Friday 26 March 2010

Mtambwe wahamasika kujiandikisha

Na Bakari Mussa , Pemba
Wananchi wapatao 5357 wa Jimbo la Mtambwe , wamejiandikisha katika Daftari la kudumu la Wapiga kura linaloendelea Kisiwani Pemba.

Kazi hiyo inakwenda kwa kasi kubwa sambamba na kutawaliwa na amani na utulivu licha ya Wananchi wengi kuhamasika na zoezi hilo la marejeo baada ya awamu ya kwanza kutojitokeza katika vituo hivyo.

Habari zilizopatikana kutoka Afisi ya Tume ya Uchaguzi zinaeleza kuwa katika Wilaya ya Wete Mkoa wa Kaskazini Pemba, wananchi wamekuwa na hamasa kubwa katika zoezi hilo tafauti na awamu ya kwanza ambapo waliojitokeza walikuwa wachache .

Kwa mujibu wa Afisa Uandkishaji Wilaya ya wete, Bakar Suleiman Ali ni kuwa kati ya wananchi waliojiandikisha katika Jimbo hilo Wanawake walikuwa 2935 na wanaume 2422.( Kwa habari zaidi soma Zanzibar Leo)

No comments:

Post a Comment