Thursday 11 November 2010

BUNGE LA EAC LAMPONGEZA DK. JK.

Bunge EAC lampongeza JK




BUNGE la Jumuia ya Nchi za Afrika Mashariki limempongeza Rais Jakaya Kikwete kwa kuchaguliwa tena kuwa Rais wea Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Katika salamu zake kwa Rais Kikwete, Spika wa Bunge hilo, Abdirahim Haithar Abdi alisema kwa niaba ya wabunge wa bunge hilo na kwa niaba yake binafsi linampongeza Rais Kikwete kwa kupata ushindi kwenye uchaguzi mkuu wa Oktoba 31 uliofanyika nchini.

Spika Abdirahim, amesema ushindi wa Rais Kikwete unatokana na imani ya watanzania kwake ni kubwa na alistahiki kupata ushindi huo kutokana na mafanikio makubwa katika kipindi chake cha kwanza cha uongozi.

Alisema Jumuia hiyo itaendelea kushirikiana na Tanzania katika masuala mbali mbali yakiwemo yale yanayohusu eneo zima la bara la Afrika hasa katika kuhakikisha bara hilo linatilia mkazo sualsa la amani na kuwepo hali ya utulivu ya kudumu.

Abdirahim alisema hali ya utulivu ilioijengeka Tanzania inatokana na udhibiti wa hali ya amani ya kudumu katika Tanzania, ambapo Jumuia hiyo inaipongeza hali hiyo.

Aidha amempongeza Rais Kikwete kwa kuonesha umahiri na kwamba serikali, uchaguzi mkuu Tanzania kwa kusema serikali yake, vyama vya upinzani na wananchi wenyewe wa Tanzania wameonesha ukomavu wa kisiasa na kuithibitishia dunia kwamba uchaguzi huru na wa haki unaweza kufanyika barani Afrika.

Spika huyo alisisitiza kwamba bnunge hilo linamuunga mkono Rais Kikwete na kumuombea afya njema na kwamba katika miaka ijayo, Tanzania itaendelea kuonesha njia na mwelekeo wa kudumu kwa amani na utulivu wa nchi na Afrika ya Mashariki iliyoungana.

No comments:

Post a Comment