Thursday 25 March 2010

Vifaa vya MACEMP vyahujumiwa

Na Husna Mohammed
BAADHI ya wanavikundi waliopewa vifaa vya Uvuvi Kupitia Mradi wa Usimamizi wa Mazingira ya Ukanda wa Pwani (MACEMP), wamedaiwa kuvihujumu kwa kuviuza kwa bei chee kwa maslahi binafsi.
 
Hayo aliyasema jana Meneja wa MACEMP Unguja, Sheha Idrissa Hamdani, huko katika Hoteli ya Bwawani Mjini Unguja, katika kikao cha Wenyeviti wa Kamati za Uvuvi Unguja.

Wananchi katika maeneo mbali mbali Unguja na Pemba wamegaiwa vifaa kadhaa vya Uvuvi kupitika Kamati za Uvuvi kwenye Shehia zao ikiwa ni jitihada ya Serikali kupitia mradi huo kuwaondoshea wananchi umasikini wa kipato.
 
Hata hivyo, baadhi ya Kamati hizo wanadaiwa wameviuza na kasha kutafuna fedha hizo na kuvunja matarajio ya mradi huo ya kupambana na umasikini. (Kwa habari zaidi soma Zanzibar Leo)

No comments:

Post a Comment