MKE wa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mama Mwanamwema Shein akiwahutubia Wananchi wa Kijiji cha Makunduchi wakati wa ziara yake ya kutembelea Vikundi vya Ushirika vya Wanawake wa Mkoa wa Kusini Unguja, akiwa katika Viwanja vya Skuli ya Kiongoni Makunduchi.(Picha na OthmanMaulid)
Sunday, 24 April 2011
ASKOFU ATAKA 'MAFISADI' WACHUKULIWE HATUA.
Askofu ataka ‘mafisadi’ wachukuliwe hatua
Asema Serikali zifikie matumaini ya wananchi
• Haoni sababu kuwepo maskini Tanzania
Na Mwanajuma Abdi
ASKOFU Augustine Ndeliakyama Shao wa kanisa la Roman Catholic Zanzibar, amesema watanzania wanalia na kuvunjika moyo na ubadhirifu na mishahara hewa kwa baadhi ya viongozi nchini hali inayosababisha kukosekana kwa nyenzo maskulini, vyuo na uhaba wa dawa hospitalini.
Hayo aliyasema jana, katika hotuba aliyoitoa katika kanisa la Minara miwili Shangani mjini Unguja kwa waumini wa dini ya kikristo ikiwa ni ujumbe wa Pasaka 2011 ‘mwanga unaoleta uhuru kwa mwanadamu aliyekuwa kwenye giza la maovu’.
Alisema watanzania wamekata tamaa na nchi yao kutokana kusikia ubadhirifu mkubwa na upoteaji wa fedha za mishahara hewa inayofanywa na baadhi ya viongozi waliopo katika madaraka nchini huku huduma muhimu zikikosekana katika hospitali na maskulini.
Wakati watanzania wakitarajia mengi mazuri kutoka kwa Serikali zao lakini wanapata ripoti za ubadhirifu wa baadhi ya viongozi katika Wizara, Mikoa, wilaya na taasisi mbali mbali wakifaidika kwa mishahara hewa na wengine kushindwa kutoa ankara za matumizi, wakati huku mahospitali yakiwa na uhaba wa dawa muhimu, shule na vyuo vikiwa havina nyenzo muhimu za kufundishia”, alisema Askofu Shao.
Alisema hayo hayawezi kufanyika kama hakuna utawala wa sheria, watanzania wanaotegemea huduma nzuri kwa gharama ya kodi zao hawajasikia hatua zinazochukuliwa au zilizochukuliwa dhidi ya ubadhirifu huo.
Alieleza ufufuko wa kristu ni agizo la kutafuta sababu za wengi kuwa masikini na wachache kuwa matajiri wa kupindukia katika nchi tajiri kama Tanzania, ambapo aligusia popote pale penye mateso njaa na umasikini unatokana na uvunjwaji wa haki za binadamu.
Askofu Shao alitoa wito kwa viongozi wa jamii kuangalia upya sheria za ardhi, madini na biashara katika kukuza uchumi kwa watu wote bila ya kuweka tabaka.
Aliwaeleza waumini hao kwamba, Serikali inakimbizana na wamachinga na wakulima wadogo wadogo wanaobeba mazao na bidhaa zao kichwani na migongoni kwa ajili ya kutafuta riski kwa kuwabebesha kodi kubwa huku ikiendeleza misamaha kwa wawekezaji na wafanyabiashara wakubwa, ambao wangalisaidia kunyanyua uchumi badala ya kutwishwa mzigo wadogo.
“Kodi ya mfanyabiashara anayeingiza kontena 50, muwekezaji katika hoteli au madini hawa wote wakilipa kodi uhakika kwa kipindi kifupi nchi yetu itafikia malengo ya maendeleo”, alisisitiza.
Aidha alisema, kwa miezi sita hivi kumekuwepo kwa Serikali mpya, Serikali ya Mapinduzi Zanzibar yenye muundo wa Umoja wa Kitaifa na ile ya Serikali ya Muungano Tanzania, ambapo watanzania walikuwa na matarajio makubwa ya mabadiliko hayo yataleta matumaini.
Aliongeza kusema kwamba, ni mapema mno kutoa tathmini lakini kwa kusoma alama na matukio machache, wengi wao hawajaona nia ya dhati ya kutaka mabadiliko na utayari wa baadhi ya viongozi kupokea mawazo na changamoto za wengine kwa kuona nguvu mpya, ubunifu mpya wa rika mbali mbali, vipaji tofauti na itikadi mbali mbali katika Wizara, Wilaya, Mikoa na Taasisi za Serikali.
Hata hivyo, alitoa wito kwa waumini kwamba agizo la ufufuko ni kuwaonesha watu kwa uhakika wote kwamba kristu ni Mkombozi wa dunia ameshinda maovu yote, amejenga matumaini na kwamba wote wana haki ya uhai wenye furaha.
Jana wakristo duniani kote walisherehekea maadhimisho ya kufufuka kwa kiongozi wao Yesu Kristo, baada ya kufariki siku ya Ijumaa Kuu.
Asema Serikali zifikie matumaini ya wananchi
• Haoni sababu kuwepo maskini Tanzania
Na Mwanajuma Abdi
ASKOFU Augustine Ndeliakyama Shao wa kanisa la Roman Catholic Zanzibar, amesema watanzania wanalia na kuvunjika moyo na ubadhirifu na mishahara hewa kwa baadhi ya viongozi nchini hali inayosababisha kukosekana kwa nyenzo maskulini, vyuo na uhaba wa dawa hospitalini.
Hayo aliyasema jana, katika hotuba aliyoitoa katika kanisa la Minara miwili Shangani mjini Unguja kwa waumini wa dini ya kikristo ikiwa ni ujumbe wa Pasaka 2011 ‘mwanga unaoleta uhuru kwa mwanadamu aliyekuwa kwenye giza la maovu’.
Alisema watanzania wamekata tamaa na nchi yao kutokana kusikia ubadhirifu mkubwa na upoteaji wa fedha za mishahara hewa inayofanywa na baadhi ya viongozi waliopo katika madaraka nchini huku huduma muhimu zikikosekana katika hospitali na maskulini.
Wakati watanzania wakitarajia mengi mazuri kutoka kwa Serikali zao lakini wanapata ripoti za ubadhirifu wa baadhi ya viongozi katika Wizara, Mikoa, wilaya na taasisi mbali mbali wakifaidika kwa mishahara hewa na wengine kushindwa kutoa ankara za matumizi, wakati huku mahospitali yakiwa na uhaba wa dawa muhimu, shule na vyuo vikiwa havina nyenzo muhimu za kufundishia”, alisema Askofu Shao.
Alisema hayo hayawezi kufanyika kama hakuna utawala wa sheria, watanzania wanaotegemea huduma nzuri kwa gharama ya kodi zao hawajasikia hatua zinazochukuliwa au zilizochukuliwa dhidi ya ubadhirifu huo.
Alieleza ufufuko wa kristu ni agizo la kutafuta sababu za wengi kuwa masikini na wachache kuwa matajiri wa kupindukia katika nchi tajiri kama Tanzania, ambapo aligusia popote pale penye mateso njaa na umasikini unatokana na uvunjwaji wa haki za binadamu.
Askofu Shao alitoa wito kwa viongozi wa jamii kuangalia upya sheria za ardhi, madini na biashara katika kukuza uchumi kwa watu wote bila ya kuweka tabaka.
Aliwaeleza waumini hao kwamba, Serikali inakimbizana na wamachinga na wakulima wadogo wadogo wanaobeba mazao na bidhaa zao kichwani na migongoni kwa ajili ya kutafuta riski kwa kuwabebesha kodi kubwa huku ikiendeleza misamaha kwa wawekezaji na wafanyabiashara wakubwa, ambao wangalisaidia kunyanyua uchumi badala ya kutwishwa mzigo wadogo.
“Kodi ya mfanyabiashara anayeingiza kontena 50, muwekezaji katika hoteli au madini hawa wote wakilipa kodi uhakika kwa kipindi kifupi nchi yetu itafikia malengo ya maendeleo”, alisisitiza.
Aidha alisema, kwa miezi sita hivi kumekuwepo kwa Serikali mpya, Serikali ya Mapinduzi Zanzibar yenye muundo wa Umoja wa Kitaifa na ile ya Serikali ya Muungano Tanzania, ambapo watanzania walikuwa na matarajio makubwa ya mabadiliko hayo yataleta matumaini.
Aliongeza kusema kwamba, ni mapema mno kutoa tathmini lakini kwa kusoma alama na matukio machache, wengi wao hawajaona nia ya dhati ya kutaka mabadiliko na utayari wa baadhi ya viongozi kupokea mawazo na changamoto za wengine kwa kuona nguvu mpya, ubunifu mpya wa rika mbali mbali, vipaji tofauti na itikadi mbali mbali katika Wizara, Wilaya, Mikoa na Taasisi za Serikali.
Hata hivyo, alitoa wito kwa waumini kwamba agizo la ufufuko ni kuwaonesha watu kwa uhakika wote kwamba kristu ni Mkombozi wa dunia ameshinda maovu yote, amejenga matumaini na kwamba wote wana haki ya uhai wenye furaha.
Jana wakristo duniani kote walisherehekea maadhimisho ya kufufuka kwa kiongozi wao Yesu Kristo, baada ya kufariki siku ya Ijumaa Kuu.
ASKOFU ATAKA 'MAFISADI' WACHUKULIWE HATUA.
Askofu ataka ‘mafisadi’ wachukuliwe hatua
• Asema Serikali zifikie matumaini ya wananchi
• Haoni sababu kuwepo maskini Tanzania
Na Mwanajuma Abdi
ASKOFU Augustine Ndeliakyama Shao wa kanisa la Roman Catholic Zanzibar, amesema watanzania wanalia na kuvunjika moyo na ubadhirifu na mishahara hewa kwa baadhi ya viongozi nchini hali inayosababisha kukosekana kwa nyenzo maskulini, vyuo na uhaba wa dawa hospitalini.
Hayo aliyasema jana, katika hotuba aliyoitoa katika kanisa la Minara miwili Shangani mjini Unguja kwa waumini wa dini ya kikristo ikiwa ni ujumbe wa Pasaka 2011 ‘mwanga unaoleta uhuru kwa mwanadamu aliyekuwa kwenye giza la maovu’.
Alisema watanzania wamekata tamaa na nchi yao kutokana kusikia ubadhirifu mkubwa na upoteaji wa fedha za mishahara hewa inayofanywa na baadhi ya viongozi waliopo katika madaraka nchini huku huduma muhimu zikikosekana katika hospitali na maskulini.
“Wakati watanzania wakitarajia mengi mazuri kutoka kwa Serikali zao lakini wanapata ripoti za ubadhirifu wa baadhi ya viongozi katika Wizara, Mikoa, wilaya na taasisi mbali mbali wakifaidika kwa mishahara hewa na wengine kushindwa kutoa ankara za matumizi, wakati huku mahospitali yakiwa na uhaba wa dawa muhimu, shule na vyuo vikiwa havina nyenzo muhimu za kufundishia”, alisema Askofu Shao.
Alisema hayo hayawezi kufanyika kama hakuna utawala wa sheria, watanzania wanaotegemea huduma nzuri kwa gharama ya kodi zao hawajasikia hatua zinazochukuliwa au zilizochukuliwa dhidi ya ubadhirifu huo.
Alieleza ufufuko wa kristu ni agizo la kutafuta sababu za wengi kuwa masikini na wachache kuwa matajiri wa kupindukia katika nchi tajiri kama Tanzania, ambapo aligusia popote pale penye mateso njaa na umasikini unatokana na uvunjwaji wa haki za binadamu.
Askofu Shao alitoa wito kwa viongozi wa jamii kuangalia upya sheria za ardhi, madini na biashara katika kukuza uchumi kwa watu wote bila ya kuweka tabaka.
Aliwaeleza waumini hao kwamba, Serikali inakimbizana na wamachinga na wakulima wadogo wadogo wanaobeba mazao na bidhaa zao kichwani na migongoni kwa ajili ya kutafuta riski kwa kuwabebesha kodi kubwa huku ikiendeleza misamaha kwa wawekezaji na wafanyabiashara wakubwa, ambao wangalisaidia kunyanyua uchumi badala ya kutwishwa mzigo wadogo.
“Kodi ya mfanyabiashara anayeingiza kontena 50, muwekezaji katika hoteli au madini hawa wote wakilipa kodi uhakika kwa kipindi kifupi nchi yetu itafikia malengo ya maendeleo”, alisisitiza.
Aidha alisema, kwa miezi sita hivi kumekuwepo kwa Serikali mpya, Serikali ya Mapinduzi Zanzibar yenye muundo wa Umoja wa Kitaifa na ile ya Serikali ya Muungano Tanzania, ambapo watanzania walikuwa na matarajio makubwa ya mabadiliko hayo yataleta matumaini.
Aliongeza kusema kwamba, ni mapema mno kutoa tathmini lakini kwa kusoma alama na matukio machache, wengi wao hawajaona nia ya dhati ya kutaka mabadiliko na utayari wa baadhi ya viongozi kupokea mawazo na changamoto za wengine kwa kuona nguvu mpya, ubunifu mpya wa rika mbali mbali, vipaji tofauti na itikadi mbali mbali katika Wizara, Wilaya, Mikoa na Taasisi za Serikali.
Hata hivyo, alitoa wito kwa waumini kwamba agizo la ufufuko ni kuwaonesha watu kwa uhakika wote kwamba kristu ni Mkombozi wa dunia ameshinda maovu yote, amejenga matumaini na kwamba wote wana haki ya uhai wenye furaha.
Jana wakristo duniani kote walisherehekea maadhimisho ya kufufuka kwa kiongozi wao Yesu Kristo, baada ya kufariki siku ya Ijumaa Kuu.
• Asema Serikali zifikie matumaini ya wananchi
• Haoni sababu kuwepo maskini Tanzania
Na Mwanajuma Abdi
ASKOFU Augustine Ndeliakyama Shao wa kanisa la Roman Catholic Zanzibar, amesema watanzania wanalia na kuvunjika moyo na ubadhirifu na mishahara hewa kwa baadhi ya viongozi nchini hali inayosababisha kukosekana kwa nyenzo maskulini, vyuo na uhaba wa dawa hospitalini.
Hayo aliyasema jana, katika hotuba aliyoitoa katika kanisa la Minara miwili Shangani mjini Unguja kwa waumini wa dini ya kikristo ikiwa ni ujumbe wa Pasaka 2011 ‘mwanga unaoleta uhuru kwa mwanadamu aliyekuwa kwenye giza la maovu’.
Alisema watanzania wamekata tamaa na nchi yao kutokana kusikia ubadhirifu mkubwa na upoteaji wa fedha za mishahara hewa inayofanywa na baadhi ya viongozi waliopo katika madaraka nchini huku huduma muhimu zikikosekana katika hospitali na maskulini.
“Wakati watanzania wakitarajia mengi mazuri kutoka kwa Serikali zao lakini wanapata ripoti za ubadhirifu wa baadhi ya viongozi katika Wizara, Mikoa, wilaya na taasisi mbali mbali wakifaidika kwa mishahara hewa na wengine kushindwa kutoa ankara za matumizi, wakati huku mahospitali yakiwa na uhaba wa dawa muhimu, shule na vyuo vikiwa havina nyenzo muhimu za kufundishia”, alisema Askofu Shao.
Alisema hayo hayawezi kufanyika kama hakuna utawala wa sheria, watanzania wanaotegemea huduma nzuri kwa gharama ya kodi zao hawajasikia hatua zinazochukuliwa au zilizochukuliwa dhidi ya ubadhirifu huo.
Alieleza ufufuko wa kristu ni agizo la kutafuta sababu za wengi kuwa masikini na wachache kuwa matajiri wa kupindukia katika nchi tajiri kama Tanzania, ambapo aligusia popote pale penye mateso njaa na umasikini unatokana na uvunjwaji wa haki za binadamu.
Askofu Shao alitoa wito kwa viongozi wa jamii kuangalia upya sheria za ardhi, madini na biashara katika kukuza uchumi kwa watu wote bila ya kuweka tabaka.
Aliwaeleza waumini hao kwamba, Serikali inakimbizana na wamachinga na wakulima wadogo wadogo wanaobeba mazao na bidhaa zao kichwani na migongoni kwa ajili ya kutafuta riski kwa kuwabebesha kodi kubwa huku ikiendeleza misamaha kwa wawekezaji na wafanyabiashara wakubwa, ambao wangalisaidia kunyanyua uchumi badala ya kutwishwa mzigo wadogo.
“Kodi ya mfanyabiashara anayeingiza kontena 50, muwekezaji katika hoteli au madini hawa wote wakilipa kodi uhakika kwa kipindi kifupi nchi yetu itafikia malengo ya maendeleo”, alisisitiza.
Aidha alisema, kwa miezi sita hivi kumekuwepo kwa Serikali mpya, Serikali ya Mapinduzi Zanzibar yenye muundo wa Umoja wa Kitaifa na ile ya Serikali ya Muungano Tanzania, ambapo watanzania walikuwa na matarajio makubwa ya mabadiliko hayo yataleta matumaini.
Aliongeza kusema kwamba, ni mapema mno kutoa tathmini lakini kwa kusoma alama na matukio machache, wengi wao hawajaona nia ya dhati ya kutaka mabadiliko na utayari wa baadhi ya viongozi kupokea mawazo na changamoto za wengine kwa kuona nguvu mpya, ubunifu mpya wa rika mbali mbali, vipaji tofauti na itikadi mbali mbali katika Wizara, Wilaya, Mikoa na Taasisi za Serikali.
Hata hivyo, alitoa wito kwa waumini kwamba agizo la ufufuko ni kuwaonesha watu kwa uhakika wote kwamba kristu ni Mkombozi wa dunia ameshinda maovu yote, amejenga matumaini na kwamba wote wana haki ya uhai wenye furaha.
Jana wakristo duniani kote walisherehekea maadhimisho ya kufufuka kwa kiongozi wao Yesu Kristo, baada ya kufariki siku ya Ijumaa Kuu.
MAMA SHEIN; WANACCM CHAGUENI VIONGOZI WAKWELI WAADILIFU.
Mama Shein: WanaCCM chagueni viongozi wakweli, waadilifu
Na Mwanajuma Abdi
MKE wa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mama Mwanamwema Shein amewataka wanaCCM kuchagua viongozi waadilifu na wakweli katika uchaguzi wa chama hicho mwakani kwa ajili ya kujiandaa na ushindi wa uchaguzi mkuu wa 2015.
Mama Shein aliyasema hayo jana, katika viwanja vya skuli ya Kiongoni Makunduchi kwenye mkutano maalum wa wanavikundi vya ushirika vya SACCOS katika shehia mbali mbali, ambapo ikiwa ni sambamba na ziara ya siku moja ya kuwashukuru wananchi wa Jimbo la Makunduchi kwa kukipatia ushindi chama hicho katika uchaguzi wa mwaka jana.
Mapema alitembelea na kuweka jiwe la msingi ya Mwelekeo Mwema SACCOS ya Mtende, ambapo alichangia shilingi 300,000 na kufungua ofisi ya Mkombozi SACCOS ya Kizimkazi Dimbani pia alikabidhi shilingi 200,000 kwa ajili ya kuendeleza mtaji wa ushirika huo pamoja na kukutana na vikundi ya ushirika vya shehia ya mbali mbali huko Kiongoni Makunduchi.
Alisema wanaCCM wajiandae na uchaguzi wa ndani ya Chama hicho utaofanyika mwakani ili kuweza kuchagua viongozi wataoweza kuendeleza ushindi katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2015, pamoja na kuwahimiza wazazi kuwashajiisha vijana waliofikia umri wa kwenda kujiandikisha katika daftari la wapiga kura waende.
Alieleza uchaguzi umemalizika kwa utulivu na amani, ambao umeendeshwa kwa uhuru na haki na kufanikisha kushika madaraka Rais wa Zanzibar Dk. Ali Mohamed Shein, hali ambayo umesaidia ulimwengu mzima kuipongeza nchi kwa mafanikio makubwa yaliyofikiwa katika kudumisha amani nchini, hivyo alisisitiza umoja na mshikamano uendele kuwepo kwa ajili ya maendeleo endelevu.
Akizungumzia kuhusu SACCOS, alisema Serikali inatambua mchango mkubwa wa kinamama na akinababa kupitia vikundi vya ushirika na ndio maana ikawekwa Wizara maalum ya kushughulikia masuala hayo kwa ajili ya kukuza uchumi na kupunguza umasikini.
Alisema wananchi wamejikita katika masuala ya kuwanyanyua kiuchumi katika sekta mbali mbali zikiwemo za kilimo, biashara na ufugaji, ambapo hiyo ni hatua kubwa katika kuwakomboa na umasikini.
Aliwapongeza wanaSACCOS hao kwa juhudi zao kubwa za kuanzisha ushirika huo katika kujikomboa kiuchumi na kimaisha, ambapo aliwahimiza wadumishe umoja na mashirikiano kwani bila hayo hawatoweza kufikia malengo waliyojipangia.
Mama Mwanamwema Shein aliwahimiza wanaSACCOS kuwa wawazi katika masuala ya fedha ili ushirika huo uweze kupiga hatua, sambamba na kuwashajiisha wanaokopa warudishe pesa kwa wakati ili na wenzao wakopeshwe.
Nae Mke wa Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Mama Asha Seif Iddi, aliahidi kuwasaidia matreki suti kwa kikundi cha mazoezi cha Kizimkazi Dimbani, pamoja na kutoa wito kwa vikundi vya Ushirika kuungana pamoja ili wawe wengi na waweze kukopesheka katika mabenki.
Waziri wa Kazi, Uwezeshaji wananchi, Kiuchumi na Ushirika ambae pia ni Mwakilishi wa Jimbo la Makunduchi, Haroun Ali Suleiman alitilia mkazo umuhimu wa kuunganisha vikundi vya ushirika ili vifikie vitatu vikubwa katika Jimbo hilo kwa lengo la kupata misaada mingi na kuweza kukopesheka katika mabenki.
Alisema katika jimbo hilo wanaCCM hawana masihara, ambapo wanapotoa ahadi lazima watimize kwa kuwapa kura zote wagombea wa Chama cha Mapinduzi kama walivyofanya uchaguzi uliopita na ujao utakuwa hivyo hivyo.
Mapema wakisoma risala zao wanaSACCOS wa Kijiji cha Mtende, Makunduchi na Kizimkazi Dimbani walimshukuru Mama Mwanamwema Shein kwa kutimiza ahadi yake ya kwenda kuwashukuru baada ya kumaliza uchaguzi mkuu mwaka jana.
Hata hivyo baadhi ya wanaSACCOS walitaka kusaidiwa kupatiwa mafunzo, nyenzo za kumaliza jengo lao pamoja na kuongezewa mitaji, ambapo pia waliwapongeza Rais wa Tanzania Dk. Jakaya Mrisho Mrisho na Rais wa Zanzibar Dk. Ali Mohamed Shein kwa kutimia miaka 47 ya Muungano wa Tanzania.
Nao kikundi cha michezo, waliwashajiisha wananchi kufanya mazoezi kwa ajili ya kujiweka vizuri kiafya na kuondokana kuonana na daktari mara kwa mara wakisumbuliwa maradhi mbali mbali.
Na Mwanajuma Abdi
MKE wa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mama Mwanamwema Shein amewataka wanaCCM kuchagua viongozi waadilifu na wakweli katika uchaguzi wa chama hicho mwakani kwa ajili ya kujiandaa na ushindi wa uchaguzi mkuu wa 2015.
Mama Shein aliyasema hayo jana, katika viwanja vya skuli ya Kiongoni Makunduchi kwenye mkutano maalum wa wanavikundi vya ushirika vya SACCOS katika shehia mbali mbali, ambapo ikiwa ni sambamba na ziara ya siku moja ya kuwashukuru wananchi wa Jimbo la Makunduchi kwa kukipatia ushindi chama hicho katika uchaguzi wa mwaka jana.
Mapema alitembelea na kuweka jiwe la msingi ya Mwelekeo Mwema SACCOS ya Mtende, ambapo alichangia shilingi 300,000 na kufungua ofisi ya Mkombozi SACCOS ya Kizimkazi Dimbani pia alikabidhi shilingi 200,000 kwa ajili ya kuendeleza mtaji wa ushirika huo pamoja na kukutana na vikundi ya ushirika vya shehia ya mbali mbali huko Kiongoni Makunduchi.
Alisema wanaCCM wajiandae na uchaguzi wa ndani ya Chama hicho utaofanyika mwakani ili kuweza kuchagua viongozi wataoweza kuendeleza ushindi katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2015, pamoja na kuwahimiza wazazi kuwashajiisha vijana waliofikia umri wa kwenda kujiandikisha katika daftari la wapiga kura waende.
Alieleza uchaguzi umemalizika kwa utulivu na amani, ambao umeendeshwa kwa uhuru na haki na kufanikisha kushika madaraka Rais wa Zanzibar Dk. Ali Mohamed Shein, hali ambayo umesaidia ulimwengu mzima kuipongeza nchi kwa mafanikio makubwa yaliyofikiwa katika kudumisha amani nchini, hivyo alisisitiza umoja na mshikamano uendele kuwepo kwa ajili ya maendeleo endelevu.
Akizungumzia kuhusu SACCOS, alisema Serikali inatambua mchango mkubwa wa kinamama na akinababa kupitia vikundi vya ushirika na ndio maana ikawekwa Wizara maalum ya kushughulikia masuala hayo kwa ajili ya kukuza uchumi na kupunguza umasikini.
Alisema wananchi wamejikita katika masuala ya kuwanyanyua kiuchumi katika sekta mbali mbali zikiwemo za kilimo, biashara na ufugaji, ambapo hiyo ni hatua kubwa katika kuwakomboa na umasikini.
Aliwapongeza wanaSACCOS hao kwa juhudi zao kubwa za kuanzisha ushirika huo katika kujikomboa kiuchumi na kimaisha, ambapo aliwahimiza wadumishe umoja na mashirikiano kwani bila hayo hawatoweza kufikia malengo waliyojipangia.
Mama Mwanamwema Shein aliwahimiza wanaSACCOS kuwa wawazi katika masuala ya fedha ili ushirika huo uweze kupiga hatua, sambamba na kuwashajiisha wanaokopa warudishe pesa kwa wakati ili na wenzao wakopeshwe.
Nae Mke wa Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Mama Asha Seif Iddi, aliahidi kuwasaidia matreki suti kwa kikundi cha mazoezi cha Kizimkazi Dimbani, pamoja na kutoa wito kwa vikundi vya Ushirika kuungana pamoja ili wawe wengi na waweze kukopesheka katika mabenki.
Waziri wa Kazi, Uwezeshaji wananchi, Kiuchumi na Ushirika ambae pia ni Mwakilishi wa Jimbo la Makunduchi, Haroun Ali Suleiman alitilia mkazo umuhimu wa kuunganisha vikundi vya ushirika ili vifikie vitatu vikubwa katika Jimbo hilo kwa lengo la kupata misaada mingi na kuweza kukopesheka katika mabenki.
Alisema katika jimbo hilo wanaCCM hawana masihara, ambapo wanapotoa ahadi lazima watimize kwa kuwapa kura zote wagombea wa Chama cha Mapinduzi kama walivyofanya uchaguzi uliopita na ujao utakuwa hivyo hivyo.
Mapema wakisoma risala zao wanaSACCOS wa Kijiji cha Mtende, Makunduchi na Kizimkazi Dimbani walimshukuru Mama Mwanamwema Shein kwa kutimiza ahadi yake ya kwenda kuwashukuru baada ya kumaliza uchaguzi mkuu mwaka jana.
Hata hivyo baadhi ya wanaSACCOS walitaka kusaidiwa kupatiwa mafunzo, nyenzo za kumaliza jengo lao pamoja na kuongezewa mitaji, ambapo pia waliwapongeza Rais wa Tanzania Dk. Jakaya Mrisho Mrisho na Rais wa Zanzibar Dk. Ali Mohamed Shein kwa kutimia miaka 47 ya Muungano wa Tanzania.
Nao kikundi cha michezo, waliwashajiisha wananchi kufanya mazoezi kwa ajili ya kujiweka vizuri kiafya na kuondokana kuonana na daktari mara kwa mara wakisumbuliwa maradhi mbali mbali.
WANAFUNZI WASIO WALEMAVU KUFUNDISHWA LUGHA YA ALAMA.
Wanafunzi wasio walemavu kufundishwa lugha ya alama
Na Halima Abdalla
WIZARA ya Elimu na Mafunzo ya Amali kwa kushirikiana na Jumuia ya Watu wenye ulemavu wa akili Zanzibar (ZPDD), imeandaa mafunzo juu ya ufahamu wa lugha za alama kwa wanafunzi ili yaweze kuwa na mawasiliano ya karibu kati ya wanafunzi waliokuwa viziwi na wasio viziwi wanapokuwa darasani.
Akizungumza na waandishi wa habari skuli ya Mwanakwerekwe ‘F’, Msimamizi wa mafunzo ya lugha za alama Ameir Khatib Hassan, alisema mafunzo haya yanasaidia sana kupata uelewa na ufahamu kwa wanafunzi waliokuwa viziwi na wasiokuwa viziwi kuweza kuwasiliana pamoja na mwalimu anapofundisha kuweza kuelewana.
Aidha alisema wanafunzi wanapopatiwa elimu ya lugha za alama inasaidia kuhamasika kutokana na ule mchanganyiko kwa wanafunzi wanapokuwa madarasani na kuzungumza kwa lugha za alama na kujenga ukaribu na urafiki kati yao.
Nae mwalimu wa lugha za alama katika Skuli ya Mwanakwerekwe ‘F’, Kazija Khatib Juma, alisema wanapofundisha lugha za alama wakiwa madarasani wanakabiliwa na ukosefu wa vifaa vya ufundishaji kwa wanafunzi viziwi ikiwemo kioo cha kuweza kuona matamshi yanavyotoka na kuweza kumsaidia mwanafunzi kufahamu.
Aidha alisema wanakabiliwa na uhaba wa vifaa vya kukalia baadhi ya madarasa wanafunzi wanalazimika kukaa chini kutokana na kukosekana kwa madawati.
Kwa upande wake Msaidizi Mwalimu Mkuu wa Skuli ya Mwanakwerekwe ‘F’, Asha Mtaji Hassan, alisema idadi ya wanafunzi wenye mahitaji maalum katika skuli yake kila mwaka inaongezeka ukilinganisha na miaka ya nyuma ambapo wazazi walikuwa hawako tayari kuwatoa watoto wao kwa ajili ya kupata elimu.
Alisema kwa sasa wazazi na walimu wamekuwa na ushirikiano mzuri na wa karibu na wazee wamekuwa wakifuatilia vizuri maendeleo ya watoto wao.
Alisema mpaka sasa katika skuli yake robo tatu ya walimu wote wameshapatiwa mafunzo ya lugha za alama na pia wamekuwa na kipindi maalum kwa ajili ya kufundishana kwa walimu wote.
Aidha alitoa wito kwa Wizara ya Elimu kujali hali ya watoto wenye mahitaji maalum pamoja na kuthamini kitengo cha elimu mjumuisho.
Katika mafunzo hayo jumla ya wanafunzi 101 walipatiwa mafunzo hayo ya lugha za alama ikiwemo watatu kutoka Skuli ya Darajani, watatu kutoka Dimani na 95 kutoka skuli ya mwanakwerekwe ‘F’.
Mafunzo hayo ya siku tano yameandaliwa na Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali kwa kushirikiana na Jumuia ya watu wenye ulemavu wa akili Zanzibar (ZPDD), chini ya ufadhili wa shirika la (NFU) kutoka Norway.
Na Halima Abdalla
WIZARA ya Elimu na Mafunzo ya Amali kwa kushirikiana na Jumuia ya Watu wenye ulemavu wa akili Zanzibar (ZPDD), imeandaa mafunzo juu ya ufahamu wa lugha za alama kwa wanafunzi ili yaweze kuwa na mawasiliano ya karibu kati ya wanafunzi waliokuwa viziwi na wasio viziwi wanapokuwa darasani.
Akizungumza na waandishi wa habari skuli ya Mwanakwerekwe ‘F’, Msimamizi wa mafunzo ya lugha za alama Ameir Khatib Hassan, alisema mafunzo haya yanasaidia sana kupata uelewa na ufahamu kwa wanafunzi waliokuwa viziwi na wasiokuwa viziwi kuweza kuwasiliana pamoja na mwalimu anapofundisha kuweza kuelewana.
Aidha alisema wanafunzi wanapopatiwa elimu ya lugha za alama inasaidia kuhamasika kutokana na ule mchanganyiko kwa wanafunzi wanapokuwa madarasani na kuzungumza kwa lugha za alama na kujenga ukaribu na urafiki kati yao.
Nae mwalimu wa lugha za alama katika Skuli ya Mwanakwerekwe ‘F’, Kazija Khatib Juma, alisema wanapofundisha lugha za alama wakiwa madarasani wanakabiliwa na ukosefu wa vifaa vya ufundishaji kwa wanafunzi viziwi ikiwemo kioo cha kuweza kuona matamshi yanavyotoka na kuweza kumsaidia mwanafunzi kufahamu.
Aidha alisema wanakabiliwa na uhaba wa vifaa vya kukalia baadhi ya madarasa wanafunzi wanalazimika kukaa chini kutokana na kukosekana kwa madawati.
Kwa upande wake Msaidizi Mwalimu Mkuu wa Skuli ya Mwanakwerekwe ‘F’, Asha Mtaji Hassan, alisema idadi ya wanafunzi wenye mahitaji maalum katika skuli yake kila mwaka inaongezeka ukilinganisha na miaka ya nyuma ambapo wazazi walikuwa hawako tayari kuwatoa watoto wao kwa ajili ya kupata elimu.
Alisema kwa sasa wazazi na walimu wamekuwa na ushirikiano mzuri na wa karibu na wazee wamekuwa wakifuatilia vizuri maendeleo ya watoto wao.
Alisema mpaka sasa katika skuli yake robo tatu ya walimu wote wameshapatiwa mafunzo ya lugha za alama na pia wamekuwa na kipindi maalum kwa ajili ya kufundishana kwa walimu wote.
Aidha alitoa wito kwa Wizara ya Elimu kujali hali ya watoto wenye mahitaji maalum pamoja na kuthamini kitengo cha elimu mjumuisho.
Katika mafunzo hayo jumla ya wanafunzi 101 walipatiwa mafunzo hayo ya lugha za alama ikiwemo watatu kutoka Skuli ya Darajani, watatu kutoka Dimani na 95 kutoka skuli ya mwanakwerekwe ‘F’.
Mafunzo hayo ya siku tano yameandaliwa na Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali kwa kushirikiana na Jumuia ya watu wenye ulemavu wa akili Zanzibar (ZPDD), chini ya ufadhili wa shirika la (NFU) kutoka Norway.
RED CROSS YATUMIA 150/= KUCHIMBA VISIMA PEMBA.
Red Cross yatumia 150m/- kuchimba visima Pemba
Na Yussuf Hamad, Pemba
ZAIDI ya shilingi 150 milioni zimetumiwa na chama cha Msalaba Mwekundu Tanzania (Red Cross), kwa ajili ya kuchimba visima 30 vya pampu za mkono katika katika Shehia na Vijiji mbali mbali wilaya nne za Pemba.
Akitoa taarifa za uchimbaji wa visima katika sherehe za kufunga mradi wa maji na Usafi wa mazingira huko Mfikiwa nje kidogo ya mji wa Chake Chake Kisiwani Pemba, msimamizi Mkuu wa mradi huo Mohammed Ali Saleh, alisema mradi huo uliochukuwa miaka mitatu na umewanufaisha zaidi ya wananchi 15,000.
Alisema mradi ulilenga kuondoa tatizo la maji katika maeneo ambayo huduma hiyo inapatikana kwa wananchi kuifuata umbali mrefu au haipatikani kabisa.
“Ili wananchi wachimbiwe kisima ni lazima waandike barua ya maombi kwa Red-Cross Pemba, na sisi baadae tunapeleka wataalamu wetu kwenda katika kijiji kuona hali halisi ya tatizo la maji tukiona lipo tatizo basi tunasaidia”alifafanua.
Mohammed, alisema mchango wa jamii katika kazi ya uchimbaji wa kisima ni nguvu kazi yao, na kuongeza kuwa hivyo imewafanya wajenge imani kwamba miradi hiyo ni yao.
Alifafanuwa kuwa kisima kimoja kimekuwa kikigharimu kati ya shilingi milioni tatu hadi milioni sita kulingana na ukubwa wa kisima kilivyo.
Alivitaja idadi ya visima hivyo vilivyochimbwa kuwa wilaya ya Mkoani visima 13, wilaya ya Chake Chake visima sita, wilaya ya Wete visima 7 na wilaya ya Micheweni visima sita.
“Visima vingi tumevichimba Shehia na Vijiji ambavyo maji ya bomba hayajafika, tumefanya hivyo ili kuwaepusha wananchi kuendelea kutumia maji yasio salama “alieleza.
Akizungumza katika Sherehe hizo, Mkuu wa Mkoa wa Kusini Pemba, Juma Kasim Tindwa, alisifu juhudi zinazochukuliwa na Red Cross katika kuwapatia wananchi maji safi na salama.
Alisema maji ni muhimu kawa maisha ya binadamu na viumbe wengine, hivyo juhudi hizo zinafaa kuendelezwa na wananchi wenyewe kwa kuvitunza visima hivyo ili viweze kutumika kwa kipindi kirefu kijacho.
“Nyinyi Red Cross sio tu mnawasaidia tu watu bali pia mmeunga mkono juhudi za Serikali, kwani Sera ya Serikali imetamka wazi kwamba kila mwananchi atapatiwa huduma ya maji safi na salama “alifafanua Tindwa.
Tindwa alisema Serikali itaendelea kuunga mkono juhudi za Red Cross, pale ambapo wanahitaji msaada wa Serikali kwa lengo la kuwawezesha kutoa huduma bora kwa wananchi.
Mapema katika risala yao wanachama wa Red Cross wa Mikoa miwili ya Pemba wameiomba Serikali kuwapatia nafasi za ajira pale panapotokea mahitaji Serikalini ili waweze kujikimu kimaisha kwani kazi wanazozifanya katika chama chao ni ya kujitolea.
Na Yussuf Hamad, Pemba
ZAIDI ya shilingi 150 milioni zimetumiwa na chama cha Msalaba Mwekundu Tanzania (Red Cross), kwa ajili ya kuchimba visima 30 vya pampu za mkono katika katika Shehia na Vijiji mbali mbali wilaya nne za Pemba.
Akitoa taarifa za uchimbaji wa visima katika sherehe za kufunga mradi wa maji na Usafi wa mazingira huko Mfikiwa nje kidogo ya mji wa Chake Chake Kisiwani Pemba, msimamizi Mkuu wa mradi huo Mohammed Ali Saleh, alisema mradi huo uliochukuwa miaka mitatu na umewanufaisha zaidi ya wananchi 15,000.
Alisema mradi ulilenga kuondoa tatizo la maji katika maeneo ambayo huduma hiyo inapatikana kwa wananchi kuifuata umbali mrefu au haipatikani kabisa.
“Ili wananchi wachimbiwe kisima ni lazima waandike barua ya maombi kwa Red-Cross Pemba, na sisi baadae tunapeleka wataalamu wetu kwenda katika kijiji kuona hali halisi ya tatizo la maji tukiona lipo tatizo basi tunasaidia”alifafanua.
Mohammed, alisema mchango wa jamii katika kazi ya uchimbaji wa kisima ni nguvu kazi yao, na kuongeza kuwa hivyo imewafanya wajenge imani kwamba miradi hiyo ni yao.
Alifafanuwa kuwa kisima kimoja kimekuwa kikigharimu kati ya shilingi milioni tatu hadi milioni sita kulingana na ukubwa wa kisima kilivyo.
Alivitaja idadi ya visima hivyo vilivyochimbwa kuwa wilaya ya Mkoani visima 13, wilaya ya Chake Chake visima sita, wilaya ya Wete visima 7 na wilaya ya Micheweni visima sita.
“Visima vingi tumevichimba Shehia na Vijiji ambavyo maji ya bomba hayajafika, tumefanya hivyo ili kuwaepusha wananchi kuendelea kutumia maji yasio salama “alieleza.
Akizungumza katika Sherehe hizo, Mkuu wa Mkoa wa Kusini Pemba, Juma Kasim Tindwa, alisifu juhudi zinazochukuliwa na Red Cross katika kuwapatia wananchi maji safi na salama.
Alisema maji ni muhimu kawa maisha ya binadamu na viumbe wengine, hivyo juhudi hizo zinafaa kuendelezwa na wananchi wenyewe kwa kuvitunza visima hivyo ili viweze kutumika kwa kipindi kirefu kijacho.
“Nyinyi Red Cross sio tu mnawasaidia tu watu bali pia mmeunga mkono juhudi za Serikali, kwani Sera ya Serikali imetamka wazi kwamba kila mwananchi atapatiwa huduma ya maji safi na salama “alifafanua Tindwa.
Tindwa alisema Serikali itaendelea kuunga mkono juhudi za Red Cross, pale ambapo wanahitaji msaada wa Serikali kwa lengo la kuwawezesha kutoa huduma bora kwa wananchi.
Mapema katika risala yao wanachama wa Red Cross wa Mikoa miwili ya Pemba wameiomba Serikali kuwapatia nafasi za ajira pale panapotokea mahitaji Serikalini ili waweze kujikimu kimaisha kwani kazi wanazozifanya katika chama chao ni ya kujitolea.
Tuesday, 19 April 2011
WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI, UTALII NA MICHEZO JIHADI
WAZIRI wa Habari, Utamaduni, Utaliina Michezo Abdilah Jihad Hassan, akitowa maelekezo kwa watendaji wake katika ghala pango la Watumwa Mangapwani alipofanya ziara kutembelea sehemu mbalimbali za magofu ya Kitalii jana.(Picha Masangu Abdalla)
Subscribe to:
Posts (Atom)