Thursday 11 November 2010

MGAO WA MAJINA YA WABUNGE NEC HUU HAPA

Mgao majina ya wabunge NEC huu hapa


Na Mwandishi Wetu

TUME ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imetangaza mgao wa majina ya wabunge wa viti maalum kwa vyama vitatu vya siasa vilivyopata kura nyingi katika uchaguzi mkuu wa Oktoba 31.

Mwenyekiti wa NEC, Jaji Mstaafu Lewisi Makame alisema Chama cha Mapinduzi (CCM) kilipata nafasi 65 ya viti maalum, Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) viti 23 na Chama cha CUF kimepata viti 10 huku vyama vyengine 15 vilivyoshiriki uchaguzi mkuu vimekosa viti hivyo.

Kwa mujibu wa ibara ya 66 (1) (b) ya katiba ya Jamhuri ya Muungano, sura ya pili kutakuwa inasema kutakuwa na wabunge wanawake idadi isiyopungua asilimia 30 ya wabunge wote.

Hata hivyo, mwaka 2009, Serikali kupitia Baraza la Mawaziri iliamua uchaguzi wa mwaka huu, idadi ya viti maalum iongezeke hadi asilimia 40, badala ya asilimia 30 iliyotumika mwaka 2005.

Jaji Lewisi aliwataja majina hayo kwa CCM ni Sophia Simba, Amina Makilagi, Gaudensia Kabaka, Ummi Ally Mwalimu, Agness Hokororo, Martha Umbulla, Lucy Mayenga, Faida Mohammed Bakari, Felister Bura, Kidawa Hamid Saleh, Injinia Stella Manyanya, Maria Hewa, Cynthia Hilda Ngoye, Josephine Genzabuke, Ester Midimu, Maida Hamad Abdallah, Asha Mshimba Jecha, Zaria Madabida na Namelok Sokoine.

Wengine wa CCM ni Munde Abdallah, Benardetha Mushashu, Vicky Kamata, Pindi Chana, Fatuna Mikidadi, Mchungaji Dk. Getrude Rwakatare, Betty Machangu, Diana Chilolo, Fakharia Shomar Khamis, Zynabu Vullu, Abia Nyabakari, Pudenciana Kikwembe, Lediana Mng'ong'o, Sara Ally na Catherine Magige.

Wajumbe wengine wa viti vya wanawake CCM ni Ester Bulaya, Neema Hamid, Tauhida Cassian, Asha Mohamed Omari, Rita Mlaki, Anna Abdallah, Dk. Fenella Mukangara, Dk. Terezya Huvisa, Al- Shaymaa Kwegyir, Margareth Mkanga, Angella Kairuki, Zainab Kawawa, Mwanakhamis Kassim Said na Riziki Lulida.

Aidha wengine ni Devotha Likokola, Dk. Christine, Ishengoma, Mariam Mfaki, Margaret Sitta, Subira Mgalu, Ritta Kabati, Martha Mlata, Dk. Maua Daftari, Elizabeth Batenga, Azza Hamad, Mary Mwanjelwa, Josephine Changulla, Bahati Abeid, Kumbwa Makame Mbaraka, Rosweeter Kasikila, Anastazia Wambura na Mary Chatande.

Hata hivyo wajumbe wa viti maalum wa CHADEMA ni pamoja na Lucy Owenya, Esther Matiko, Muhonga Ruhwanya, Anna Mallac, Paulina Gekul, Conchesta Rwamlaza, Suzan Kiwanga na Grace Kiwelu.

Wengine ni Suzan Lyimo, Regia Mtema, Christowaja Mtinda, Anna Komu, Mwanamrisho Abama, Joyce Mukya, Leticia Nyerere, Naomi Kaihula, Chiku Abwao, Rose Kamili, Christina Lissu Mughiwa, Raya Ibharim, Filipa Mturano, Mariam Msabaha na Rachael Mashishanga.

No comments:

Post a Comment