Friday 26 March 2010

China yasaidia kuimarisha sekta ya Afya Zanzibar

Na Ali Mohamed, Maelezo
SERIKALI ya Mapinduzi Zanzibar imesifu mashirikiano yaliyopo baina na Zanzibar na Serikali ya Jamhuri ya Watu wa China katika sekta ya Afya na kueleza kuwa mashirikiano hayo yatazidi kuimarika.


WAZIRI wa Afya na Usatawi wa Jamii Sultan Mohamed Mugheir aliyasema hayo Vuga mjini Zanzibar alipofungua rasmi nyumba ya timu ya wataalamu wa Afya kutoka China iliyofanyiwa matengenezo makubwa hivi karibuni.


Aliyaelezea mashirikiano hayo kuwa yamesadia kwa kiasi kikubwa kuimarika kwa huduma za Afya nchini kupitia kwa wataalamu hao wa China.

Alisema kufunguliwa kwa nyumba hiyo na nyumba nyengine iliyopo Kisiwani Pemba ambayo ipo katika hatua za mwisho kukamilika kutawawezesha wataalamu hao wa China kufanya kazi vyema za kutoa huduma za Afya nchini.

Nae Mshauri Mkuu wa timu hiyo ya wataalamu wa China hapa Zanzibar Li Yiping alisema China ilianza mashirikino na Zanzibar tangu mwaka 1964 na aliyaelezea mashirikiano hayo kuwa ni yamafanikio makubwa.

No comments:

Post a Comment