Wednesday 28 July 2010

Mchakato wa uchaguzi usidhoofishe CCM- Shamuhuna

Na Abdi Shamnah
WAJUMBE wa Mkutano mkuu wa UWT Mkoa wa Kaskazini Unguja, unaowachagua Wawakilishi na Wabunge kupitia viti maalum, wametakiwa kuhakikisha mchakato wa uchaguzi kupitia kura za maoni, hauwagawi na kudhoofisha nguvu za CCM katika kukiletea ushindi chama hicho katika uchaguzi mkuu ujao.

Changamoto jiyo imetolewa jana na Naibu Waziri Kiongozi na Waziri wa Habari, Utamaduni na michezo Zanzibar, Ali Juma Shamuhuna wakati alipofungua mkutano huo katika ukumbi wa Chuo cha Amali Mkokotoni.

Shamuhuna amesema CCM imeweka utaratibu maalum wa kuwapata viongozi wake kwa lengo la kukijengea nguvu chama hicho kukabiliana na na mikikimikiki ya vyama vya upinzani katika chaguzi mbali mbali.

Aliwataka wanaoshiriki katika kinyang'anyiro hicho kukubali matokeo yatakayojiri na hatimae kujenga nguvu na ushirikiano wa kukiimarisha chama kiweze kufanya vyema katika uchaguzi ujao.

Alisema Jumuia ya wanawake nchini ina mtandao mpana kwa kuhusisha asilimia kubwa ya wananchi wote, hivyo, aliwataka kuitumia vyema fursa hiyo kuongeza wingi wa viongozi kupitia nafasi mbali mbali.

Alisema mafanikio ya CCM na vyama vilivyotangulia kabla yake yanatokana na umoja na harakati za akinamama,hivyo

aliwataka kujitokeza kwa wingi kuwania nafasi za kuchaguliwa badala ya kungojea nafasi za upendeleo kwani hazitoi tafsiri nzuri ya uwezo walionao.

Katika hatua nyingine, aliwakumbusha wajumbe hao umuhimu wa kushiriki katika kura ya maoni itakayoamua fumo upi umafaa utumike uundwaji wa Serikali baada ya Uhaguzi mkuu.
 
Alisema kuingia katika Serikali ya Umoja wa kitaifa haina maana ya kupoteza uongozi wa Taifa bali ni kujenga ushirikiano na vyama vya upinzani ili kuendesha nchi kwa amani na utulivu.

Alisema ili CCM iweze kupata mafanikio ya kweli ni muhimu kuchagua 'viongozi bora' watakaoweza kutekeleza kikamilifu sera za chama hicho.

Alisema pale wana CCM watakapochagua 'bora viongozi' watakuwa wamechaguwa wasikilizaji tu katika mikutano na kamwe hawatoweza kukitetea chama hicho.

Jumla ay wajumbe watano kutoka nafasi za Uwakilishi na Ubunge wanahitajika kuwakilisha mkoa huo kupitia viti maalum.aikufahamika mara mja wangapi wamejitokeza kuwaia nafasi hizo maalum.

No comments:

Post a Comment