14,000 kutoka shilingi 9,000 na pishi moja ya daraja hilo itauzwa shilingi 21,000 kutoka shilingi 13,500.
Katika tangazo hilo jipya, bei ya makonyo itauzwa kilo moja shilingi 1,500 huku kila mwenye shamba la karafuu akitakiwa kumlipa shilingi 2,000 mchumaji kwa kila pishi moja.
Mkurugenzi huyo alisema kupandishwa kwa bei hiyo mpya kunafuatia ahadi iliyowekwa na Rais wa Zanzibar kupandisha bei ya zao hilo ili liweze kuleta tija kwa wakulima.
"Katika kutekeleza ahadi ya Rais, serikali inatangaza mabadiliko ya bei ya karafuu itakayotumika hivi sasa badala ya zile zilizotangazwa hapo awali”, ilieleza sehemu ya taarifa hiyo.
Alisema kupandishwa huko sio mwisho wa safari kwani, serikali itapandisha bei ya zao hilo kulingana na kupanda bei katika soko la dunia.
Mkurugenzi huyo aliwaomba wananchi watoe ushirikiano kwa kuhakikisha kuwa karafuu zao zote wanaziuza kupitia shirika la ZSTC na kuacha kabisa kuzisafirisha kwa njia ya magendo ambayo yanaangusha uchumi wa Zanzibar.
Kenya inatajwa kuwa imekuwa ikipokea karafuu za Zanzibar kwa njia ya magendo na kuziuza katika soko la dunia pamoja na kwamba nchi hiyo haizalishi karafuu.
Nchi nyengine maarufu zinazozalisha karafuu ukiachilia Zanzibar ni pamoja na Indonesia, India, Madagascar, Brazil, Comoro na Sri Lanka.
SPIKA KIFICHO BACK BENCHERS NI KIBOKO
Spika Kificho: ‘Back Benchers’ ni kiboko
Asema wanawachangamshwa mawaziri
Dk. Migoro UN imefurahishwa hali ya Zanzibar
Na Himid Choko, BLW
SPIKA Baraza la Wawakilishi la Zanzibar Pandu Ameir Kificho amesema wajumbe wa Baraza hilo hasa wale wasiokuwa mawaziri (Back Benchers), wamekuwa makini zaidi kufutilia utendaji wa serikali jambo ambalo ni wajibu wao wa kikatiba.
Alisema hatua hiyo imekuwa ikileta changamoto kwa mawaziri na serikali kwa ujumla na kuongeza uwajibikaji, ambapo mawaziri wasipokuwa makini wanaweza kujikuta wajumbe wanaelewa zaidi kuhusiana na wizara zao kuliko wao wenyewe.
Spika Kificho alisema jana wakati akizungumza na Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Dk. Asha Rose Migiro huko ofisini kwake Chukwani nje kidogo ya mji wa Zanzibar.
Alisema katika mkutano wa bajeti uliomalizika mwishoni mwa wiki iliyopita mijadala ya mkutano huo ilikuwa kivutio na kutoa msisimko mkubwa kwa wananchi kutokana na umakini wa wajumbe wa Baraza hilo kuhoji na mawaziri kujibu hoja mbali mbali.
“Ingawa hivi sasa hakuna kambi ya upinzani, lakini Baraza limekuwa likiendelea vizuri na kuwavutia wananchi wengi kwani ‘Benchers’ wamekuwa makini kuhakikisha utendaji unakwenda vizuri chini ya usimamizi wa Baraza la Wawakilishi”, Kificho alimueleza Dk. Migiro.
Naye Naibu Dk. Migiro alisema Umoja wa Mataifa umefurahishwa na hatua iliyofikiwa na Zanzibar kwa kiungia katika mfumo wa Serikali ya Umoja wa Kitaifa na mafanikio makubwa yaliyofikiwa na kuwa mfano wa kuigwa duniani.
Alisema Umoja wa Mataifa unaamini kwamba mfumo huo umechangia kwa kiasi kikubwa hali ya amani na utulivu uliopo hapa nchini.
Alisema hali ya mambo Zanzibar imekuwa kivutio kikubwa kwa Umoja huo katika kutoa fursa nzuri zaidi ya kusaidia nyanja mbali mbali za maendeleo hapa Zanzibar.
“Amani na utulivu ni miongoni mwa mihimili mikuu ya Umoja wa Mataifa , tutapokuwa na amani kwenye nchi ndipo na sisi Umoja wa Mataifa tunapokuwa na fursa nzuri zaidi ya kusaidia kufikia katika maendeleo”, alisisitiza Dk. Migiro ambae alikuwa akitoa salamu za Katibu Mkuu wake , Ban Kimoon.
Alisema umoja huo unafuatilia kwa karibu utendaji wa serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar chini ya muundo wa Umoja wa Kitaifa na umeridhishwa na utendaji wa serikali hiyo.
Asema wanawachangamshwa mawaziri
Dk. Migoro UN imefurahishwa hali ya Zanzibar
Na Himid Choko, BLW
SPIKA Baraza la Wawakilishi la Zanzibar Pandu Ameir Kificho amesema wajumbe wa Baraza hilo hasa wale wasiokuwa mawaziri (Back Benchers), wamekuwa makini zaidi kufutilia utendaji wa serikali jambo ambalo ni wajibu wao wa kikatiba.
Alisema hatua hiyo imekuwa ikileta changamoto kwa mawaziri na serikali kwa ujumla na kuongeza uwajibikaji, ambapo mawaziri wasipokuwa makini wanaweza kujikuta wajumbe wanaelewa zaidi kuhusiana na wizara zao kuliko wao wenyewe.
Spika Kificho alisema jana wakati akizungumza na Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Dk. Asha Rose Migiro huko ofisini kwake Chukwani nje kidogo ya mji wa Zanzibar.
Alisema katika mkutano wa bajeti uliomalizika mwishoni mwa wiki iliyopita mijadala ya mkutano huo ilikuwa kivutio na kutoa msisimko mkubwa kwa wananchi kutokana na umakini wa wajumbe wa Baraza hilo kuhoji na mawaziri kujibu hoja mbali mbali.
“Ingawa hivi sasa hakuna kambi ya upinzani, lakini Baraza limekuwa likiendelea vizuri na kuwavutia wananchi wengi kwani ‘Benchers’ wamekuwa makini kuhakikisha utendaji unakwenda vizuri chini ya usimamizi wa Baraza la Wawakilishi”, Kificho alimueleza Dk. Migiro.
Naye Naibu Dk. Migiro alisema Umoja wa Mataifa umefurahishwa na hatua iliyofikiwa na Zanzibar kwa kiungia katika mfumo wa Serikali ya Umoja wa Kitaifa na mafanikio makubwa yaliyofikiwa na kuwa mfano wa kuigwa duniani.
Alisema Umoja wa Mataifa unaamini kwamba mfumo huo umechangia kwa kiasi kikubwa hali ya amani na utulivu uliopo hapa nchini.
Alisema hali ya mambo Zanzibar imekuwa kivutio kikubwa kwa Umoja huo katika kutoa fursa nzuri zaidi ya kusaidia nyanja mbali mbali za maendeleo hapa Zanzibar.
“Amani na utulivu ni miongoni mwa mihimili mikuu ya Umoja wa Mataifa , tutapokuwa na amani kwenye nchi ndipo na sisi Umoja wa Mataifa tunapokuwa na fursa nzuri zaidi ya kusaidia kufikia katika maendeleo”, alisisitiza Dk. Migiro ambae alikuwa akitoa salamu za Katibu Mkuu wake , Ban Kimoon.
Alisema umoja huo unafuatilia kwa karibu utendaji wa serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar chini ya muundo wa Umoja wa Kitaifa na umeridhishwa na utendaji wa serikali hiyo.
TENDWA SINA UBAVU KUDHIBITI UTOVU WA NIDHAMU BUNGENI.
Tendwa: Sina ubavu kudhibiti utovu wa nidhamu Bungeni
Joseph Ishengoma na Mpoki Ngoloke, Dar
MSAJILI wa vyama vya siasa nchini John Tendwa amesema ofisi yake haina upavu kisheria kukifuta chama chochote cha siasa kutokana na wabunge wake kukosa heshima bungeni.
Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake jana jinini Dar es Salaam Tendwa alisema Bunge ni mhimili wa serikali baada ya Mahakama na Utawala, na kuna kanuni lililojiwekea za kuwaongoza namna ya kufanyakazi zao.
Hivi karibuni kumekuwepo na vitendo vya vurugu bungeni, kuwasha vipaza sauti ovyo na kupiga kelele bila kuruhusiwa na Spika au Mwenyekiti wa Bunge, hali ambayo imesababisha baadhi ya wabunge kupewa adhabu ya kutolewa nje ya ukumbi kwa kukiuka kanuni.
“Wabunge wakiwa ndani ya bunge sio wangu, sina madaraka nao, lakini wakiwa nje ya kuta za bunge ni wangu. Ndani ya Bunge mikono na midomo yangu imefungwa kabisa, lakini kwa mtazamo wa wananchi wanajua kuwa mimi ninamamlaka ya kuwawajibisha kutokana na utovu wa nidhamu wanouonyesha bungeni, lakini sio,” alisema.
“Mimi nimechukia sana kuona vitendo hivi kwasababu natupiwa lawama na watu kuwa wanaofanya vurugu bungeni ni watu wanaotoka katika vyama vyangu. Ninafurahi kwakuwa vyama vyangu nilivyovisajili viko ndani ya bunge, lakini sifurahishwi na utovu wa nidhamu wanaofanya”,alisema Tendwa.
Kwa mujibu wa Msajili wa vyama vya Siasa, baadhi ya wabunge vitendo wanavyofanya ndani ya Bunge kila anayesikia au kushuhdia vitendo hivyo, lazima asikitike.
Taratibu na mamlaka ya kudhibiti utovu huo wa nidhamu uko ndani ya Bunge. Bunge ni taasisi inayojitegemea haiingiliwi na upande wowote (Mahakama na Utawala).
Baadaye mwezi huu, Msajili wa Vyama vya Siasa atakutana na viongozi mbalimbali wa vyama vya siasa katika baraza la vyama na kuwaelezea masikitiko yake.
“Tutakuwa katika baraza la vyama kabla ya bunge lijalo. Tutazungumzia hali hii na kutoa jibu,” amesema.
Joseph Ishengoma na Mpoki Ngoloke, Dar
MSAJILI wa vyama vya siasa nchini John Tendwa amesema ofisi yake haina upavu kisheria kukifuta chama chochote cha siasa kutokana na wabunge wake kukosa heshima bungeni.
Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake jana jinini Dar es Salaam Tendwa alisema Bunge ni mhimili wa serikali baada ya Mahakama na Utawala, na kuna kanuni lililojiwekea za kuwaongoza namna ya kufanyakazi zao.
Hivi karibuni kumekuwepo na vitendo vya vurugu bungeni, kuwasha vipaza sauti ovyo na kupiga kelele bila kuruhusiwa na Spika au Mwenyekiti wa Bunge, hali ambayo imesababisha baadhi ya wabunge kupewa adhabu ya kutolewa nje ya ukumbi kwa kukiuka kanuni.
“Wabunge wakiwa ndani ya bunge sio wangu, sina madaraka nao, lakini wakiwa nje ya kuta za bunge ni wangu. Ndani ya Bunge mikono na midomo yangu imefungwa kabisa, lakini kwa mtazamo wa wananchi wanajua kuwa mimi ninamamlaka ya kuwawajibisha kutokana na utovu wa nidhamu wanouonyesha bungeni, lakini sio,” alisema.
“Mimi nimechukia sana kuona vitendo hivi kwasababu natupiwa lawama na watu kuwa wanaofanya vurugu bungeni ni watu wanaotoka katika vyama vyangu. Ninafurahi kwakuwa vyama vyangu nilivyovisajili viko ndani ya bunge, lakini sifurahishwi na utovu wa nidhamu wanaofanya”,alisema Tendwa.
Kwa mujibu wa Msajili wa vyama vya Siasa, baadhi ya wabunge vitendo wanavyofanya ndani ya Bunge kila anayesikia au kushuhdia vitendo hivyo, lazima asikitike.
Taratibu na mamlaka ya kudhibiti utovu huo wa nidhamu uko ndani ya Bunge. Bunge ni taasisi inayojitegemea haiingiliwi na upande wowote (Mahakama na Utawala).
Baadaye mwezi huu, Msajili wa Vyama vya Siasa atakutana na viongozi mbalimbali wa vyama vya siasa katika baraza la vyama na kuwaelezea masikitiko yake.
“Tutakuwa katika baraza la vyama kabla ya bunge lijalo. Tutazungumzia hali hii na kutoa jibu,” amesema.
MAOFISA, WAKULIMA KUSHIRIKI MAONESHO DODOMA
Maofisa, wakulima kushiriki maonesho Dodoma
Na Shauri Makame
WAKULIMA 53 na maofisa 12 kutoka wizara ya Kilimo na Maliasili, wanatarajiwa kuondoka Zanzibar kuelekea mkoani Dodoma kwenye maonesho ya wakulima (nane nane).
Maonesha hayo ambayo yanayofanyika katika ngazi ya kitaifa mkoani humo kwa mwaka wa nne mfululizo yaliyofunguliwa rasmin juzi na rais wa Jamhuri ya Tanzania, Jakaya Mrisho Kikwete, yanatarajiwa kumalizika Agosti 8 mwaka huu.
Msafara huo wa Zanzibar utaongozwa na ofisa Ufatiliaji na Tathmini (AM&E) wa Programu za Kuimarisha Huduma za Kilimo na Sekta ya Kuendeleza Mifugo (ASSP na ASDP-L), program ndogo ya Zanzibar, Mtingwa Ramadhan Mapuri.
Akizungumza na mwandishi wa habari hizi kabla ya kuondoka mkuu huyo wa msafara aliwataka wakulima kuithamini ziara hiyo ya mafunzo ambayo inalengo la kubadilishana mawazo na uzowefu miongoni mwa wakulima wa Tanzania.
Alisema uzowefu wa ziara kama hizo zilizopita umeonesha kwamba wakulima na wafugaji wengi wa Zanzibar hupiga hatua kubwa ya uzalishaji kwa kuiga taaluma mbali mbali kutoka kwa wakulima wenzao wa Tanzania Bara.
Maonesho ya wakulima nane nane ambayo hufanyika kila mwaka katika mwezi wa Agosti ambapo wakulima na wafugaji hupata fursa ya kuonesha bidhaa mbali mbali wanazozalisha sambamba na kubadilishana mawazo miongoni mwao.
Ziara hiyo ambayo imefadhiliwa na progamu za ASSP na ASDP-L, progamu ndogo ya Zanzibar, imegharimu jumla ya shilingi milioni 23,220,000.
Programu za ASSP na ASDP-L ambapo lengo lake ni kumpunguzia umasikini mkulima na kumwezesha kuwa na uhakika wa chakula, zimekuwa zikiwapeleka wakulima kwenye maonesho kama hayo tangu mwaka 2008 kwa lengo la kupata mbinu mbadala za uzalishaji wenye tija zaidi.
Na Shauri Makame
WAKULIMA 53 na maofisa 12 kutoka wizara ya Kilimo na Maliasili, wanatarajiwa kuondoka Zanzibar kuelekea mkoani Dodoma kwenye maonesho ya wakulima (nane nane).
Maonesha hayo ambayo yanayofanyika katika ngazi ya kitaifa mkoani humo kwa mwaka wa nne mfululizo yaliyofunguliwa rasmin juzi na rais wa Jamhuri ya Tanzania, Jakaya Mrisho Kikwete, yanatarajiwa kumalizika Agosti 8 mwaka huu.
Msafara huo wa Zanzibar utaongozwa na ofisa Ufatiliaji na Tathmini (AM&E) wa Programu za Kuimarisha Huduma za Kilimo na Sekta ya Kuendeleza Mifugo (ASSP na ASDP-L), program ndogo ya Zanzibar, Mtingwa Ramadhan Mapuri.
Akizungumza na mwandishi wa habari hizi kabla ya kuondoka mkuu huyo wa msafara aliwataka wakulima kuithamini ziara hiyo ya mafunzo ambayo inalengo la kubadilishana mawazo na uzowefu miongoni mwa wakulima wa Tanzania.
Alisema uzowefu wa ziara kama hizo zilizopita umeonesha kwamba wakulima na wafugaji wengi wa Zanzibar hupiga hatua kubwa ya uzalishaji kwa kuiga taaluma mbali mbali kutoka kwa wakulima wenzao wa Tanzania Bara.
Maonesho ya wakulima nane nane ambayo hufanyika kila mwaka katika mwezi wa Agosti ambapo wakulima na wafugaji hupata fursa ya kuonesha bidhaa mbali mbali wanazozalisha sambamba na kubadilishana mawazo miongoni mwao.
Ziara hiyo ambayo imefadhiliwa na progamu za ASSP na ASDP-L, progamu ndogo ya Zanzibar, imegharimu jumla ya shilingi milioni 23,220,000.
Programu za ASSP na ASDP-L ambapo lengo lake ni kumpunguzia umasikini mkulima na kumwezesha kuwa na uhakika wa chakula, zimekuwa zikiwapeleka wakulima kwenye maonesho kama hayo tangu mwaka 2008 kwa lengo la kupata mbinu mbadala za uzalishaji wenye tija zaidi.
MARUFUKU KUINGIZA BIDHAA ZA MIGAMBA KUTOKA BARA.
Marufuku kuingiza bidhaa za mgomba kutoka Bara
Na Nafisa Madai, Maelezo
WIZARA ya Kilimo Maliasili imepiga marufuku uingizaji wa bidhaa zinazotokana mgomba ikiwemo ndizi, miche ya migomba, majani ya migomba pamoja vigogo vya mgomba kutoka Tanzania bara.
Akitoa taarifa hiyo kwa vyombo vya habari huko ofisini kwake Mwanakwerekwe wiliya ya Magharib, Mkuu wa Kitengo cha Uhifadhi na Utibabu wa mazao Zainab Salim Abdallah, alisema marufuku ya kuingizwa kwa bidhaa hizo inafuatia kuibuka maradhi mnyauko.
Alisema maradhi hayo yanayosababishwa na bakteria yamekuwa yakiathiri migomba pamoja na mazao yake ambapo kizuizi kilichowekwa kinalenga kuiepusha Zanzibar kukumbwa na maradhi hayo.
Mkuu huyo alisema Tanzania bara imekumbwa na maradhi hayo tangu mwaka 2007, ambapo kama Idara inalazimika kuchukua hatua ya kuzuia hasa katika kipindi hicho cha mwezi wa Ramadhani kutokana na walaji ndizi kuongezeka kuliko siku za kawaida.
Zainab alisema kuwa maradhi ya mnyauko hayamuathiri mlaji wa ndizi bali athari kubwa anaweza akaipata mkulima wa migomba endapo bidhaa hiyo kwani itamsababishia hasara kubwa mkulima huyo kwa asilimia 100.
Aliwaomba Wazanzibari kutoa mashirikiano katika kutekelezwa kwa ahizo hilo ili kuepusha kusambaa kwa maradhi hayo kwa migomba ya Zanzibar.
Zainab alisema mtu yoyote atayekamata anaingiza bidhaa hiyo kutoka bara atafikishwa katika vyombo vya sheria na sheria itashika mkono wake kwa muingizaji huyo.
Alisema kitengo chake tayari kimeshakamata ndizi amabazo zimebainika na maradhi hayo kutoka bara na mipango inaandaliwa kuziangamiza ndizi hizo ili iwe fundisho kwa wengine ambao wanampango wa kuingiza ndizi Zanzibar.
Akizungumzia nzi wa matunda alisema nzi hao hivi sasa wameshamiri sana visiwani hapa na wamekuwa wakishambulia embe kwa kiasi kubwa jambo ambalo limekua likiwavunja moyo wakulima wa zao hilo.
Aidha alisema nzi hao ambao chimbulo lake Indonesia wamekua wakileta hasara kubwa kwa wakulima kwani soko limekua dogo sana ikilinganisha na hapo awali.
Hata hivyo alisema juhudi zinafanywa za kuangamizwa nzi hao za kuwawekea mitego maalum na kwasasa tayari wameanza katika wilaya ya Kusini na wamefanikiwa kwa aslimia hamsini ambapo zoezi hilo linategemewa kufanya katika mikoa yote ya Zanzibar.
Akizungumzia mende wadogo ambao nao wameshamiri kwa wingi katika visiwa vya Unguja, alisema mende hao wanaathiri sana katika makaazi ya watu kwani hushambulia nguo na vitu vyengine majumbani.
Amesema kuwa mende hao wametokea ulaya na wamekuja kutokana na vifaa vya umeme vinavyoingizwa na ambavyo vimezagaa katika Manispaa ya mji wa Zanzibar.
Aidha alisema juhudi za makusudi zinachukuliwa za kutokomeza mende hao maarufu mende wa Ulaya, na kuwaasa wale wote wanafanya biashara hiyo ya vifaa vilivyokwisha tumika kuangalia kwa makini vifaa hiyo kwani athari yake baadae inaweza kuwa kubwa zaidi.
Na Nafisa Madai, Maelezo
WIZARA ya Kilimo Maliasili imepiga marufuku uingizaji wa bidhaa zinazotokana mgomba ikiwemo ndizi, miche ya migomba, majani ya migomba pamoja vigogo vya mgomba kutoka Tanzania bara.
Akitoa taarifa hiyo kwa vyombo vya habari huko ofisini kwake Mwanakwerekwe wiliya ya Magharib, Mkuu wa Kitengo cha Uhifadhi na Utibabu wa mazao Zainab Salim Abdallah, alisema marufuku ya kuingizwa kwa bidhaa hizo inafuatia kuibuka maradhi mnyauko.
Alisema maradhi hayo yanayosababishwa na bakteria yamekuwa yakiathiri migomba pamoja na mazao yake ambapo kizuizi kilichowekwa kinalenga kuiepusha Zanzibar kukumbwa na maradhi hayo.
Mkuu huyo alisema Tanzania bara imekumbwa na maradhi hayo tangu mwaka 2007, ambapo kama Idara inalazimika kuchukua hatua ya kuzuia hasa katika kipindi hicho cha mwezi wa Ramadhani kutokana na walaji ndizi kuongezeka kuliko siku za kawaida.
Zainab alisema kuwa maradhi ya mnyauko hayamuathiri mlaji wa ndizi bali athari kubwa anaweza akaipata mkulima wa migomba endapo bidhaa hiyo kwani itamsababishia hasara kubwa mkulima huyo kwa asilimia 100.
Aliwaomba Wazanzibari kutoa mashirikiano katika kutekelezwa kwa ahizo hilo ili kuepusha kusambaa kwa maradhi hayo kwa migomba ya Zanzibar.
Zainab alisema mtu yoyote atayekamata anaingiza bidhaa hiyo kutoka bara atafikishwa katika vyombo vya sheria na sheria itashika mkono wake kwa muingizaji huyo.
Alisema kitengo chake tayari kimeshakamata ndizi amabazo zimebainika na maradhi hayo kutoka bara na mipango inaandaliwa kuziangamiza ndizi hizo ili iwe fundisho kwa wengine ambao wanampango wa kuingiza ndizi Zanzibar.
Akizungumzia nzi wa matunda alisema nzi hao hivi sasa wameshamiri sana visiwani hapa na wamekuwa wakishambulia embe kwa kiasi kubwa jambo ambalo limekua likiwavunja moyo wakulima wa zao hilo.
Aidha alisema nzi hao ambao chimbulo lake Indonesia wamekua wakileta hasara kubwa kwa wakulima kwani soko limekua dogo sana ikilinganisha na hapo awali.
Hata hivyo alisema juhudi zinafanywa za kuangamizwa nzi hao za kuwawekea mitego maalum na kwasasa tayari wameanza katika wilaya ya Kusini na wamefanikiwa kwa aslimia hamsini ambapo zoezi hilo linategemewa kufanya katika mikoa yote ya Zanzibar.
Akizungumzia mende wadogo ambao nao wameshamiri kwa wingi katika visiwa vya Unguja, alisema mende hao wanaathiri sana katika makaazi ya watu kwani hushambulia nguo na vitu vyengine majumbani.
Amesema kuwa mende hao wametokea ulaya na wamekuja kutokana na vifaa vya umeme vinavyoingizwa na ambavyo vimezagaa katika Manispaa ya mji wa Zanzibar.
Aidha alisema juhudi za makusudi zinachukuliwa za kutokomeza mende hao maarufu mende wa Ulaya, na kuwaasa wale wote wanafanya biashara hiyo ya vifaa vilivyokwisha tumika kuangalia kwa makini vifaa hiyo kwani athari yake baadae inaweza kuwa kubwa zaidi.
Tuesday, 2 August 2011
MAALIM SEIF KUKOSEKANA UMOJA KUMEREJESHA NYUMA ZANZIBAR.
Maalim Seif: Kukosekana umoja kumeirejesha nyuma Zanzibar
Na Mwanajuma Abdi
MAKAMU wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Maalim Seif Sharif Hamad, amesema kukosekana kwa umoja kulipelekea kujengeka uadui wa kutoaminiana, na kuheshimia miongoni mwa wananchi na kusababisha hali kuwa mbaya iliyorejesha nyuma maendeleo ya kiuchumi nchini.
Maalim Seif alieleza hayo jana wakati akifungua kongamano la siku ya Umoja wa Kitaifa, iliyotimia mwaka mmoja tokea wazanzibari kuamua mfumo huo, lililoandaliwa na Jumuiya ya Waandishi wa Habari za Maendeleo Zanzibar (WAHAMAZA) lililofanyika ukumbi wa Beyt El Yamin, mjini hapa, ambapo kauli mbiu ni ‘Zanzibar Haitarudi tena Nyuma’.
Alisema kukosekana kwa umoja huo kulisababisha imani kudhoofika, kununiana, kutukanana, kutengana, kuhujumiana na kuuana ilimradi ubinaadamu uliondoka kabisa, jambo ambalo kwa sasa mambo hayo yameondoka.
“Wenye busara wamekuwa wakisema ‘ikiondoka imani, hakuna amani’, hakuna aliyeishi kwa amani, hata kama akilindwa nje ya maridhiano na umoja wa kitaifa”, alisisitiza maalim Seif.
Alieleza wengi wao ni mashahidi kuwa Zanzibar haijawahi kuwa na utulivu na kisiasa takriban nusu karne nzima, uanzishwaji wa mfumo wa kisiasa wa vyama vingi wakati wa ukoloni katika miaka ya 1950, ulisababisha mpasuko mkubwa wa kisiasa, ambapo kuanzia enzi hizo jamii ya kizanzibari iligawika karibu katikati katika mapande mawili na kila pande lilijitambulisha na chama kimoja au muungano wa zaidi chama kimoja.
“Kipindi cha 1957-1964 Zanzibar ilishuhudia msuguano mkali baina ya wafuasi wa Chama cha Afro Shirazi (ASP) kwa upande mmoja na muungano wa vyama vya Zanzibar Nationalist Party – Hizb al Wattan (ZNP) na Zanzibar Pemba Peoples Party (ZPPP), msuguano huo ulipelekea wazanzibari kuukaribisha uhuru wake Disemba 10, 1963 kwa mitazamo tofauti”, alisema.
Alisema masikitiko makubwa walioyashuhudia wananchi baada ya mfumo wa vyama vingi kurejeshwa ni kurejea kwa ule mpasuko wa jamii ya kizanzibari, ambapo nchi iligawika nusu ya watu wakaunga mkono chama mrithi wa ASP yaani CCM na nusu wakaunga mkono chama kipya cha CUF.
Alieleza mfumo wa utawala uliokuwepo wa mshindi kuchua kila kitu na alieshindwa kupoteza kila kitu ulichochea msuguano uliowepo.
Aidha alifahamisha kuwa, sasa ni miezi tisa tangu kuundwa kwa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar yenye mfumo wa Umoja wa Kitaifa, ambapo alimshukuru Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Ali Mohamed Shein kwa kuiongoza serikali hiyo kwa hekima na busara kubwa kiasi kwamba viongozi wanashirikiana katika kazi kwa ajili ya kuwaletea maslahi wananchi wa visiwa hivi.
Aliongeza kusema kwamba, Umoja wa Kitaifa ni hazina ya wazanzibari kwa zama na zama huko nyuma, hazina hiyo ilikuwa imepotea kwa zaidi kidogo ya nusu karne sasa imepatikana kwa watu kuishi kwa kuvumiliana, kuheshimiana, kusaidiana na kutakiana kila la kheri kwa hakika na kufikia ukombozi wa kweli wa nchi na maisha kwa ujumla.
Nae Katibu wa WAHAMAZA, Mwandishi Mwandamizi, Salma Said alisema ni mwaka mmoja uliopita nchi kuripuka kwa furaha baada ya matokeo ya kura ya maoni ya kudhihirisha kuwa karibu thuluthi mbili ya wazanzibari walichagua kupiga NDIO katika kura hiyo na hivyo kufungua ukurasa mpya wa kisiasa.
Aliomba Serikali siku hiyo ifanywe iwe kumbukumbu kwa ajili ya vizazi vijavyo.
Nao watoa mada katika kongamano hilo, walishauri Serikali kuangalia changamoto mbali mbali zinazoikabili Serikali hiyo ikiwemo ufisadi na rushwa iliyotawala nchini, matumizi ya magari ya fahari ya Mawaziri na muundo mkubwa wa Baraza la Mawaziri, ambapo wengine hata Wizara hawana, jambo ambalo kwa nchi kama hii changa linaongeza umasikini.
Makamu wa Kwanza wa Rais, maalim Seif Sharif Hamad alitoa ufafanuzi juu ya maswali hayo kwa kusema si vyema wananchi wakalalamika kwani bado ni mapema kwa Serikali hiyo, ambapo aliahidi kufanyiwa kazi kasoro hizo.
Alisema suala la rushwa, mswada unatarajiwa kufikishwa katika Baraza la wawakilishi katika kikao kijacho, sambamba na kuvipongeza vyombo vya habari hasa vya Serikali kwa kupiga hatua kubwa katika utoaji wao wa taarifa.
Nao wananchi mbali mbali wakichangia katika kongamano hilo, waliomba iendelezwe na watu wasirudi kamwe walikotoka na kinachotakiwa wazanzibari wawe wamoja katika kudai mambo yanayohusu nchi yao.
Na Mwanajuma Abdi
MAKAMU wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Maalim Seif Sharif Hamad, amesema kukosekana kwa umoja kulipelekea kujengeka uadui wa kutoaminiana, na kuheshimia miongoni mwa wananchi na kusababisha hali kuwa mbaya iliyorejesha nyuma maendeleo ya kiuchumi nchini.
Maalim Seif alieleza hayo jana wakati akifungua kongamano la siku ya Umoja wa Kitaifa, iliyotimia mwaka mmoja tokea wazanzibari kuamua mfumo huo, lililoandaliwa na Jumuiya ya Waandishi wa Habari za Maendeleo Zanzibar (WAHAMAZA) lililofanyika ukumbi wa Beyt El Yamin, mjini hapa, ambapo kauli mbiu ni ‘Zanzibar Haitarudi tena Nyuma’.
Alisema kukosekana kwa umoja huo kulisababisha imani kudhoofika, kununiana, kutukanana, kutengana, kuhujumiana na kuuana ilimradi ubinaadamu uliondoka kabisa, jambo ambalo kwa sasa mambo hayo yameondoka.
“Wenye busara wamekuwa wakisema ‘ikiondoka imani, hakuna amani’, hakuna aliyeishi kwa amani, hata kama akilindwa nje ya maridhiano na umoja wa kitaifa”, alisisitiza maalim Seif.
Alieleza wengi wao ni mashahidi kuwa Zanzibar haijawahi kuwa na utulivu na kisiasa takriban nusu karne nzima, uanzishwaji wa mfumo wa kisiasa wa vyama vingi wakati wa ukoloni katika miaka ya 1950, ulisababisha mpasuko mkubwa wa kisiasa, ambapo kuanzia enzi hizo jamii ya kizanzibari iligawika karibu katikati katika mapande mawili na kila pande lilijitambulisha na chama kimoja au muungano wa zaidi chama kimoja.
“Kipindi cha 1957-1964 Zanzibar ilishuhudia msuguano mkali baina ya wafuasi wa Chama cha Afro Shirazi (ASP) kwa upande mmoja na muungano wa vyama vya Zanzibar Nationalist Party – Hizb al Wattan (ZNP) na Zanzibar Pemba Peoples Party (ZPPP), msuguano huo ulipelekea wazanzibari kuukaribisha uhuru wake Disemba 10, 1963 kwa mitazamo tofauti”, alisema.
Alisema masikitiko makubwa walioyashuhudia wananchi baada ya mfumo wa vyama vingi kurejeshwa ni kurejea kwa ule mpasuko wa jamii ya kizanzibari, ambapo nchi iligawika nusu ya watu wakaunga mkono chama mrithi wa ASP yaani CCM na nusu wakaunga mkono chama kipya cha CUF.
Alieleza mfumo wa utawala uliokuwepo wa mshindi kuchua kila kitu na alieshindwa kupoteza kila kitu ulichochea msuguano uliowepo.
Aidha alifahamisha kuwa, sasa ni miezi tisa tangu kuundwa kwa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar yenye mfumo wa Umoja wa Kitaifa, ambapo alimshukuru Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Ali Mohamed Shein kwa kuiongoza serikali hiyo kwa hekima na busara kubwa kiasi kwamba viongozi wanashirikiana katika kazi kwa ajili ya kuwaletea maslahi wananchi wa visiwa hivi.
Aliongeza kusema kwamba, Umoja wa Kitaifa ni hazina ya wazanzibari kwa zama na zama huko nyuma, hazina hiyo ilikuwa imepotea kwa zaidi kidogo ya nusu karne sasa imepatikana kwa watu kuishi kwa kuvumiliana, kuheshimiana, kusaidiana na kutakiana kila la kheri kwa hakika na kufikia ukombozi wa kweli wa nchi na maisha kwa ujumla.
Nae Katibu wa WAHAMAZA, Mwandishi Mwandamizi, Salma Said alisema ni mwaka mmoja uliopita nchi kuripuka kwa furaha baada ya matokeo ya kura ya maoni ya kudhihirisha kuwa karibu thuluthi mbili ya wazanzibari walichagua kupiga NDIO katika kura hiyo na hivyo kufungua ukurasa mpya wa kisiasa.
Aliomba Serikali siku hiyo ifanywe iwe kumbukumbu kwa ajili ya vizazi vijavyo.
Nao watoa mada katika kongamano hilo, walishauri Serikali kuangalia changamoto mbali mbali zinazoikabili Serikali hiyo ikiwemo ufisadi na rushwa iliyotawala nchini, matumizi ya magari ya fahari ya Mawaziri na muundo mkubwa wa Baraza la Mawaziri, ambapo wengine hata Wizara hawana, jambo ambalo kwa nchi kama hii changa linaongeza umasikini.
Makamu wa Kwanza wa Rais, maalim Seif Sharif Hamad alitoa ufafanuzi juu ya maswali hayo kwa kusema si vyema wananchi wakalalamika kwani bado ni mapema kwa Serikali hiyo, ambapo aliahidi kufanyiwa kazi kasoro hizo.
Alisema suala la rushwa, mswada unatarajiwa kufikishwa katika Baraza la wawakilishi katika kikao kijacho, sambamba na kuvipongeza vyombo vya habari hasa vya Serikali kwa kupiga hatua kubwa katika utoaji wao wa taarifa.
Nao wananchi mbali mbali wakichangia katika kongamano hilo, waliomba iendelezwe na watu wasirudi kamwe walikotoka na kinachotakiwa wazanzibari wawe wamoja katika kudai mambo yanayohusu nchi yao.
WAWAKILISHI WATAKA EWURA ISHITAKIWE.
Wawakilishi wataka EWURA ishitakiwe
Na Mwantanga Ame
UAMUZI wa Shirika la kudhibiti Nishati na Maji (EWURA), juu ya kuchukua jukumu la kuiuzia Zanzibar huduma ya umeme badala ya Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), umewachafua Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi na kuiomba serikali kulishitaki shirika hilo.
Wawakilishi hao walitoa kauli hiyo karibuni wakichangia hotuba ya Wizara ya Biashara, Viwanda na Masoko, iliyowasilishwa na Waziri wa Wizara hiyo Nassor Ahmed Mazrui, aliyowasilisha jana asubuhi kwa wajumbe wa baraza hilo Zanzibar.
Hapo awali Waziri huyo akiwasilisha bajeti hiyo katika maelezo yake alisema katika ukaguzi walioufanya katika baadhi ya viwanda wamebaini vimekuwa vinakabiliwa na matatizo mengi likiwemo suala la huduma ya umeme gharama zake kuwa ni kubwa.
Mwakilishi wa Wete Asaa Othman Hamad, alisema hali hiyo, serikali inapaswa kutolivumilia shirika hilo na ipo haja ya Waziri wa Nishati Zanzibar kuifungulia mashtaka taasisi hiyo.
Alisema Zanzibar hapo awali wakati inataka kutumia huduma za Shirika hilo ilifanya makubaliano na shirika la TANESCO na sio EWURA ambapo hivi sasa wamekuwa wakitakiwa kununua huduma hiyo huko.
Alisema huo ni ukiukwaji mkubwa wa mkataba wa makubaliano juu ya ununuzi wa huduma hiyo ya umeme kwani hawaoni haja ya kununuliwa katika duka la rejareja wakati makubaliano ni katika duka la jumla.
Alisema inawezekana ikawa shirika hilo linafanya kwa makusudi ili kuwakatisha tamaa watumiaji wa huduma hiyo ya umeme, jambo ambalo hivi sasa watu wengi wanashindwa kuwa na huduma hiyo majumbani na baadhi ya sehemu za uzalishaji kulikosababishwa na gaharama kuwa ni kubwa.
Alisema Shirika hilo la EWURA tangu kupewa Mamlaka ya kuuzia umeme Zanzibar imekuwa ikipandishia viwango vikubwa ikilinganishwa na mikoa mingine ya Tanzania ambayo hununua kwa bei ya chini huku Zanzibar ikitozwa kiasi kikubwa.
Mwakilishi huyo aliyekuwa akitoa maoni yake hayo kwa hasira alisema ni vyema kwa Waziri wa wizara hiyo hivi sasa akajiandaa kulishitaki shirika hilo kwani sio lenye mamlaka ya kuiuzia umeme Zanzibar na imekuwa ikifanya biashara kinyume na sheria.
“Kwa nini Zanzibar iuziwe umeme na EWURA inawezekana kuna watu hawataki kununua umeme Zanzibar kwani gharama kuwa ni kubwa, EWURA haikupaswa kuiuzia umeme Zanzibar maana wamefungua duka la rejareja hivi sasa tutanunua mpaka lini huu umeme rejareja si wanatuumiza kusudi hawa Waziri tunaomba ukawashtaki hawa” alisema Mwakilishi huyo.
Nae Mwakilishi wa Jimbo la Ziwani, Rashid Seif, alisema inasikitisha kuona Shirika la EWURA, limejipa majukumu la kuiuzia umeme Zanzibar jambo ambalo linahitaji kuangaliwa kwani inaitoza Zanzibar gharama kubwa.
Alisema hatari iliyopo kama serikali itashindwa kuliingilia kati suala hilo linaweza kuuwa viwanda na kudhoofisha uwekezaji kwani wanaweza kukimbia baada ya kuona gharama ni kubwa.
Mwakilishi wa Kitope, Makame Mshimba, alisema matatizo ya wafanyabiashara bado suala hilo linaonekana kufanywa kuwa ni nyimbo kwani serikali imeeleza limemalizika lakini bado Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), inaendelea kuwatoza kodi mara mbili.
Alisema hiyo ni kero ambayo inahitaji serikali kuiangalia kwa umakini kwani hata Wajumbe wa Baraza hilo imeshawachosha na ni vyema kwa serikali ikafikiria kuifuta TRA isifanye kazi zake Zanzibar.
Mwakilishi huyo aliwataka Wajumbe wa baraza hilo kuhakikisha wanawatetea vizuri wananchi na sio kufanya udanganyifu kwa kukubali nyimbo za kujiridhi juu ya maslahi yao, kwani wanasahau viapo wanavyokula na ndio maana wanapoanguka katika uchaguzi hubakia wakibeba masusu ya matenga ya biashara.
Aidha, alihoji ni kwa nini serikali imekitoa kiwanda cha kuku kilichopo Mtoni kugeuzwa kuwa ni ghala la kuhifadhia saruji badala ya kutumika kwa ufugaji wa kuku ambapo walimuomba Waziri huyo kumtaja aliyepewa kiwanda hicho na alieruhusiwa kujenga mbele ya kiwanda cha maziwa.
Aidha, Wawakilishi hao pia walieleza ipo haja kwa serikali kuangalia suala la utoaji wa leseni za biashara kutokana na hivi sasa kuonekana kuna maduka mengi hayana leseni na yapo kwa ajili ya kuwahudumia wafanyakazi wa Baraza la Manispaa binafsi.
Mwakilishi wa Chambani, Hassan alisema ipo haja ya Wizara ya Biashara ikajiandaa vyema kuweka mazingira bora ya biashara hasa katika kukabiliana na tatizo la magendo ya karafuu kutokana na baadhi ya wanunuzi wa zao hilo kubuni mbinu mpya kwa wasafirishaji zao kwa kuwaongezea bei zaidi.
Mwakilishi wa Micheweni Subeit Khamis Faki akichangia bajeti hiyo alisema mazingira ya biashara bado yanahitaji kuangaliwa hasa katika ufufuaji wa viwanda.
Na Mwantanga Ame
UAMUZI wa Shirika la kudhibiti Nishati na Maji (EWURA), juu ya kuchukua jukumu la kuiuzia Zanzibar huduma ya umeme badala ya Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), umewachafua Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi na kuiomba serikali kulishitaki shirika hilo.
Wawakilishi hao walitoa kauli hiyo karibuni wakichangia hotuba ya Wizara ya Biashara, Viwanda na Masoko, iliyowasilishwa na Waziri wa Wizara hiyo Nassor Ahmed Mazrui, aliyowasilisha jana asubuhi kwa wajumbe wa baraza hilo Zanzibar.
Hapo awali Waziri huyo akiwasilisha bajeti hiyo katika maelezo yake alisema katika ukaguzi walioufanya katika baadhi ya viwanda wamebaini vimekuwa vinakabiliwa na matatizo mengi likiwemo suala la huduma ya umeme gharama zake kuwa ni kubwa.
Mwakilishi wa Wete Asaa Othman Hamad, alisema hali hiyo, serikali inapaswa kutolivumilia shirika hilo na ipo haja ya Waziri wa Nishati Zanzibar kuifungulia mashtaka taasisi hiyo.
Alisema Zanzibar hapo awali wakati inataka kutumia huduma za Shirika hilo ilifanya makubaliano na shirika la TANESCO na sio EWURA ambapo hivi sasa wamekuwa wakitakiwa kununua huduma hiyo huko.
Alisema huo ni ukiukwaji mkubwa wa mkataba wa makubaliano juu ya ununuzi wa huduma hiyo ya umeme kwani hawaoni haja ya kununuliwa katika duka la rejareja wakati makubaliano ni katika duka la jumla.
Alisema inawezekana ikawa shirika hilo linafanya kwa makusudi ili kuwakatisha tamaa watumiaji wa huduma hiyo ya umeme, jambo ambalo hivi sasa watu wengi wanashindwa kuwa na huduma hiyo majumbani na baadhi ya sehemu za uzalishaji kulikosababishwa na gaharama kuwa ni kubwa.
Alisema Shirika hilo la EWURA tangu kupewa Mamlaka ya kuuzia umeme Zanzibar imekuwa ikipandishia viwango vikubwa ikilinganishwa na mikoa mingine ya Tanzania ambayo hununua kwa bei ya chini huku Zanzibar ikitozwa kiasi kikubwa.
Mwakilishi huyo aliyekuwa akitoa maoni yake hayo kwa hasira alisema ni vyema kwa Waziri wa wizara hiyo hivi sasa akajiandaa kulishitaki shirika hilo kwani sio lenye mamlaka ya kuiuzia umeme Zanzibar na imekuwa ikifanya biashara kinyume na sheria.
“Kwa nini Zanzibar iuziwe umeme na EWURA inawezekana kuna watu hawataki kununua umeme Zanzibar kwani gharama kuwa ni kubwa, EWURA haikupaswa kuiuzia umeme Zanzibar maana wamefungua duka la rejareja hivi sasa tutanunua mpaka lini huu umeme rejareja si wanatuumiza kusudi hawa Waziri tunaomba ukawashtaki hawa” alisema Mwakilishi huyo.
Nae Mwakilishi wa Jimbo la Ziwani, Rashid Seif, alisema inasikitisha kuona Shirika la EWURA, limejipa majukumu la kuiuzia umeme Zanzibar jambo ambalo linahitaji kuangaliwa kwani inaitoza Zanzibar gharama kubwa.
Alisema hatari iliyopo kama serikali itashindwa kuliingilia kati suala hilo linaweza kuuwa viwanda na kudhoofisha uwekezaji kwani wanaweza kukimbia baada ya kuona gharama ni kubwa.
Mwakilishi wa Kitope, Makame Mshimba, alisema matatizo ya wafanyabiashara bado suala hilo linaonekana kufanywa kuwa ni nyimbo kwani serikali imeeleza limemalizika lakini bado Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), inaendelea kuwatoza kodi mara mbili.
Alisema hiyo ni kero ambayo inahitaji serikali kuiangalia kwa umakini kwani hata Wajumbe wa Baraza hilo imeshawachosha na ni vyema kwa serikali ikafikiria kuifuta TRA isifanye kazi zake Zanzibar.
Mwakilishi huyo aliwataka Wajumbe wa baraza hilo kuhakikisha wanawatetea vizuri wananchi na sio kufanya udanganyifu kwa kukubali nyimbo za kujiridhi juu ya maslahi yao, kwani wanasahau viapo wanavyokula na ndio maana wanapoanguka katika uchaguzi hubakia wakibeba masusu ya matenga ya biashara.
Aidha, alihoji ni kwa nini serikali imekitoa kiwanda cha kuku kilichopo Mtoni kugeuzwa kuwa ni ghala la kuhifadhia saruji badala ya kutumika kwa ufugaji wa kuku ambapo walimuomba Waziri huyo kumtaja aliyepewa kiwanda hicho na alieruhusiwa kujenga mbele ya kiwanda cha maziwa.
Aidha, Wawakilishi hao pia walieleza ipo haja kwa serikali kuangalia suala la utoaji wa leseni za biashara kutokana na hivi sasa kuonekana kuna maduka mengi hayana leseni na yapo kwa ajili ya kuwahudumia wafanyakazi wa Baraza la Manispaa binafsi.
Mwakilishi wa Chambani, Hassan alisema ipo haja ya Wizara ya Biashara ikajiandaa vyema kuweka mazingira bora ya biashara hasa katika kukabiliana na tatizo la magendo ya karafuu kutokana na baadhi ya wanunuzi wa zao hilo kubuni mbinu mpya kwa wasafirishaji zao kwa kuwaongezea bei zaidi.
Mwakilishi wa Micheweni Subeit Khamis Faki akichangia bajeti hiyo alisema mazingira ya biashara bado yanahitaji kuangaliwa hasa katika ufufuaji wa viwanda.
UAZISHWAJI CHUO CHA ANGA UBAHARIA WAIVA.
Uanzishwaji chuo cha anga, ubaharia waiva
Na Mwantanga Ame
WAZIRI wa Miundombinu na Mawasiliano, Hamad Masoud amesema kuanzishwa Chuo cha Usafiri wa Anga na Ubaharia kunalenga kuleta mageuzi ya kiajira kwa vijana wa Kizanzibari watakasoma fani hizo.
Masoud alisema hayo jana ofisi za Mamlaka ya Viwanja wa Ndege Zanzibar, alipokuwa akizindua kamati mbili za kusimamia uanzishwaji wa vyuo hivyo, ambazo zitatoa mapendekezo serikalini namna ya kufanikisha mpango huo.
Alisema sekta ya mawasiliano inahitaji mabadiliko ambayo yataleta mbinu mpya za kisasa na kitaalamu, hivyo Zanzibar lazima ichangamkie mabadiliko ili isiachwe nyuma kwa kuanzisha vyuo vitakavyoweza kuwafunza fani hizo vijana.
Waziri huyo alisema kuwepo vyuo hivyo kutawafanya vijana wa Zanzibar kuzitumia fursa za ajira za fani hizo bila ya wasiwasi, kwani wengi wao tayari ni wenye kuishi katika visiwa ambavyo wananchi wake hutegemea usafiri wa bahari pamoja na ndege.
Alifahamisha kuwa hivi sasa Zanzibar imekuwa na mabaharia wengi wanaofanya kazi katika meli mbali mbali za kigeni duniani lakini tatizo kubwa linalowakabili ni elimu ya kutosha juu ya shughuli hizo, jambo ambalo linaweza kuwasababishia kutofahamu haki zao wakiwa kazini.
Waziri huyo alisema kuwepo kwa vyuo hivyo hapa Zanzibar kutasaidia kupatikana kwa faida kadhaa ikiwemo kuokoa fedha nyingi ambazo zimekuwa zikitumika kuwasomeshea vijana nje ya Zanzibar.
Alisema nia ya serikali ni kuhakikisha inaleta mabadiliko katika sekta ya mawasiliano ya anga na bahari, ikiwa pamoja na kufungua milango kwa taasisi za nje kushirikiana na serikali kuwekeza kwa pamoja.
Alisema kamati hizo zitazingatia hadidu rejea tisa ikiwemo ya kuangalia kwa kina taratibu za kuanzisha chuo cha Usafiri wa Anga na Ubaharia hapa Zanzibar, kupendekeza mfumo wa uendeshaji wa Chuo hicho na kuangalia kwa kina soko la Chuo hicho hapa Zanzibar na nje ya nchi.
Maeneo mengine ambayo kamati hizo itazingatia ni kuendeleza taratibu zitazotumika katika kutoa mafunzo katika chuo, kupendekeza mipango ya muda mfupi na muda mrefu ya kitaaluma na uendeshaji wa vyuo hivyo na kupendekeza utaratibu za kutambuliwa Chuo hicho duniani na taratibu za kuingia kwenye ‘White list’ ya I.M.O.
Kamati itakayosimamia uanzishwaji wa vyuo hivyo, Chuo cha Usafiri wa Anga, Mwenyekiti wake ni Abdulla Hussein Kombo, wajumbe ni Kepteni Said Ndumbugani, Abdulhalym M. Sururu, Said Sumry, Seif Said Issa, Kapten Khamis Suleiman na Katibu wake ni Zaid R. Taufik.
Upande wa Chuo cha Mabaharia, kamati hiyo inaundwa na Mwenyekiti Abdulla Hussein Kombo, wajumbe ni Abdulrahman Chande, Injinia Haji Vuai Ussi, Salma Suleiman Omar, Kepteni Alhaj Sururu, Said Salim Bakhressa na Katibu wake ni Zaid R. Taufik.
Mkurugenzi wa Mamlaka ya Anga, Said Ndumbugani, akitoa shukrani zake alisema dhamira ya mamlaka hiyo ni kuona inainua sekta ya usafiri wa anga ambapo watahakikisha wanafanikisha mpango huo wa serikali kwani utawawezesha Wazanzibari kupata elimu hiyo hapa nchini.
Katika hatua nyengine waziri huyo alisema Zanzibar inajiandaa kuanzisha shirika lake la ndege, huku nchi kadhaa zikiwa tayari kushirikiana katika mpango huo zikiwemo Falme za Kiarabu, Malaysia, na Wazanzibari walioko nchini Oman huku mazungumzo yakiendelea katika kufanikisha mpango wa kuanzishwa shirika hilo.
Na Mwantanga Ame
WAZIRI wa Miundombinu na Mawasiliano, Hamad Masoud amesema kuanzishwa Chuo cha Usafiri wa Anga na Ubaharia kunalenga kuleta mageuzi ya kiajira kwa vijana wa Kizanzibari watakasoma fani hizo.
Masoud alisema hayo jana ofisi za Mamlaka ya Viwanja wa Ndege Zanzibar, alipokuwa akizindua kamati mbili za kusimamia uanzishwaji wa vyuo hivyo, ambazo zitatoa mapendekezo serikalini namna ya kufanikisha mpango huo.
Alisema sekta ya mawasiliano inahitaji mabadiliko ambayo yataleta mbinu mpya za kisasa na kitaalamu, hivyo Zanzibar lazima ichangamkie mabadiliko ili isiachwe nyuma kwa kuanzisha vyuo vitakavyoweza kuwafunza fani hizo vijana.
Waziri huyo alisema kuwepo vyuo hivyo kutawafanya vijana wa Zanzibar kuzitumia fursa za ajira za fani hizo bila ya wasiwasi, kwani wengi wao tayari ni wenye kuishi katika visiwa ambavyo wananchi wake hutegemea usafiri wa bahari pamoja na ndege.
Alifahamisha kuwa hivi sasa Zanzibar imekuwa na mabaharia wengi wanaofanya kazi katika meli mbali mbali za kigeni duniani lakini tatizo kubwa linalowakabili ni elimu ya kutosha juu ya shughuli hizo, jambo ambalo linaweza kuwasababishia kutofahamu haki zao wakiwa kazini.
Waziri huyo alisema kuwepo kwa vyuo hivyo hapa Zanzibar kutasaidia kupatikana kwa faida kadhaa ikiwemo kuokoa fedha nyingi ambazo zimekuwa zikitumika kuwasomeshea vijana nje ya Zanzibar.
Alisema nia ya serikali ni kuhakikisha inaleta mabadiliko katika sekta ya mawasiliano ya anga na bahari, ikiwa pamoja na kufungua milango kwa taasisi za nje kushirikiana na serikali kuwekeza kwa pamoja.
Alisema kamati hizo zitazingatia hadidu rejea tisa ikiwemo ya kuangalia kwa kina taratibu za kuanzisha chuo cha Usafiri wa Anga na Ubaharia hapa Zanzibar, kupendekeza mfumo wa uendeshaji wa Chuo hicho na kuangalia kwa kina soko la Chuo hicho hapa Zanzibar na nje ya nchi.
Maeneo mengine ambayo kamati hizo itazingatia ni kuendeleza taratibu zitazotumika katika kutoa mafunzo katika chuo, kupendekeza mipango ya muda mfupi na muda mrefu ya kitaaluma na uendeshaji wa vyuo hivyo na kupendekeza utaratibu za kutambuliwa Chuo hicho duniani na taratibu za kuingia kwenye ‘White list’ ya I.M.O.
Kamati itakayosimamia uanzishwaji wa vyuo hivyo, Chuo cha Usafiri wa Anga, Mwenyekiti wake ni Abdulla Hussein Kombo, wajumbe ni Kepteni Said Ndumbugani, Abdulhalym M. Sururu, Said Sumry, Seif Said Issa, Kapten Khamis Suleiman na Katibu wake ni Zaid R. Taufik.
Upande wa Chuo cha Mabaharia, kamati hiyo inaundwa na Mwenyekiti Abdulla Hussein Kombo, wajumbe ni Abdulrahman Chande, Injinia Haji Vuai Ussi, Salma Suleiman Omar, Kepteni Alhaj Sururu, Said Salim Bakhressa na Katibu wake ni Zaid R. Taufik.
Mkurugenzi wa Mamlaka ya Anga, Said Ndumbugani, akitoa shukrani zake alisema dhamira ya mamlaka hiyo ni kuona inainua sekta ya usafiri wa anga ambapo watahakikisha wanafanikisha mpango huo wa serikali kwani utawawezesha Wazanzibari kupata elimu hiyo hapa nchini.
Katika hatua nyengine waziri huyo alisema Zanzibar inajiandaa kuanzisha shirika lake la ndege, huku nchi kadhaa zikiwa tayari kushirikiana katika mpango huo zikiwemo Falme za Kiarabu, Malaysia, na Wazanzibari walioko nchini Oman huku mazungumzo yakiendelea katika kufanikisha mpango wa kuanzishwa shirika hilo.
WAZANZIBAR WATAKA TAASISI YA KUPAMBANA NA RUSHWA.
Wazanzibari wataka taasisi ya kupambana na rushwa
Na Kassim Kassim, TUDARCO
SERIKALI ya Mapinduzi ya Zanzibar iliyo chini ya muundo wa Umoja wa Kitaifa, imeshauriwa kuwa umefika wakati wa kuwa na taasisi yake itakayodhibiti rushwa na mambo ya kifisadi.
Ushauri huo umetolewa na baadhi ya washiriki wa kongamano la siku moja lililoandaliwa na Jumuia ya Waandishi wa Habari za Maendeleo Zanzibar (WAHAMAZA), lililofanyika ukumbi wa Beyet el Yamin Malindi mjini hapa.
Mmoja wa washiriki wa kongamano hilo, Mohammed Yussuf alisema Zanzibar imekuwa ikikabiliwa na tatizo la rushwa na vitendo vya kifisadi kwa baadhi ya watendaji serikalini, hivyo wakati umefika kwa serikali kuvikomesha vitendo hivyo kwa kuwa na taasisi maalum itakayokabiliana navyo.
"Serikali ya Umoja wa kitaifa ni vyema ikaangalia uwezekano wa kuunda ‘Anti Corruption Commission’ maana rushwa kwa baadhi ya watendaji wa serikali imetawala na kila siku wanajijengea majumba na miradi ya gharama ambayo hayaendani na kipato chao", alisema Yussuf.
Aidha mdau huyo wa kongamano alisema serikali na hasa mawaziri kupunguza matumizi ya ununuzi wa gari za kifahari ambazo zina gharama kubwa zaidi ikilinganishwa na gari anayotumia Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa au waziri Mkuu wa Sweden.
Alisema vigogo wa serikali wakiwemo mawaziri, manaibu na baadhi ya maofisa wakuu wanatumia gari aina ya ‘Prado’ ambazo ni ghali zaidi ikilinganishwa na gari aina ya Volvo inayotumiwa na Ban Ki-moon katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa na waziri Mkuu wa Sweden.
Kwa upande mwengine aliipongeza serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa juhudi zake za kuleta umoja miongoni mwa wananchi wa Zanzibar hasa baada ya kukubali kuundwa serikali ya Umoja wa Kitaifa baada ya uchaguzi mkuu iliyotokana na zoezi la kura ya maoni lililofanyika mwaka mmoja uliopita.
Na Mwandishi wa Habari mkongwe visiwani hapa, Said Salim Said, akitoa mada alisema ni vyema serikali ikabuni utaratibu wa kuwa na mafunzo ya ndani kwa watendaji wa serikali, ambayo yatakuza uwajibikaji na kuwa wepesi wa kuwahudumia wananchi.
"Serikali ya Zanzibar ni vyema ikawa na ‘in house training’, kwa ajili ya kuinua uwajibikaji wa watendaji wake, maana sasa unaweza kwenda katika ofisi fulani ukapata majibu yasiyoridhisha, hivyo ni vyema serikali ikaandaa mafunzo ya ndani kuinua uwajibikaji wa watendaji hao", alisema mkongwe huyo.
Kwa upande wake Mhadhiri wa Chuo cha Taifa cha Zanzibar (SUZA), Ali Vuai aliiomba serikali kupitia upya mpango wa maendeleo wa Zanzibar ujulikanao kama MKUZA ili uweze kuendana na azma yake ya kuinua hali za wananchi wa kawaida.
Alisema serikali ni vyema ikapeleka mpango huo kwa wananchi ili waujadili na kuutolea ufafanuzi wa namna ya kuweza kuutekeleza na sio kuambiwa tu utainua vipi hali za wananchi ambao wengi wao ni masikini.
"Serikali ni muhimu ikapitia upya mpango wake wa maendeleo ili uweze kutekelezeka kama ulivyokusudiwa kwa kuwatoa wananchi kwenye umasikini, serikali ipeleke mpango huo kwa wananchi waweze kuujadili na kuutolea mapendekezo yao."
Aidha alipendekeza kwa serikali kuachana na mfumo wa kutegemea mapato kutoka kwenye kodi ya ongezeko la thamani (VAT) bali iangalie uwezekano wa kutoza kodi kwa makampuni (corporate tax) ambayo mengi yao hukwepa kulipa kodi kwa kubadilisha majina kila baada ya muda na kupelekea kwa serikali kukosa mapato yanayoweza kuondoa umasikini kwa wananchi.
Kongamano hilo mgeni rasmi alikuwa Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Maalim Seif Sharif Hamad.
Na Kassim Kassim, TUDARCO
SERIKALI ya Mapinduzi ya Zanzibar iliyo chini ya muundo wa Umoja wa Kitaifa, imeshauriwa kuwa umefika wakati wa kuwa na taasisi yake itakayodhibiti rushwa na mambo ya kifisadi.
Ushauri huo umetolewa na baadhi ya washiriki wa kongamano la siku moja lililoandaliwa na Jumuia ya Waandishi wa Habari za Maendeleo Zanzibar (WAHAMAZA), lililofanyika ukumbi wa Beyet el Yamin Malindi mjini hapa.
Mmoja wa washiriki wa kongamano hilo, Mohammed Yussuf alisema Zanzibar imekuwa ikikabiliwa na tatizo la rushwa na vitendo vya kifisadi kwa baadhi ya watendaji serikalini, hivyo wakati umefika kwa serikali kuvikomesha vitendo hivyo kwa kuwa na taasisi maalum itakayokabiliana navyo.
"Serikali ya Umoja wa kitaifa ni vyema ikaangalia uwezekano wa kuunda ‘Anti Corruption Commission’ maana rushwa kwa baadhi ya watendaji wa serikali imetawala na kila siku wanajijengea majumba na miradi ya gharama ambayo hayaendani na kipato chao", alisema Yussuf.
Aidha mdau huyo wa kongamano alisema serikali na hasa mawaziri kupunguza matumizi ya ununuzi wa gari za kifahari ambazo zina gharama kubwa zaidi ikilinganishwa na gari anayotumia Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa au waziri Mkuu wa Sweden.
Alisema vigogo wa serikali wakiwemo mawaziri, manaibu na baadhi ya maofisa wakuu wanatumia gari aina ya ‘Prado’ ambazo ni ghali zaidi ikilinganishwa na gari aina ya Volvo inayotumiwa na Ban Ki-moon katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa na waziri Mkuu wa Sweden.
Kwa upande mwengine aliipongeza serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa juhudi zake za kuleta umoja miongoni mwa wananchi wa Zanzibar hasa baada ya kukubali kuundwa serikali ya Umoja wa Kitaifa baada ya uchaguzi mkuu iliyotokana na zoezi la kura ya maoni lililofanyika mwaka mmoja uliopita.
Na Mwandishi wa Habari mkongwe visiwani hapa, Said Salim Said, akitoa mada alisema ni vyema serikali ikabuni utaratibu wa kuwa na mafunzo ya ndani kwa watendaji wa serikali, ambayo yatakuza uwajibikaji na kuwa wepesi wa kuwahudumia wananchi.
"Serikali ya Zanzibar ni vyema ikawa na ‘in house training’, kwa ajili ya kuinua uwajibikaji wa watendaji wake, maana sasa unaweza kwenda katika ofisi fulani ukapata majibu yasiyoridhisha, hivyo ni vyema serikali ikaandaa mafunzo ya ndani kuinua uwajibikaji wa watendaji hao", alisema mkongwe huyo.
Kwa upande wake Mhadhiri wa Chuo cha Taifa cha Zanzibar (SUZA), Ali Vuai aliiomba serikali kupitia upya mpango wa maendeleo wa Zanzibar ujulikanao kama MKUZA ili uweze kuendana na azma yake ya kuinua hali za wananchi wa kawaida.
Alisema serikali ni vyema ikapeleka mpango huo kwa wananchi ili waujadili na kuutolea ufafanuzi wa namna ya kuweza kuutekeleza na sio kuambiwa tu utainua vipi hali za wananchi ambao wengi wao ni masikini.
"Serikali ni muhimu ikapitia upya mpango wake wa maendeleo ili uweze kutekelezeka kama ulivyokusudiwa kwa kuwatoa wananchi kwenye umasikini, serikali ipeleke mpango huo kwa wananchi waweze kuujadili na kuutolea mapendekezo yao."
Aidha alipendekeza kwa serikali kuachana na mfumo wa kutegemea mapato kutoka kwenye kodi ya ongezeko la thamani (VAT) bali iangalie uwezekano wa kutoza kodi kwa makampuni (corporate tax) ambayo mengi yao hukwepa kulipa kodi kwa kubadilisha majina kila baada ya muda na kupelekea kwa serikali kukosa mapato yanayoweza kuondoa umasikini kwa wananchi.
Kongamano hilo mgeni rasmi alikuwa Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Maalim Seif Sharif Hamad.
JAMII YATAKIWA KUUHESHIMU MWEZI WA RAMADHANI.
Jamii yatakiwa kuuheshimu mwezi wa Ramadhani
Na Mwantanga Ame
OFISI ya Mufti Zanzibar, imeitaka jamii kuacha vitendo viovu ikiwemo kuvaa mavazi yasiostahili ili kuuheshimu mwezi Mtukufu wa Ramadhan.
Taarifa iliyosambazwa jana kwa vyombo vya habari hapa nchini na Katibu wa Afisi hiyo Sheikh Fadhil Soraga, ilieleza kuwa ni vyema kwa jamii kuupa heshima mwezi huo kwa kuacha vitendo viovu wakati funga hiyo ikiwa inaendelea.
Waumini wa dini ya kiislamu wameanza kufunga mwezi wa Ramadhan jana ikiwa ni utekelezaji wa nguzo ya nne katika dini hiyo ambapo Zanzibar ni asilimia kubwa ya waumini hao.
Sheikh Soraga, alisema suala la kuupa heshima mwezi huo ni jambo la msingi kwa wananchi wote wa Zanzibar kujizuia na vitendo viovu ambavyo vitaweza kubatilisha saumu za wengine ikiwa ni hatua itayosaidia funga hiyo kufanyika kwa utulivu.
Alisema si jambo la busara kwa watu wenye tabia ya kupenda kufanya mambo maovu ama kuvaa mavazi yasiyokuwa na heshima katika mwezi huu.
Hata hivyo, Sheikh Soraga, amewapongeza wananchi kwa kutoa ushirikiano wao kwa Afisi hiyo kwa kuipatia taarifa za kuandama kwa mwezi baada ya kuuona katika maeneo yao.
Alisema wananchi hao waliweza kuuona mwezi huo katika maeneo ya Taveta, Nyerere, Jambiani na Mombasa ingawa katika ukanda wa pwani ya Afrika Mashariki ulishindwa kuonekana kutokana na kuwepo kwa mawingu mazito baada ya kuzama kwa jua.
Na Mwantanga Ame
OFISI ya Mufti Zanzibar, imeitaka jamii kuacha vitendo viovu ikiwemo kuvaa mavazi yasiostahili ili kuuheshimu mwezi Mtukufu wa Ramadhan.
Taarifa iliyosambazwa jana kwa vyombo vya habari hapa nchini na Katibu wa Afisi hiyo Sheikh Fadhil Soraga, ilieleza kuwa ni vyema kwa jamii kuupa heshima mwezi huo kwa kuacha vitendo viovu wakati funga hiyo ikiwa inaendelea.
Waumini wa dini ya kiislamu wameanza kufunga mwezi wa Ramadhan jana ikiwa ni utekelezaji wa nguzo ya nne katika dini hiyo ambapo Zanzibar ni asilimia kubwa ya waumini hao.
Sheikh Soraga, alisema suala la kuupa heshima mwezi huo ni jambo la msingi kwa wananchi wote wa Zanzibar kujizuia na vitendo viovu ambavyo vitaweza kubatilisha saumu za wengine ikiwa ni hatua itayosaidia funga hiyo kufanyika kwa utulivu.
Alisema si jambo la busara kwa watu wenye tabia ya kupenda kufanya mambo maovu ama kuvaa mavazi yasiyokuwa na heshima katika mwezi huu.
Hata hivyo, Sheikh Soraga, amewapongeza wananchi kwa kutoa ushirikiano wao kwa Afisi hiyo kwa kuipatia taarifa za kuandama kwa mwezi baada ya kuuona katika maeneo yao.
Alisema wananchi hao waliweza kuuona mwezi huo katika maeneo ya Taveta, Nyerere, Jambiani na Mombasa ingawa katika ukanda wa pwani ya Afrika Mashariki ulishindwa kuonekana kutokana na kuwepo kwa mawingu mazito baada ya kuzama kwa jua.
UMEME WAPELEKA NEEMA YA UWEKEZAJI PEMBA.
Umeme wapeleka neema ya uwekezaji Pemba
Na Ali Haji Mwadini, Pemba
IKIWA ni mwaka mmoja sasa tokea kuzinduliwa kwa umeme wa uhakika kutoka Tanga, tayari jumla ya makampuni kumi (10) ya uwekezaji yameshapeleka maombi yao kwa Mamlaka ya Ukuzaji vitega Uchumi (ZIPA), ili waweze kuruhusiwa kuwekeza katika sekta mbali mbali kisiwani Pemba.
Akizungumza na mwandishi wa habari hizi, Afisini kwake Chake Chake Pemba, Mkurugenzi Mkaazi wa Mamlaka hiyo Pemba, Fadhila Hassan Abdallah, alisema kuwa wawekezaji hao wameonesha nia hiyo kutokana na kuwepo kwa umeme wa uhakika kisiwani humo.
Alisema kuwepo kwa umeme wa uhakika kisiwani Pemba, ndiko kulikotoa hamu kwa wawekazaji mbali mbali na kutuma maombi yao, ambapo hapo awali kasi ya wawekezaji ilikuwa ndogo.
“Kwa sasa wawekezaji wanaongezeka, tayari jumla ya wawekezaji 10 kutoka sehemu mbali mbali, wameshatuma maombi yao kwetu na tunayafanyika kazi kwa mujibu wa sheria na taratibu za nchi, hii imetokana na kupatikana kwa umeme wa uhakika” alielezea Fadhila.
Aliyataja makampuni hayo kuwa ni Barrick International, GS limited, MS Company, Medical Tourism, Pemba Bottlers Company, Holding Company, Kigomasha Ecology, AQUA farms, Fundu Lagon na Manta reef, ambayo yanatoka nchi za Kenya, Marekani, Sweden, Ujerumani na Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE).
Alifafanua kuwa pamoja na kuwepo kwa umeme wa uhakika, chengine kilichowavuti wawekezaji hao ni suala zima la amani na utulivu uliotawala hapa Zanzibar na hasa baada ya kumalizika kwa uchaguzi mkuu mwaka jana.
Akizungumzia juhudi zinazofanywa na ZIPA katika kuwavutia wawekezaji, Fadhila alibainisha kuwa, wameanzisha kituo kimoja cha ushirikiano (One stop centre) ambacho kinawajumuisha wataalamu kutoka Idara za Uhamiaji, Ardhi kwa lengo la kuweka mazingira mazuri ambayo yatawavutia wawekezaji kutoka mataifa mbali mbali.
“Wawekezaji hawa wanataka kuwekeza katika kutayarisha maji ya Chupa, Mwani, kujenga Skuli, kusindika matunda na kuimarisha utalii kwa kuweka mazingira mazuri katika mahoteli yao” alisema Mkurugenzi Mkaazi.
Akitolea mfano kijiji ya Kiuyu Mbuyuni Micheweni Pemba, kilichokataa utalii, alisema kuwa mamlaka inakabiliana na changamoto kubwa kutoka kwa wanajamii kwa kukataa kuwekezwa katika vijiji vyao, hivyo mamlaka inajipanga vizuri ili kuendeleza kasi yake ya utowaji taaluma kwa jamii kisiwani Pemba.
Hivyo alitoa wito kwa jamii, kuunga mkono juhudi za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa kutoa mashirikiano mazuri kwa wawekezaji wakati wote na kusisitiza kuwa kuwepo kwa wawekezaji kunapelekea wananchi kupata fursa ya kuuza mazao yao mbali mbali na kupata misaada ya kimaendeleo kutoka kwa wawekezaji kama wanavyofaidika watu wa Wambaa, ambapo Fundu lagon wameanzisha shamba darasa kwa lengo la kufundisha wanajamii juu ya kutayarisha mboga mboga.
Na Ali Haji Mwadini, Pemba
IKIWA ni mwaka mmoja sasa tokea kuzinduliwa kwa umeme wa uhakika kutoka Tanga, tayari jumla ya makampuni kumi (10) ya uwekezaji yameshapeleka maombi yao kwa Mamlaka ya Ukuzaji vitega Uchumi (ZIPA), ili waweze kuruhusiwa kuwekeza katika sekta mbali mbali kisiwani Pemba.
Akizungumza na mwandishi wa habari hizi, Afisini kwake Chake Chake Pemba, Mkurugenzi Mkaazi wa Mamlaka hiyo Pemba, Fadhila Hassan Abdallah, alisema kuwa wawekezaji hao wameonesha nia hiyo kutokana na kuwepo kwa umeme wa uhakika kisiwani humo.
Alisema kuwepo kwa umeme wa uhakika kisiwani Pemba, ndiko kulikotoa hamu kwa wawekazaji mbali mbali na kutuma maombi yao, ambapo hapo awali kasi ya wawekezaji ilikuwa ndogo.
“Kwa sasa wawekezaji wanaongezeka, tayari jumla ya wawekezaji 10 kutoka sehemu mbali mbali, wameshatuma maombi yao kwetu na tunayafanyika kazi kwa mujibu wa sheria na taratibu za nchi, hii imetokana na kupatikana kwa umeme wa uhakika” alielezea Fadhila.
Aliyataja makampuni hayo kuwa ni Barrick International, GS limited, MS Company, Medical Tourism, Pemba Bottlers Company, Holding Company, Kigomasha Ecology, AQUA farms, Fundu Lagon na Manta reef, ambayo yanatoka nchi za Kenya, Marekani, Sweden, Ujerumani na Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE).
Alifafanua kuwa pamoja na kuwepo kwa umeme wa uhakika, chengine kilichowavuti wawekezaji hao ni suala zima la amani na utulivu uliotawala hapa Zanzibar na hasa baada ya kumalizika kwa uchaguzi mkuu mwaka jana.
Akizungumzia juhudi zinazofanywa na ZIPA katika kuwavutia wawekezaji, Fadhila alibainisha kuwa, wameanzisha kituo kimoja cha ushirikiano (One stop centre) ambacho kinawajumuisha wataalamu kutoka Idara za Uhamiaji, Ardhi kwa lengo la kuweka mazingira mazuri ambayo yatawavutia wawekezaji kutoka mataifa mbali mbali.
“Wawekezaji hawa wanataka kuwekeza katika kutayarisha maji ya Chupa, Mwani, kujenga Skuli, kusindika matunda na kuimarisha utalii kwa kuweka mazingira mazuri katika mahoteli yao” alisema Mkurugenzi Mkaazi.
Akitolea mfano kijiji ya Kiuyu Mbuyuni Micheweni Pemba, kilichokataa utalii, alisema kuwa mamlaka inakabiliana na changamoto kubwa kutoka kwa wanajamii kwa kukataa kuwekezwa katika vijiji vyao, hivyo mamlaka inajipanga vizuri ili kuendeleza kasi yake ya utowaji taaluma kwa jamii kisiwani Pemba.
Hivyo alitoa wito kwa jamii, kuunga mkono juhudi za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa kutoa mashirikiano mazuri kwa wawekezaji wakati wote na kusisitiza kuwa kuwepo kwa wawekezaji kunapelekea wananchi kupata fursa ya kuuza mazao yao mbali mbali na kupata misaada ya kimaendeleo kutoka kwa wawekezaji kama wanavyofaidika watu wa Wambaa, ambapo Fundu lagon wameanzisha shamba darasa kwa lengo la kufundisha wanajamii juu ya kutayarisha mboga mboga.
Monday, 25 July 2011
JK AONGOZA WATANZANIA KUKUMBUKA MASHAJAA
JK aongoza Watanzania kukumbuka mashujaa
Na Rajab Mkasaba, Ikulu
RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Jakaya Mrisho Kikwete, amewaongoza maelfu ya wananchi na viongozi mbali mbali wa kitaifa, akiwemo Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Ali Mohamed Shein, kuadhimisha siku ya kumbukumbu ya Mashujaa.
Maadhimisho hayo yamefanyika jana katika viwanja vya Naliendele Mjini Mtwara eneo ambalo pana makaburi ya mashujaa waliopigana vita vya Msumbiji.
Miongoni mwa viongozi waliohudhuria maadhimisho hayo ni Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Mohamed Gharib Bilali, Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Balozi Seif Idd, Waziri wa Ulinzi na Majeshi ya Kujenga Taifa, Dk. Hussein Mwinyi pamoja na Waziri wa Ulinzi wa Msumbiji, Philipe Nyasi.
Wengine ni Waziri Kiongozi Mstaafu wa Zanzibar, Ramadhan Haji, baadhi ya Mawaziri wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar na Serikali ya Jamhuri ya Muungano, Wakuu wa vikosi vya Ulinzi wa Tanzania na Msumbiji, Mabalozi wanaoziwakilisha nchi zao Tanzania, Majenerali wastaafu waliopigana vita vya Msumbiji pamoja na vita vya dunia na viongozi wengineo.
Katika maadhimisho hayo kama ilivyo kawaida baadhi ya viongozi akiwemo Rais Kikwete waliweka silaha za asili ambapo kwa uande wake aliweka Mkuki na Ngao, Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Davis Mwamunyange aliweka sime, Kiongozi wa Mabalozi, Balozi wa DRC, Balozi Juma Khalfan aliweka shada la maua ambapo Meya wa Manispaa ya Mtwara Mikindani Mstahiki Suleiman Mtalika aliweka upinde na mshale.
Baada ya tukio hilo dua na sala kutoka kwa viongozi wa Dini zilizomwa ambapo Sheikh Jamaldin alisoma dua kwa upande wa Waislamu, Mchungaji Lucas Mendule aliwakilisha Kanisa la CCT na Kanisa Katoliki liliwakilishwa na Padri Gabriel Mule.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete pamoja na baadhi ya viongozi wengine wakuu walitembelea makaburi ya mashujaa hao na baadae kuwasalimia wananchi waliohudhuria maadhimisho hayo, ambapo katika salamu zake Rais Kikwete alieleza kuwa kila mwaka Taifa limekuwa na utaratibu wa kuhifadhi kumbukumbu za mashujaa na kutoa pongezi kwa wananchi wengi kujitokeza katika maadhimisho hayo.
Rais Kikwete alisema kuwa kabla ya sherehe hizo kufanywa tarehe hiyo ya jana hapo mwanzo zilikuwa zikifanyika Septemba mosi kutokana na kumbukumbu za kuwapokea Majeshi kwa ushindi walioupata huko nchini Uganda.
Alisema kuwa hivi sasa kila ifikipo tarehe 25 husherehekea maisha ya wakombozi hao kutokana na juhudi kubwa walizozifanya katika kuikomboa nchi ya Msumbiji na sio kusherehekea kufa kwao.
Akieleza historia ya mashujaa hao kwa ufupi, Rais Kikwete alisema kuwa wanajeshi wa Tanzania waliokufa nchini Masumbiji katika jitihada za kuikomboa nchi hiyo kutoka kwa Wakoloni wa Kireno.
Alieleza kuwa Tanzania ilitoa msaada mkubwa katika vita hivyo kutokana na kiongozi wa FRELIMO wakati huo hayati Samora Mashel kumuomba hayati Mwalimu Nyerere kusaidiwa mafunzo na hatimae Majeshi ambapo pia, baada ya ukombozi huo kulitokea watu wachache waliokuwa hawakufurahishwa na ukombozi huo na ndipo walipowatumia waasi wa RENAMO na kuanzisha vita vingine.
Alieleza kuwa katika mapambano ambapo hatimae walisambaratishwa na Majeshi ya Msumbiji kwa mashirikiano na Majeshi ya Tanzania na ndipo baadhi ya wanajeshi wa Tanzania walipoteza maisha katika vita hivyo.
Aidha, alieleza kuwa Mashujaa hao awali walizikwa nchini Msumbiji na baadae ndipo ikaamuliwa kuzikwa katika eneo hilo ambapo pia, alitumia nafasi hiyo kutoa pongezi kwa Jeshi la Tanzania kwa kuwawekea mazingira mazuri mashujaa hao.
Nae Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapainduzi, Dk. Ali Mohamed Shein alitoa pongezi kwa wananchi wa Mtwara kwa kujitokeza kwa wingi katika maadhimisho hayo na kuwapa salamu za wananchi wa Zanzibar.
Nae Waziri wa Ulinzi wa Msumbiji alieleza kuwa uhuru wa Msumbiji ulitokana na damu za Mashujaa hao na kupelekea nchini yao hivi sasa kuendelea kuwa na amani na utulivu mkubwa.
Baada ya hapo viongozi hao wakuu kwa pamoja pamoja na viongozi wengine wakiongozwa na Amiri Jeshi Mkuu, Rais Jakaya Mrisho Kikwete walitembelea nyumba ya Makumbusho ya Naliendele iliyopo katika eneo hilo ambapo mna vifaa mbali mbali vilivyotumiwa na mashujaa hao katika ukumbozi wa Msumbiji. Katika maadhimisho hayo mizinga ilipigwa pamoja na wimbo wa Taifa sambamba na kutolewa salamu za Rais.
Na Rajab Mkasaba, Ikulu
RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Jakaya Mrisho Kikwete, amewaongoza maelfu ya wananchi na viongozi mbali mbali wa kitaifa, akiwemo Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Ali Mohamed Shein, kuadhimisha siku ya kumbukumbu ya Mashujaa.
Maadhimisho hayo yamefanyika jana katika viwanja vya Naliendele Mjini Mtwara eneo ambalo pana makaburi ya mashujaa waliopigana vita vya Msumbiji.
Miongoni mwa viongozi waliohudhuria maadhimisho hayo ni Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Mohamed Gharib Bilali, Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Balozi Seif Idd, Waziri wa Ulinzi na Majeshi ya Kujenga Taifa, Dk. Hussein Mwinyi pamoja na Waziri wa Ulinzi wa Msumbiji, Philipe Nyasi.
Wengine ni Waziri Kiongozi Mstaafu wa Zanzibar, Ramadhan Haji, baadhi ya Mawaziri wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar na Serikali ya Jamhuri ya Muungano, Wakuu wa vikosi vya Ulinzi wa Tanzania na Msumbiji, Mabalozi wanaoziwakilisha nchi zao Tanzania, Majenerali wastaafu waliopigana vita vya Msumbiji pamoja na vita vya dunia na viongozi wengineo.
Katika maadhimisho hayo kama ilivyo kawaida baadhi ya viongozi akiwemo Rais Kikwete waliweka silaha za asili ambapo kwa uande wake aliweka Mkuki na Ngao, Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Davis Mwamunyange aliweka sime, Kiongozi wa Mabalozi, Balozi wa DRC, Balozi Juma Khalfan aliweka shada la maua ambapo Meya wa Manispaa ya Mtwara Mikindani Mstahiki Suleiman Mtalika aliweka upinde na mshale.
Baada ya tukio hilo dua na sala kutoka kwa viongozi wa Dini zilizomwa ambapo Sheikh Jamaldin alisoma dua kwa upande wa Waislamu, Mchungaji Lucas Mendule aliwakilisha Kanisa la CCT na Kanisa Katoliki liliwakilishwa na Padri Gabriel Mule.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete pamoja na baadhi ya viongozi wengine wakuu walitembelea makaburi ya mashujaa hao na baadae kuwasalimia wananchi waliohudhuria maadhimisho hayo, ambapo katika salamu zake Rais Kikwete alieleza kuwa kila mwaka Taifa limekuwa na utaratibu wa kuhifadhi kumbukumbu za mashujaa na kutoa pongezi kwa wananchi wengi kujitokeza katika maadhimisho hayo.
Rais Kikwete alisema kuwa kabla ya sherehe hizo kufanywa tarehe hiyo ya jana hapo mwanzo zilikuwa zikifanyika Septemba mosi kutokana na kumbukumbu za kuwapokea Majeshi kwa ushindi walioupata huko nchini Uganda.
Alisema kuwa hivi sasa kila ifikipo tarehe 25 husherehekea maisha ya wakombozi hao kutokana na juhudi kubwa walizozifanya katika kuikomboa nchi ya Msumbiji na sio kusherehekea kufa kwao.
Akieleza historia ya mashujaa hao kwa ufupi, Rais Kikwete alisema kuwa wanajeshi wa Tanzania waliokufa nchini Masumbiji katika jitihada za kuikomboa nchi hiyo kutoka kwa Wakoloni wa Kireno.
Alieleza kuwa Tanzania ilitoa msaada mkubwa katika vita hivyo kutokana na kiongozi wa FRELIMO wakati huo hayati Samora Mashel kumuomba hayati Mwalimu Nyerere kusaidiwa mafunzo na hatimae Majeshi ambapo pia, baada ya ukombozi huo kulitokea watu wachache waliokuwa hawakufurahishwa na ukombozi huo na ndipo walipowatumia waasi wa RENAMO na kuanzisha vita vingine.
Alieleza kuwa katika mapambano ambapo hatimae walisambaratishwa na Majeshi ya Msumbiji kwa mashirikiano na Majeshi ya Tanzania na ndipo baadhi ya wanajeshi wa Tanzania walipoteza maisha katika vita hivyo.
Aidha, alieleza kuwa Mashujaa hao awali walizikwa nchini Msumbiji na baadae ndipo ikaamuliwa kuzikwa katika eneo hilo ambapo pia, alitumia nafasi hiyo kutoa pongezi kwa Jeshi la Tanzania kwa kuwawekea mazingira mazuri mashujaa hao.
Nae Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapainduzi, Dk. Ali Mohamed Shein alitoa pongezi kwa wananchi wa Mtwara kwa kujitokeza kwa wingi katika maadhimisho hayo na kuwapa salamu za wananchi wa Zanzibar.
Nae Waziri wa Ulinzi wa Msumbiji alieleza kuwa uhuru wa Msumbiji ulitokana na damu za Mashujaa hao na kupelekea nchini yao hivi sasa kuendelea kuwa na amani na utulivu mkubwa.
Baada ya hapo viongozi hao wakuu kwa pamoja pamoja na viongozi wengine wakiongozwa na Amiri Jeshi Mkuu, Rais Jakaya Mrisho Kikwete walitembelea nyumba ya Makumbusho ya Naliendele iliyopo katika eneo hilo ambapo mna vifaa mbali mbali vilivyotumiwa na mashujaa hao katika ukumbozi wa Msumbiji. Katika maadhimisho hayo mizinga ilipigwa pamoja na wimbo wa Taifa sambamba na kutolewa salamu za Rais.
WANAHABARI WATAKIWA KUWAUNGANISHA WA ZANZIBARI.
Wanahabari watakiwa kuwaunganisha Wazanzibari
Na Mwandishi Wetu
VYOMBO vya habari vina wajibu wa kuwaunganisha wananchi Zanzibar, umuhimu wa kuwa na serikali ya Umoja wa Kitaifa, hasa baada ya wananchi hao kupita katika kipindi kigumu na cha muda mrefu cha hitilafu za maelewano zilizotokana na hali ya siasa.
Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Richard Mbunda alieleza hayo jana alipokuwa akitoa mada kwenye warsha ya siku mbili inayoelezea nafasi ya vyombo vya habari katika kuimarisha serikali ya Umoja wa kitaifa.
Mhadhiri huyo alisema kihistoria Zanzibar imepitia katika mkondo mrefu wa wa kuhitilafiana kisiasa, hali ambayo imezikwa na maridhiano ya kisiasa yaliyofikiwa baina ya vyama vya CUF na CCM.
Alifahamisha kuwa baada ya kupatikana kwa serikali ya Mapindui ya Zanzibar iliyo katika mfumo wa Umoja wa Kitaifa, ambayo imekuwa msingi imara wa utengamano baina ya Wazanzibari hivi sasa umefika wakati wa kuzienzi na kuzitunza tunu za taifa.
Alizitaja tunu hizo ambazo hazijawekwa katika utaratibu mzuri na baadhi yao zinahitaji kufanyiwa mapitio ni pamoja na amani, umoja,, uzalendo, mshikamano, usawa, haki, muungano, uvumilivu katika dini, rangi na siasa.
Muwezeshaji huyo alisema jamii ipaswa kuelimishwa kwa undani umuhimu wa tunu hizo ambazo zina umuhimu mkubwa katika kujiletea maendeleo, na kueleza kuwa kazi hiyo inaweza kufanywa kwa usahihi na vyombo vya habari.
Kwa upande wake Rashid Omar Kombo ambaye ni Mhadhiri wa Chuo cha Habari Zanzibar, akiwasilisha mada katika warsha hiyo alisema vyombo vya habari vinawajibu wa kuitathmini hali ya utawala bora kwa kutumia viashiria vilivyopo hasa wakati huu ambapo Zanzibar ina serikali ya umoja wa Kitaifa.
Alisema utawala bora una mchango mkubwa katika kukuza maendeleo ya nchi yoyote sambamba na upatikanaji wa haki za msingi ambazo kila mwanadamu anatarajiwa kuzipata bila ya kuwepo mizengwe yeyote.
Wakichangia washiriki wa warsha hiyo walipendekeza uwepo uwajibikaji wa vyombo vya habari katika kutoa taarifa sahihi kwa wasikilizaji, wasomaji na watazamaji wa vyombo vyao na kutaka uweledi utumike ili kuepusha kuandika habari zinazoweza kusababisha mifarakano katika jamii.
Awali akifungua warsha hiyo waziri wa Biashara na Viwanda, Nassor Ahmed Mazrui, kwa niaba ya waziri wa Habari, Utamaduni Utalii na Michezo, Abdilahi Jihad Hassan, alivitaka vyombo vya habari viandike habari zao kwa misingi ya uweledi ili kuepuka kuwa msingi wa mitafaruku katika jamii.
Waziri huyo alisema umefika wakati wananchi kuelimishwa na kuzielewa tunu za taifa ikiwemo Mapinduzi matukufu ya mwaka 1964, ambayo ndiyo yaliyomkomboa kila Mzanzibari.
Waziri Jihad Hassan alivitaka vyombo hivyo viandike habari zao kwa misingi ya uweledi ili kuepuka kuwa msingi wa mitafaruku katika jamii na kueleza kuwa Zanzibar tuitakayo inaweza kujengwa na wazanzibari wenyewe.
Warsha hiyo ya siku mbili inawashirikisha waandishi wa habari, watendaji wa vyama vya siasa pamoja na taasisi za kiraia, na imeandaliwa na Mpango wa Utafiti na Elimu ya Demokrasia Tanzania (REDET).
Na Mwandishi Wetu
VYOMBO vya habari vina wajibu wa kuwaunganisha wananchi Zanzibar, umuhimu wa kuwa na serikali ya Umoja wa Kitaifa, hasa baada ya wananchi hao kupita katika kipindi kigumu na cha muda mrefu cha hitilafu za maelewano zilizotokana na hali ya siasa.
Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Richard Mbunda alieleza hayo jana alipokuwa akitoa mada kwenye warsha ya siku mbili inayoelezea nafasi ya vyombo vya habari katika kuimarisha serikali ya Umoja wa kitaifa.
Mhadhiri huyo alisema kihistoria Zanzibar imepitia katika mkondo mrefu wa wa kuhitilafiana kisiasa, hali ambayo imezikwa na maridhiano ya kisiasa yaliyofikiwa baina ya vyama vya CUF na CCM.
Alifahamisha kuwa baada ya kupatikana kwa serikali ya Mapindui ya Zanzibar iliyo katika mfumo wa Umoja wa Kitaifa, ambayo imekuwa msingi imara wa utengamano baina ya Wazanzibari hivi sasa umefika wakati wa kuzienzi na kuzitunza tunu za taifa.
Alizitaja tunu hizo ambazo hazijawekwa katika utaratibu mzuri na baadhi yao zinahitaji kufanyiwa mapitio ni pamoja na amani, umoja,, uzalendo, mshikamano, usawa, haki, muungano, uvumilivu katika dini, rangi na siasa.
Muwezeshaji huyo alisema jamii ipaswa kuelimishwa kwa undani umuhimu wa tunu hizo ambazo zina umuhimu mkubwa katika kujiletea maendeleo, na kueleza kuwa kazi hiyo inaweza kufanywa kwa usahihi na vyombo vya habari.
Kwa upande wake Rashid Omar Kombo ambaye ni Mhadhiri wa Chuo cha Habari Zanzibar, akiwasilisha mada katika warsha hiyo alisema vyombo vya habari vinawajibu wa kuitathmini hali ya utawala bora kwa kutumia viashiria vilivyopo hasa wakati huu ambapo Zanzibar ina serikali ya umoja wa Kitaifa.
Alisema utawala bora una mchango mkubwa katika kukuza maendeleo ya nchi yoyote sambamba na upatikanaji wa haki za msingi ambazo kila mwanadamu anatarajiwa kuzipata bila ya kuwepo mizengwe yeyote.
Wakichangia washiriki wa warsha hiyo walipendekeza uwepo uwajibikaji wa vyombo vya habari katika kutoa taarifa sahihi kwa wasikilizaji, wasomaji na watazamaji wa vyombo vyao na kutaka uweledi utumike ili kuepusha kuandika habari zinazoweza kusababisha mifarakano katika jamii.
Awali akifungua warsha hiyo waziri wa Biashara na Viwanda, Nassor Ahmed Mazrui, kwa niaba ya waziri wa Habari, Utamaduni Utalii na Michezo, Abdilahi Jihad Hassan, alivitaka vyombo vya habari viandike habari zao kwa misingi ya uweledi ili kuepuka kuwa msingi wa mitafaruku katika jamii.
Waziri huyo alisema umefika wakati wananchi kuelimishwa na kuzielewa tunu za taifa ikiwemo Mapinduzi matukufu ya mwaka 1964, ambayo ndiyo yaliyomkomboa kila Mzanzibari.
Waziri Jihad Hassan alivitaka vyombo hivyo viandike habari zao kwa misingi ya uweledi ili kuepuka kuwa msingi wa mitafaruku katika jamii na kueleza kuwa Zanzibar tuitakayo inaweza kujengwa na wazanzibari wenyewe.
Warsha hiyo ya siku mbili inawashirikisha waandishi wa habari, watendaji wa vyama vya siasa pamoja na taasisi za kiraia, na imeandaliwa na Mpango wa Utafiti na Elimu ya Demokrasia Tanzania (REDET).
ATEKWA NYARA KWA KUTAKA KUUZA MCHELE BEI NAFUU.
Atekwa nyara kwa kutaka kuuza mchele bei nafuu
• SMZ yawakoromea wafanyabiashara wanyanyasaji
• Yahamasisha wote wenye uwezo kuagiza bidhaa
Na Abdi Shamnah, OMKR
MAKAMU wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Maalim Seif Sharif Hamad amewataka wafanyabiashara wenye uwezo wa kuleta bidhaa mbali mbali nchini, kufanya hivyo na kusema Serikali itatoa kila aina ya ushirikiano.
Maalim Seif, ambae pia ni Katibu Mkuu wa CUF, amesema hayo jana kwa nyakati tofauti alipozungumza na wananchi wa majimbo ya Matemwe na Chaani, kufuatia ziara zake za kuyatembelea Majimbo yote Unguja na Pemba kuonana na wajumbe wa CUF pamoja na kuzungumza na wananchi.
Amesema wakati huu wananchi wakilalamika kupanda kwa gharama za maisha kutokana na ongezeko la bei za bidhaa, kuna baadhi ya wafanyabiashara wanaopinga hatua ya wafanyabiashara wengine kuleta bidhaa ikiwemo mchele kwa hofu ya bidhaa hizo kuteremka bei.
Alisema katika tukio la hivi karibuni kuna mfanyabiashara (hakumtaja jina) aliedhamiria kuleta mchele na kuuza kwa bei ya chini, lakini wamejitokeza baadhi ya wafanyabiashara wanaomtishia maisha kupitia meseji za simu, ili aondokane na dhamira hizo.
Bila kufafanua kwa undani, Maalim Seif alisema taarifa zilizopo ni kuwa mfanyabaishara huyo ametekwa nyara.
Alisema wafanyabiashara hao wanafanya hivyo kwa kuamini kuwa pale mfanyabiashara huyo atakapoleta bidhaa hizo na kuuza kwa bei nafuu, watalazimika kupunguza bei za bidhaa zao au zitawaozea madukani.
Alisema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar itashirikiana na wafanyabiashara wote wenye dhamira ya kuwaondolea wananchi dhiki ya maisha inayotokana na kupanda kwa gharama za bidhaa pamoja na kuwachukulia hatua kali za kisheria wale wote watakaobainika kuhusika na vitendo visivyokubalika na jamii.
Maalim Seif aliwaeleza wananchi hao kuwa Serikali imedhamiria kunyanyua kipato chao kupitia mazao ya biashara, ikiwemo mwani ambao hivi sasa umekuwa ukiuzwa kwa bei ya chini mno.
Alisema Serikali imeipa Wizara ya Biashara,Viwanda na Masoko jukumu la kuhakikisha bei ya zao hilo inapanda kama ilivyo kwa karafuu, na kubainisha changamoto iliyopo, kufuatia zao kutokuwa mikononi mwa Serikali.
Alisema hali ya bei ya zao hilo hivi sasa hairidhishi, kwani wakulima hulipwa wastani wa shilingi 400/- tu kwa kilo, wakati bei katika soko la dunia ni zaidi ya shilingi 2,500/-.
Aliwatupia lawama wafanyabiashara (matajiri) wanaojishughulisha na ununuzi wa zao hilo kutoka kwa wakulima, kwa kuwakandamiza kwa makusudi wakulima na kutoa visingizio vya uongo vya kupanda kwa gharama za uendeshaji.
Alisema tayari kuna taarifa zinazoonesha nia ya kuja kwa makampuni yenye lengo la kupandisha bei ya zao hilo na hivyo kutoa ushindani katika soko la ndani ya zao hilo.
Aliweka wazi kuwa lengo la Serikali ni kuhakikisha bei ya zao hilo inapanda kutoka shilingi 400/- hadi kufikia shilingi 1,000/- kwa kilo, hatua aliyosema itamuwezesha mkulima kunufaika kutokana na jasho lake.
Katika hatua nyengine Maalim Seif aliwahakikishia wananchi wa Majimbo hayo kuwa Serikali imekusudia kulivalia njuga na kulizamaliza kabisa tatizo la ukosefu wa maji safi na salama, ndani ya kipindi cha miaka mitatu, kupitia bajeti yake ya kila mwaka.
Vile vile Maalim Seif alitumia fursa ya kukutana na wananchi hao kuwaeleza azma za Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuwasilisha Bungeni mswada wa kuundwa kwa katiba mpya, hivyo aliwataka kujitokeza kwa wingi kutoa maoni yao bila woga, pale Tume itakapopita kukusanya maoni.
Aliwataka wananchi hao kutoa mawazo yao juu ya aina gani ya Muungano wanaoutaka na mambo mbali mbali yaliyomo ndani ya Muungano huo, ili hatimae Tanzania iweze kuwa na Katiba nzuri yenye maslahi kwa pande zote mbili za Muungano huo.
• SMZ yawakoromea wafanyabiashara wanyanyasaji
• Yahamasisha wote wenye uwezo kuagiza bidhaa
Na Abdi Shamnah, OMKR
MAKAMU wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Maalim Seif Sharif Hamad amewataka wafanyabiashara wenye uwezo wa kuleta bidhaa mbali mbali nchini, kufanya hivyo na kusema Serikali itatoa kila aina ya ushirikiano.
Maalim Seif, ambae pia ni Katibu Mkuu wa CUF, amesema hayo jana kwa nyakati tofauti alipozungumza na wananchi wa majimbo ya Matemwe na Chaani, kufuatia ziara zake za kuyatembelea Majimbo yote Unguja na Pemba kuonana na wajumbe wa CUF pamoja na kuzungumza na wananchi.
Amesema wakati huu wananchi wakilalamika kupanda kwa gharama za maisha kutokana na ongezeko la bei za bidhaa, kuna baadhi ya wafanyabiashara wanaopinga hatua ya wafanyabiashara wengine kuleta bidhaa ikiwemo mchele kwa hofu ya bidhaa hizo kuteremka bei.
Alisema katika tukio la hivi karibuni kuna mfanyabiashara (hakumtaja jina) aliedhamiria kuleta mchele na kuuza kwa bei ya chini, lakini wamejitokeza baadhi ya wafanyabiashara wanaomtishia maisha kupitia meseji za simu, ili aondokane na dhamira hizo.
Bila kufafanua kwa undani, Maalim Seif alisema taarifa zilizopo ni kuwa mfanyabaishara huyo ametekwa nyara.
Alisema wafanyabiashara hao wanafanya hivyo kwa kuamini kuwa pale mfanyabiashara huyo atakapoleta bidhaa hizo na kuuza kwa bei nafuu, watalazimika kupunguza bei za bidhaa zao au zitawaozea madukani.
Alisema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar itashirikiana na wafanyabiashara wote wenye dhamira ya kuwaondolea wananchi dhiki ya maisha inayotokana na kupanda kwa gharama za bidhaa pamoja na kuwachukulia hatua kali za kisheria wale wote watakaobainika kuhusika na vitendo visivyokubalika na jamii.
Maalim Seif aliwaeleza wananchi hao kuwa Serikali imedhamiria kunyanyua kipato chao kupitia mazao ya biashara, ikiwemo mwani ambao hivi sasa umekuwa ukiuzwa kwa bei ya chini mno.
Alisema Serikali imeipa Wizara ya Biashara,Viwanda na Masoko jukumu la kuhakikisha bei ya zao hilo inapanda kama ilivyo kwa karafuu, na kubainisha changamoto iliyopo, kufuatia zao kutokuwa mikononi mwa Serikali.
Alisema hali ya bei ya zao hilo hivi sasa hairidhishi, kwani wakulima hulipwa wastani wa shilingi 400/- tu kwa kilo, wakati bei katika soko la dunia ni zaidi ya shilingi 2,500/-.
Aliwatupia lawama wafanyabiashara (matajiri) wanaojishughulisha na ununuzi wa zao hilo kutoka kwa wakulima, kwa kuwakandamiza kwa makusudi wakulima na kutoa visingizio vya uongo vya kupanda kwa gharama za uendeshaji.
Alisema tayari kuna taarifa zinazoonesha nia ya kuja kwa makampuni yenye lengo la kupandisha bei ya zao hilo na hivyo kutoa ushindani katika soko la ndani ya zao hilo.
Aliweka wazi kuwa lengo la Serikali ni kuhakikisha bei ya zao hilo inapanda kutoka shilingi 400/- hadi kufikia shilingi 1,000/- kwa kilo, hatua aliyosema itamuwezesha mkulima kunufaika kutokana na jasho lake.
Katika hatua nyengine Maalim Seif aliwahakikishia wananchi wa Majimbo hayo kuwa Serikali imekusudia kulivalia njuga na kulizamaliza kabisa tatizo la ukosefu wa maji safi na salama, ndani ya kipindi cha miaka mitatu, kupitia bajeti yake ya kila mwaka.
Vile vile Maalim Seif alitumia fursa ya kukutana na wananchi hao kuwaeleza azma za Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuwasilisha Bungeni mswada wa kuundwa kwa katiba mpya, hivyo aliwataka kujitokeza kwa wingi kutoa maoni yao bila woga, pale Tume itakapopita kukusanya maoni.
Aliwataka wananchi hao kutoa mawazo yao juu ya aina gani ya Muungano wanaoutaka na mambo mbali mbali yaliyomo ndani ya Muungano huo, ili hatimae Tanzania iweze kuwa na Katiba nzuri yenye maslahi kwa pande zote mbili za Muungano huo.
NEC - CCM ZANZIBAR YATANGAZA SAFU MPYA.
NEC-CCM Zanzibar yatangaza safu mpya
Na Mwanajuma Abdi
KAMATI Maluum ya Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM Zanzibar, imewateuwa wajumbe wapya wa sekretarieti ya Kamati hiyo pamoja na kupitia majina 21 ya UVCCM wanaowania nafasi ya Mwenyekiti wa Taifa.
Akizungumza na waandishi wa habari, oOisi Kuu ya CCM Kisiwandui, Katibu wa Kamati Maalum ya NEC Zanzibar, Itikadi na Uenezi Zanzibar, Issa Haji Ussi, amesema wajumbe hao wameteuliwa baada ya kufanyika kikao cha Kamati hiyo kilichofanyika Jumapili Ofisi hiyo mjini hapa, chini ya Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Zanzibar, Dk. Amani Abeid Karume.
Alisema walioteuliwa kushika nyadhifa za wajumbe wa Sekretarieti ya Kamati Maalum ya Halmashauri Kuu ya Taifa Zanzibar ambao wataongoza katika Idara mbali mbali ni Machano Othman Said ameteuliwa kuwa katibu Kamati Maalum ya NEC- Organaizesheni, ambapo awali alikuwa ni Katibu wa Kamati Maalum ya NEC Siasa na Uhusiano wa Kimataifa (SUKI) nafasi ambayo kwa sasa itashikiliwa na Haroun Ali Suleiman.
Alieleza wajumbe wengine walioteuliwa ni Issa Haji Ussi atakuwa ni Katibu wa Kamati Maalum ya NEC- Itikadi na Uenezi, ambapo nafasi hiyo awali ilikuwa ikishikiliwa na Vuai Ali Vuai ambae ni Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar na Mansoor Yussuf Himid ataendelea kuwa Katibu wa Kamati Maalum ya NEC, Uchumi na Fedha kwa chama hicho.
Aidha aliongeza, kikao hicho kilijadili majina 21 ya wanachama wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) waliojitokeza kuomba kugombea nafasi ya Mwenyekiti wa Taifa wa Umoja huo, ambapo mapendekezo ya kamati hiyo yametolewa.
"Jumla ya wanachama 21 wa UVCCM wamejitokeza kuomba kugombea nafasi hiyo kufuatia kujiuzulu kwa aliyekuwa akishikilia nafasi hiyo Hamad Masauni Yussuf mnamo Mei 18, mwaka jana", alisema Issa.
Alifafanua kuwa, kati ya majina hayo 19 ni vijana kutoka Zanzibar na wawili kutoka Tanzania Bara, ambapo alisisitiza kwa mujibu wa utaratibu na kanuni za UVCCM kwamba Makamu Mwenyekiti akitokea Tanzania, lazima Mwenyekiti awe Mzanzibari hivyo majina hayo mawili yatakuwa hayawezi kufuzu katika mchujo hapo baadae.
Alisema tayari kanuni zishawekwa haziwezi kuvunjwa, ambapo wagombea hao wawili wa Tanzania Bara wametumia haki yao ya kidemokrasia lakini wamekiuka kanuni.
Hata hivyo, Issa alikanusha kuchukuwa fomu ya kuwania nafasi ya Mwenyekiti wa UVCCM, ambapo alisisitiza kwa waandishi waamini kauli yake na sio kusikia maneno pembeni.
Alieleza kwamba, CCM ni chama kikubwa chenye wanachama wengi, kimbilio la wanyonge, kinaheshimika na kinafuata misingi ya kidemokrasia, ambapo alihahakisha ushindi mkubwa wa kishindo utapatikana katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2015.
Alisema Kamati Maalum ilimpongeza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Ali Mohamed Shein kwa kazi nzuri ya kusimamia utekelezaji wa ilani ya CCM ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2010-2015, pamoja na ahadi zake alizozitoa wakati wa kampeni za uchaguzi kuanza kuzitekeleza kwa vitendo.
Aliendelea kusema, hatua zinazochukuliwa na Dk. Shein zina lengo la kuinua hali za wananchi wa Unguja na Pemba za kuwapunguzia mzigo wa maisha ili kufanikisha lengo la kupunguza umasikini, ambapo miongoni mwa hatua hizo ni kuongeza mishahara ya watumishi wa Serikali kwa asilimia 25, kupandisha bei ya karafuu kutoka shilingi 5,000 hadi shilingi 10,000 kwa kilo moja ya daraja la kwanza na shilingi 9,500 kwa daraja la pili.
Issa alifahamisha kuwa, Serikali imeelekeza nguvu katika kuimarisha sekta ya kilimo kwa kutumia kauli mbiu ya 'Mapinduzi ya kilimo' kwa kupunguza bei ya pembejeo za kilimo na gharama za matrekta, ambapo kwa polo moja la mbolea ya TSP itauzwa kwa shilingi 16,000 badala ya shilingi 32,000 na mbolea ya UREA ni shilingi 10,000 badala ya 20,000, punguzo hili ni la asilimia 50 pamoja na mbegu ya mpunga itauzwa kwa shilingi 10,000 kwa kilo badala ya shilingi 25,000.
Hata hivyo, alieleza Serikali imepunguza kwa asilimia 75 bei ya kuchimbua na kuburuga mashamba kwa kutumia trekta kutoka shilingi 32,000 kwa eka hapo mwanzo na sasa ni shilingi 16,000 kwa eka, sambamba na kupunguzwa kwa bei ya dawa ya kuua magugu kutoka shilingi 12,500 kwa lita hadi shilingi 6,000 ikiwa ni punguzo la asilimia 52.
Alisema kamati Maalum ya Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) Zanzibar imeridhiswa na hatua zilizofikiwa na Serikali, ikiwemo utekelezaji wa vitendo wa ilani ya CCM ya Uchaguzi Mkuu wa 2010, Dira ya maendeleo ya 2020 na mkakati wa kukuza uchumi na kupunguza umasikini Zanzibar wa mwaka 2010-2015 (MKUZA II).
Na Mwanajuma Abdi
KAMATI Maluum ya Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM Zanzibar, imewateuwa wajumbe wapya wa sekretarieti ya Kamati hiyo pamoja na kupitia majina 21 ya UVCCM wanaowania nafasi ya Mwenyekiti wa Taifa.
Akizungumza na waandishi wa habari, oOisi Kuu ya CCM Kisiwandui, Katibu wa Kamati Maalum ya NEC Zanzibar, Itikadi na Uenezi Zanzibar, Issa Haji Ussi, amesema wajumbe hao wameteuliwa baada ya kufanyika kikao cha Kamati hiyo kilichofanyika Jumapili Ofisi hiyo mjini hapa, chini ya Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Zanzibar, Dk. Amani Abeid Karume.
Alisema walioteuliwa kushika nyadhifa za wajumbe wa Sekretarieti ya Kamati Maalum ya Halmashauri Kuu ya Taifa Zanzibar ambao wataongoza katika Idara mbali mbali ni Machano Othman Said ameteuliwa kuwa katibu Kamati Maalum ya NEC- Organaizesheni, ambapo awali alikuwa ni Katibu wa Kamati Maalum ya NEC Siasa na Uhusiano wa Kimataifa (SUKI) nafasi ambayo kwa sasa itashikiliwa na Haroun Ali Suleiman.
Alieleza wajumbe wengine walioteuliwa ni Issa Haji Ussi atakuwa ni Katibu wa Kamati Maalum ya NEC- Itikadi na Uenezi, ambapo nafasi hiyo awali ilikuwa ikishikiliwa na Vuai Ali Vuai ambae ni Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar na Mansoor Yussuf Himid ataendelea kuwa Katibu wa Kamati Maalum ya NEC, Uchumi na Fedha kwa chama hicho.
Aidha aliongeza, kikao hicho kilijadili majina 21 ya wanachama wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) waliojitokeza kuomba kugombea nafasi ya Mwenyekiti wa Taifa wa Umoja huo, ambapo mapendekezo ya kamati hiyo yametolewa.
"Jumla ya wanachama 21 wa UVCCM wamejitokeza kuomba kugombea nafasi hiyo kufuatia kujiuzulu kwa aliyekuwa akishikilia nafasi hiyo Hamad Masauni Yussuf mnamo Mei 18, mwaka jana", alisema Issa.
Alifafanua kuwa, kati ya majina hayo 19 ni vijana kutoka Zanzibar na wawili kutoka Tanzania Bara, ambapo alisisitiza kwa mujibu wa utaratibu na kanuni za UVCCM kwamba Makamu Mwenyekiti akitokea Tanzania, lazima Mwenyekiti awe Mzanzibari hivyo majina hayo mawili yatakuwa hayawezi kufuzu katika mchujo hapo baadae.
Alisema tayari kanuni zishawekwa haziwezi kuvunjwa, ambapo wagombea hao wawili wa Tanzania Bara wametumia haki yao ya kidemokrasia lakini wamekiuka kanuni.
Hata hivyo, Issa alikanusha kuchukuwa fomu ya kuwania nafasi ya Mwenyekiti wa UVCCM, ambapo alisisitiza kwa waandishi waamini kauli yake na sio kusikia maneno pembeni.
Alieleza kwamba, CCM ni chama kikubwa chenye wanachama wengi, kimbilio la wanyonge, kinaheshimika na kinafuata misingi ya kidemokrasia, ambapo alihahakisha ushindi mkubwa wa kishindo utapatikana katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2015.
Alisema Kamati Maalum ilimpongeza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Ali Mohamed Shein kwa kazi nzuri ya kusimamia utekelezaji wa ilani ya CCM ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2010-2015, pamoja na ahadi zake alizozitoa wakati wa kampeni za uchaguzi kuanza kuzitekeleza kwa vitendo.
Aliendelea kusema, hatua zinazochukuliwa na Dk. Shein zina lengo la kuinua hali za wananchi wa Unguja na Pemba za kuwapunguzia mzigo wa maisha ili kufanikisha lengo la kupunguza umasikini, ambapo miongoni mwa hatua hizo ni kuongeza mishahara ya watumishi wa Serikali kwa asilimia 25, kupandisha bei ya karafuu kutoka shilingi 5,000 hadi shilingi 10,000 kwa kilo moja ya daraja la kwanza na shilingi 9,500 kwa daraja la pili.
Issa alifahamisha kuwa, Serikali imeelekeza nguvu katika kuimarisha sekta ya kilimo kwa kutumia kauli mbiu ya 'Mapinduzi ya kilimo' kwa kupunguza bei ya pembejeo za kilimo na gharama za matrekta, ambapo kwa polo moja la mbolea ya TSP itauzwa kwa shilingi 16,000 badala ya shilingi 32,000 na mbolea ya UREA ni shilingi 10,000 badala ya 20,000, punguzo hili ni la asilimia 50 pamoja na mbegu ya mpunga itauzwa kwa shilingi 10,000 kwa kilo badala ya shilingi 25,000.
Hata hivyo, alieleza Serikali imepunguza kwa asilimia 75 bei ya kuchimbua na kuburuga mashamba kwa kutumia trekta kutoka shilingi 32,000 kwa eka hapo mwanzo na sasa ni shilingi 16,000 kwa eka, sambamba na kupunguzwa kwa bei ya dawa ya kuua magugu kutoka shilingi 12,500 kwa lita hadi shilingi 6,000 ikiwa ni punguzo la asilimia 52.
Alisema kamati Maalum ya Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) Zanzibar imeridhiswa na hatua zilizofikiwa na Serikali, ikiwemo utekelezaji wa vitendo wa ilani ya CCM ya Uchaguzi Mkuu wa 2010, Dira ya maendeleo ya 2020 na mkakati wa kukuza uchumi na kupunguza umasikini Zanzibar wa mwaka 2010-2015 (MKUZA II).
WANAOTELEKEZA WATOTO WADHIIBITIWE.
Wanaotelekeza watoto wadhibitiwe
Na Halima Abdalla
BAADHI ya wajumbe wa Baraza la Wawakilishi wamesikitishwa na kukithiri kwa vitendo vya ubakaji na udhalilishaji wa watoto na wanawake kutelekezwa vinavyofanywa na baadhi ya akinababa.
Waliishauri Serikali kuweka sheria kali na nzito kwa yeyote atakaepatikana na hatia hiyo kupewa adhabu nzito na itangazwe katika vyombo vya habari ili kuweza kutoa somo kwa wabakaji wengine.
Akichangia bajeti ya Wizara ya Ustawi wa Jamii, Maendeleo ya Vijana, wanawake na Watoto, Asha Bakari Makame, aliishauri Serikali kuweka sheria kali kwa wanaume wanaofanya kazi Serikalini ambao wanatelekeza wanawake na watoto kuwakata kima cha mshahara wao kila mwezi ili aweze kupewa mwanamke kiweze kumsaidia yeye na mtoto wake.
Alisema wanawake sasa hivi wamekazana kwa kujishughulisha shughuli mbali mbali za kujipatia kipato, lakini wamekuwa wakirudi nyuma kutokana na kutelekezwa na akinababa kwa kuwaachia familia bila ya kuwashughulikia.
Sambamba na hayo aliwashauri kinababa kuwaonea huruma kinamama kutokana na kazi ngumu wanazozifanya pamoja na kuangalia familia na kazi nzito zinazowakabili.
Nae Mtumwa Kheir Mbarouk (Nafasi za wanawake ) aliwataka kinababa kuwa na imani kuacha kuwaharibu watoto wadogo walemavu na mataahira kwani vitendo hivyo ni ukiukwaji wa haki za binadamu.
Sambamba na hayo aliwashauri wazazi ambao watoto wao wamefanyiwa vitendo hivyo kutokubali kuyamaliza mitaani, ila wayafikishe katika vyombo husika pamoja na mahakama zisichelewe kesi hizo pamoja na kutoa hukumu.
Aisha alimshauri Wizara ya Ustawi wa jamii kuelimisha wananchi kuwa wanapofanyiwa vitendo hivyo vya ubakaji wasifiche kwani wanaofanyiwa vitendo hivyo ni masikini na wenye uelewa mdogo.
Kwa upande wake Mwakilishi wa Micheweni, Subeit Khamis Faki aliishauri Wizara hiyo kubuni miradi mbali mbali ya kuweza kusaidia kuajiri vijana ili kuondokana na watoto wa mitaani kwani ajira za utotoni hazifanywi kwa maksudi ila hali hiyo inatokana na hali za wazee wao kuwa ngumu na yeye ili apate kuishi.
''Hawa watoto hawafanyi kwa hiari yao wanafanya kwa lazima ili waweze kupata chakula cha kuwasaidia ili waweze kuendelea kuishi,''alisema Subeit.
Aidha alishauri Serikali kuwasaidia vijana waliopo katika wilaya ya Micheweni kwa sababu inaongoza kwa ajira za utotoni pamoja na umasikini kwa kuweza kuwatembelea na kuwapatia elimu sambamba na kuwasaidia ili kuondokana na umasikini.
Nae panya Ali Abdalla (Nafasi ya wanawake) alizishauri mahkama kuacha kuwasumbua wanawake wanapofuatilia kesi za ubakaji mahkamani kutokana na nenda rudi za kila siku ambazo zinasababisha wanawake kukata tamaa na kupelekea kesi hizo kushindwa kuendelea.
Kwa upande wake Viwe Khamis Abdalla (Nafasi ya wanawake) aliishauri akinamama wanaojifungua kuacha kutelekeza watoto kwa kuwatupa aliishauri Serikali kuchukuliwa hatua kali wanawake hao kwani wanachofanya ni ukiukwaji wa haki za binadamu.
Na Halima Abdalla
BAADHI ya wajumbe wa Baraza la Wawakilishi wamesikitishwa na kukithiri kwa vitendo vya ubakaji na udhalilishaji wa watoto na wanawake kutelekezwa vinavyofanywa na baadhi ya akinababa.
Waliishauri Serikali kuweka sheria kali na nzito kwa yeyote atakaepatikana na hatia hiyo kupewa adhabu nzito na itangazwe katika vyombo vya habari ili kuweza kutoa somo kwa wabakaji wengine.
Akichangia bajeti ya Wizara ya Ustawi wa Jamii, Maendeleo ya Vijana, wanawake na Watoto, Asha Bakari Makame, aliishauri Serikali kuweka sheria kali kwa wanaume wanaofanya kazi Serikalini ambao wanatelekeza wanawake na watoto kuwakata kima cha mshahara wao kila mwezi ili aweze kupewa mwanamke kiweze kumsaidia yeye na mtoto wake.
Alisema wanawake sasa hivi wamekazana kwa kujishughulisha shughuli mbali mbali za kujipatia kipato, lakini wamekuwa wakirudi nyuma kutokana na kutelekezwa na akinababa kwa kuwaachia familia bila ya kuwashughulikia.
Sambamba na hayo aliwashauri kinababa kuwaonea huruma kinamama kutokana na kazi ngumu wanazozifanya pamoja na kuangalia familia na kazi nzito zinazowakabili.
Nae Mtumwa Kheir Mbarouk (Nafasi za wanawake ) aliwataka kinababa kuwa na imani kuacha kuwaharibu watoto wadogo walemavu na mataahira kwani vitendo hivyo ni ukiukwaji wa haki za binadamu.
Sambamba na hayo aliwashauri wazazi ambao watoto wao wamefanyiwa vitendo hivyo kutokubali kuyamaliza mitaani, ila wayafikishe katika vyombo husika pamoja na mahakama zisichelewe kesi hizo pamoja na kutoa hukumu.
Aisha alimshauri Wizara ya Ustawi wa jamii kuelimisha wananchi kuwa wanapofanyiwa vitendo hivyo vya ubakaji wasifiche kwani wanaofanyiwa vitendo hivyo ni masikini na wenye uelewa mdogo.
Kwa upande wake Mwakilishi wa Micheweni, Subeit Khamis Faki aliishauri Wizara hiyo kubuni miradi mbali mbali ya kuweza kusaidia kuajiri vijana ili kuondokana na watoto wa mitaani kwani ajira za utotoni hazifanywi kwa maksudi ila hali hiyo inatokana na hali za wazee wao kuwa ngumu na yeye ili apate kuishi.
''Hawa watoto hawafanyi kwa hiari yao wanafanya kwa lazima ili waweze kupata chakula cha kuwasaidia ili waweze kuendelea kuishi,''alisema Subeit.
Aidha alishauri Serikali kuwasaidia vijana waliopo katika wilaya ya Micheweni kwa sababu inaongoza kwa ajira za utotoni pamoja na umasikini kwa kuweza kuwatembelea na kuwapatia elimu sambamba na kuwasaidia ili kuondokana na umasikini.
Nae panya Ali Abdalla (Nafasi ya wanawake) alizishauri mahkama kuacha kuwasumbua wanawake wanapofuatilia kesi za ubakaji mahkamani kutokana na nenda rudi za kila siku ambazo zinasababisha wanawake kukata tamaa na kupelekea kesi hizo kushindwa kuendelea.
Kwa upande wake Viwe Khamis Abdalla (Nafasi ya wanawake) aliishauri akinamama wanaojifungua kuacha kutelekeza watoto kwa kuwatupa aliishauri Serikali kuchukuliwa hatua kali wanawake hao kwani wanachofanya ni ukiukwaji wa haki za binadamu.
Saturday, 23 July 2011
WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Rais Fedha Uchumina Mipango ya Maendeleo Omar Yussuf Mzee akitiliana saini na Balozi Mdogo wa China aliyepo Zanzibar Chen Qinman, msaada wa kuwawezesha Watendaji wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kupata mafunzo nchini China, utiaji saini huo umefanyika ukumbi wa Wizara ya Fedha Vuga Mjini Zanzibar (Picha na Othman Maulid)
Subscribe to:
Posts (Atom)
