Wednesday 14 July 2010

Spika Kificho awaapisha Ferouz, Asha Bakari

Na Halima Abdalla
SPIKA wa Baraza la Wawakilishi, Pandu Ameir Kificho jana aliwaapisha wajumbe wawili wapya wa Baraza la Wawakilishi Asha Bakari Makame na Saleh Ramadhan Ferouz, walioteuliwa juzi na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi DK. Amani Abeid Karume kuwa wajumbe wa Baraza hilo.

Spika wa Baraza la Wawakilishi, aliwaapisha wajumbe hao katika Ukumbi wa Baraza la Wawakilishi, katika hafla iliofanyika barazani hapo mbele ya wajumbe wa baraza hilo.

Aidha Kificho aliwakabidhi wajumbe hao Katiba, kanuni pamoja na sheria No.3 ambayo inahusu haki na kinga ya Mjumbe wa Baraza la Wawakilishi pamoja na sheria ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Wajumbe hao wameapa kuwa watakuwa waaminifu kwa Zanzibar katika kazi zao za Uwakilishi pamoja na kuitumikia kwa moyo mmoja ,kuhifadhi na kuilinda na kuzitetea kwa dhati katiba ya Zanzibar na Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Uteuzi wa wajumbe hao umezingatia Katiba ya Zanzibar kifungu cha 66,ambacho kinampa Mamlaka Rais wa Zanzibar kuteua wajumbe 10 wa Baraza la Wawakilishi la Zanzibar

Miezi michache iliopita, Rais wa Zanzibar aliwateua wajumbe wengine Nassor Ahmed Mazrui na Juma Duni Haji.



No comments:

Post a Comment