Wednesday 14 July 2010

Dk. Karume amtumia rambirambi Museveni

Na Rajab Mkasaba Ikulu
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Amani Abeid Karume amemtumia salam za rambirambi Rais Yoweri Kaguta Museven kufuatia vifo vya zaidi ya watu 70 na wengine 70 kujeruhiwa vilivyotokea nchini Uganda kutokana na shambulio la bomu.

Katika salamu hizo za rambirambi kufuatia vifo hivyo vilivyotokea nchini Uganda. Rais Karume alieleza kuwa kwa niaba yake pamoja na wananchi wa Zanzibar wanaungana pamoja na ndugu zao wa Uganda katika kuomboleza msiba huo mkubwa.

Salamu hizo zilieleza kuwa Rais Karume amepokea kwa mshtuko mkubwa taarifa hiyo ya vifo na kuwaombea malazi mema wale wote waliopoteza maisha yao na kuwaombea kwa Mwenyezi Mungu kupata nafuu ya haraka kwa wote waliopata majeraha.

No comments:

Post a Comment