Friday 26 March 2010

Biashara ya vinyago kupigwa marufuku Mjimkongwe

Na Mwantanga Ame
BIASHARA ya vinyago katika maeneo ya Mji Mkongwe ipo hatarini kufutwa kuendelea kufanyika katika Mji huo baada ya kuonekana itaharibu soko la utalii wa Zanzibar.

Hilo limebainishwa juzi jioni baada ya Mwakilishi wa Chama cha CUF Zakia Omar, kuliambia baraza hilo kuwa biashara hiyo inafaa kuondolewa katika Mji huo ili kulinda Soko la Utalii la Zanzibar.

Hoja ya Mwakilishi huyo ilikuja wakati akichangia mswada wa kufuta sheria ya Mamlaka ya Hifadhi na Uendelezaji wa Mji Mkongwe, pamoja na mambo mengine yanayohusiana na hayo.

Mwakilishi huyo akichangia alisema wakati serikali ikiwa tayari imeamua kubadili sheria hiyo ni lazima iliangalie suala la biashara ya uuzaji wa vinyago kwani inaweza ikasababisha soko la watalii wanaokuja Zanzibar ikapungua.

Akifafanua kauli yake hiyo alisema watalii wengi wanaokuja Zanzibar, huwa tayari wanatokea katika vivutio vya utalii vilivyopo Arusha ambapo kwa kiasi kikubwa soko la vinyago huwa vimejaa kwa wingi.

No comments:

Post a Comment