Tuesday 27 July 2010

Mkaazi Mtemani ajinyonga

Na Zuhra Msabah, Pemba
SIKU saba baada ya tukio la kuinyonga Suleiman Hamad (65), mkaazi wa Wete, kijana mwengine mwenye umri wa miaka 23 mkaazi wa Mtemani naye juzi alijinyonga.

Kamanda wa Polisi Mkoa Kaskazini Pemba,Yahya Rashid Bugi alimtaja kijana huyo aliyejiondoshea uhai ni Farouk Ali Mahadhi.

Kamanda Bugi alisema kijana huyo alikutikana keshajitia kitanzi kwa kutumia kamba ya nailoni kwenye mlango wa chumba anachoishi kwenye nyumba za maendeleao Matemani.

Alisema tukio la kujinyonga kwa Farouk liliripotiwa na mwenziwe anayeishi naye nyumba Salum Khamis ambaye baada ya kuukuta mwili wa wake ukining'inia alitoa ripoti ambao walifika kuuchukua mwili ho na kuupeleka hospitali kwa uchunguzi.

"Baada ya upekuzi kwenye chumba cha marehemu tuliikuta sumu ya panya iliyokorogwa ndani ya kikombe ambayo haijawahi kuywewa", alisema kamanda Bugi.

Alisema chanzo cha kujinyonga kwa kujana huyo bado hakijajulikana na uchunguzi umeanza ambapo jana mwili huo ulikabidhiwa kwa jamaa zake kwa mazishi.

Wiki iliyopita katika kijiji cha Selem, mzee Suleiman Hamad alijinyonga kwa kutumia seruni akidaiwa mgonjwa wa akili.

No comments:

Post a Comment