Monday 29 March 2010

Wenye ulemavu wapewa mafunzo kujikinga na VVU

Na Jafar Abdalla, Pemba
MIKUSANYIKO isiyokuwa ya lazima na isiyo salama kwa jamii inaweza kuchangia kwa kiasi kikubwa ongezeko la maambukizi mapya virusi vinavyosababisha UKIMWI.

Hayo yameelezwa katika mafunzo ya siku tatu kwa watoto wenye ulemavu wa usikivu na mabubu kutoka Wilaya zote za Pemba yaliyofanyika ukumbi wa Afisi ya Waziri Kiongozi kisiwani humo.

Mwezeshaji Muhammed Said alisema, mafunzo hayo yanalenga kuwakinga watoto wenye walemavu na kupata maambukizi mapya ya VVU.

Mohammed alisema kuna uwezekano wa kuwaepusha watoto na makali ya UKIMWI kwa kuwajenga tabia ya kupima afya mara kwa mara pamoja na kuwapatia huduma waazostahiki watoto wanaobainika kuwa wameambukizwa.

Nao washiriki wa mafunzo hayo ambao ni walemavu wa usikivu na mabubu wameziomba taasisi zinazojishughulisha na utoaji elimu kuhusu UKIMWI kuendelea kuwapatia elimu kuhusiana na tatizo hilo ili waongeze kasi ya kujikinga na kuwakinga wengine.

No comments:

Post a Comment