Wednesday 14 July 2010

Wizara ya fedha kukusanya 171b/- 2010/2011

Na Halima Abdalla
WIZARA ya Fedha na Uchumi Zanzibar kwa mwaka wa fedha 2010/2011 inategemea kusimamia ukusanyaji wa mapato ya ndani yanayokadiriwa kufikia shilingi billioni 171.687.

Misaada ya kibajeti itafikia shilingi bilioni 55.236 na shilingi 211.714 kama misaada ya mikopo kutoka nje kwa ajili ya programu na miradi ya maendeleo.

Hayo yameelezwa na Waziri wa Fedha na Uchumi, DK. Mwinyi Haji Makame alipokuwa akiwasilisha bajeti wa Wizara hiyo kwa mwaka wa Fedha 2010/2011.

Alisema kwa upande wa matumiz, Wizara inaomba kuidhinishiwa jumla ya shilingi Billioni 93.616 kwa matumizi ya kawaida na maendeleo.

Aidha, alimesema Wizara ya Fedha na Uchumi itaendelea na majukumu yake ya kusimamia mwenendo wa hali ya Uchumi pamoja na kusimamia ukusanyaji wa mapato kutoka vyanzo vya ndani na nje ya Nchi ili kudhibiti matumizi ya Serikali.

DK. Mwinyi Haji alisema pia katika kuratibu utekelezaji wa MKUZA na Mkakati wa Ukuzaji Uchumi pia itaimarisha hali ya watenda kazi kiutendaji na kitalamu na kuendelea kusimamia mali za Serikali pamoja na kulipa mafao ya uzeeni kwa wastaafu.

Alisema kwa mwaka 2010/2011 Wizara ya Fedha na Uchumi itasimamia ujenzi unaoendelea wa majengo ya Wizara na Taasisi zake,ikiwemo jengo la Afisi huko Pemba ,Afisi mpya ya ZRB hapo Mazizini,Afisi mpya ya BIMA, Maisara, jengo la Dakhalia, Chuo cha Uongozi wa Chwaka na uwekezaji unaotarajiwa kufanywa na PBZ, ZSSF na Mfuko wa Barabara katika maeneo mbali mbali Zanzibar na Tanzania Bara.

Aidha alisema Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kwa mwaka wa fedha 2010/2011 imepangiwa kukusanya jumla ya shilingi 69.241billioni ambapo Idara ya Forodha imekadiriwa kukusanya 39.5 billioni na Idara ya kodi za ndani inakadiriwa kukusanya 29.7 billioni.

Alisema Bodi ya Mapato Zanzibar (ZRB) inakadiriwa kukusanya mapato ya jumla ya shilingi 60.091 billioni sawa na asilimia 95.0ya makadirio ya mwaka.

Alifahamisha kuwa kwa mwaka wa fedha uliopita 2009/2010 kwa upande wa matumizi Wizara ilipangiwa kutumia jumla shilingi billioni 56.4 zikiwemo shilingi 19.82 billioni kwa kazi za kawaida na shilingi 36.60 billioni kwa kazi za maendeleo .

Aidha alisema Serikali ilichangia jumla ya shilingi 12.89 billioni ambapo ruzuku na misaada kutoka nje iligharimu shilingi bilioni 23.71

No comments:

Post a Comment