Thursday 25 March 2010

'Hakuna mwenye hatimiliki ya Jimbo'

Na Mwantanga ame
WAKATI hofu ya kuporwa majimbo ikizidi kutanda kwa Wawakilishi na Wabunge wanaoyashikilia Majimbo hivi sasa, kigogo wa juu wa Chama Cha Mapinduzi amewataka wakongwe wenye majimbo hayo wasiwawekee nongwa kwa vile ni haki yao kuwania nafasi hizo.

Hatua ya kiongozi huyo imekuja baada ya kuanza kubainika kuwapo kwa makundi makubwa ya wanachama wa CCM wanaonyesha nia ya kutaka kunyakua majimbo ya Wajumbe waliopo sasa.

Kuanza kwa kashkash hizo tayari imebainika baadhi ya Wawakilishi na Wabunge wapo katika hali ngumu kiasi ambacho watahitaji kufanya kazi ya ziada ili kuweza kurudi katika majimbo yao.

Akizungumza na Wananchi katika Jimbo la Kitope wakati akimkaribisha Waziri wa Nchi Afisi ya Rais Katiba na Utawala Bora, Ramadhan Abdalla Shaaban, katika sherehe ya kuzawadia wanafunzi wa Jimbo hilo Mkuu wa Wilaya ya Kaskazini 'B' ambaye pia ni Katibu wa Itikadi na Ueneezi Vuai Ali Vuai alisema kuwa hakuna haja ya kununa kwa viongozi hao. (Kwa habari zaidi soma Zanzibar Leo).

No comments:

Post a Comment