Tuesday 1 March 2011

Wanafunzi wa kike wasimamishwa masomo kwa kuweka nywele dawa

Wanafunzi wa kike wasimamishwa masomo kwa kuweka nywele dawa

Na Ismail Mwinyi

WANAFUNZI wa darasa la saba na kitado cha pili katika skuli ya Kijitoupele wilaya ya Magharibi Unguja, wamesimamishwa masomo baada ya kukutwa na makosa ya kutia dawa nywele na kujitia vipodozi usoni.

Hatua hiyo imekuja kufuatia mzazi mmoja wa mwanafunzi kuwa na wasiwasi kwa mtoto wake kutokana na mabadiliko aliyokuwa nayo.

Akizungumza na gazeti hili, Msaidizi wa Mwalimu Mkuu wa Skuli hiyo, Makame Hana Ali, alisema hivi sasa wanafanya upekuzi kwa wanafunzi wa kike kwa sababu wanafunzi hano ni wakorofi zaidi.

Alisema wamewarudisha nyumbani wanafunzi hao kwa ajili ya kuwaeleza wazazi wao ili waje kulizungumza suala hilo kwa pamoja na walimu na kulipatia ufumbuzi unaofaa.

Hana alisema wanafunzi waliorejesha nyumbani 20 ambao wote wanahusika na kufanya makosa hayo kinyume na utaratibu wa skuli.

Alisema opereshini hiyo ni ya kudumu na ambayo itafanyika kila baada ya mienzi sita ambapo wanafunzi wa kike watafanyiwa ukaguzi ili kuhakikisha makosa hayo yanatoweka kabisa katika skuli hiyo.

No comments:

Post a Comment