Monday 29 November 2010

WASAFIRI PEMBA WALAKAMIKIA UTARATIBU WA KUBADILISHA BOTI

Wasafiri Pemba walalamikia utaratibu wa kubadilisha boti


Na Lulua Salum, TSJ

ABIRIA wanaosafiri kwa kutumia vyombo vya baharini wameulalamikia Uongozi wa Kampuni ya Azam Marine, juu ya mpangilio wao wa kuwabadilisha boti inayotoka Dar -es- Salaam kwenda Pemba.

Wasafiri hao walisema mpango huo wa kubadilishiwa boti, umekuwa ukiwapa usumbufu kwani wanaposafiri huwa na mizigo mingi pamoja na watoto.

Walisema licha ya kampuni hiyo kuandaa watu wa ya kushusha mizigo wakati wa kubadiliswa boti, bado tatizo la kubadilishwa na mingine kuharibika hujitokeza.

Mmoja kati wasafiri hao aliyezungumza na gazeti hili, Asha Kombo alisema kuwa mara nyingi boti wanayobadilishwa tayari imeshajaa hivyo kuwawia vigumu kwenye safari yao.

Naye Mwanajuma Rashid aliiomba kampuni hiyo kuchukua tahadhari wakati ili kuepuka matatizo hayo yanayojitokeza.

Kwa upande wake Meneja Mkuu wa Kampuni ya Azam Marine, Hussein Said, alikiri kuwepo utaratibu wa kubadilishwa boti na kueleza kuwa hajapokea malalamiko yoyote.

Alisema boti hizo zina uwezo wa kuchukua abiria zaidi ya 450 na baadhi ya siku hurejea Dar-es-Salaam, zikiwa na abiria wachache na kushangazwa suala la abiria kusema wanakosa nafasi za kukaa wanapoingia katika boti hizo.

No comments:

Post a Comment