Tuesday 30 November 2010

ZEC YATANGAZA MADIWANI VITI MAALUM

ZEC yatangaza Madiwani viti maalum


Na Mwandishi Wetu


TUME ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) imeteua Madiwani 42 wa viti maalum Wanawake kuingia katika Baraza la Manispaa la Zanzibar na Halmashauri ya Wilaya na Miji ya Chake Chake, Mkoani na Wete.

Kulingana na uteuzi huo Chama cha Mapinduzi (CCM), kimepata viti 23 vya wanawake wa viti maalum, baada ya kushinda Wadi 75 kati ya wadi 141.

Chama cha CUF, kimepata viti 19 maalum vya wanawake baada ya kuibuka na ushindi kwenye Wadi 66 kati ya wadi 141.

Kwa mujibu wa barua ya ZEC iliyosainiwa na Idrisa Haji Jecha kwa niaba ya Mkurugenzi wa Uchaguzi Zanzibar, imeeleza kuwa uteuzi wa madiwani umefanywa kwa mujibu wa sheria namba 3 ya mwaka 1995 ya Baraza la Manispaa la Zanzibar na sheria namba 4 ya mwaka 1995 ya Halmashauri za Wilaya na Mabaraza ya Miji.

Waliopenya kwenye uteuzi huo kwa upande wa Halmashauri ya wilaya ya Micheweni ni pamoja na Khadija Ali Khamis, Hadia Amir Hamad na Naima Nassor Khamis ambao wote wanatoka chama cha CUF.

Katika Halmashauri ya Wilaya ya Mkoani ambao wote kutoka chama cha CUF ni pamoja na Fatma Chum Omar, Zuleikha Ali Othman na Amina Ali Mohammed.

Walioteuliwa kuingia katika baraza la Mji la Mkoani ni pamoja na Amina Abdulla Mohammed kutoka CUF na Naima Nahodha Faki kutoka CCM.

Walioteuliwa kuingia katika Halmashauri ya Wilaya ya Wete kutoka CUF ni Salma Ali Omar, Bimkubwa Ali Mgeni na Hadia Sudi Mzee, huku Rabia Omar Salihi na Fadhila Nassor Hamad kutoka CUF wakiteuliwa kuingia katika baraza la mji wa Wete.

Kutoka Wilaya ya Chake Chake, walioteuliwa kuingia katika Halmashauri ya Wilaya ya hiyo ni Mariam Hamad Bakari, Hinaya Said Mohammed na Fatma Mohammed Saleh wote kutoka chama cha CUF.

ZEC pia imewateua Mariam Ali Suleiman na Biabu Nassor Suleiman kutoka CUF kuingia katika baraza la mji wa Chake Chake.

Kwa upande wa Wilaya ya Mjini walioteuliwa kuingia katika Baraza la Manispaa Saada Ramadhan Mwenda, Salma Abdi Ibada, Zaitun Khatib Maulid, Salma Mselem Sleyoum na Shara Ame Ahmed ambao wote wanatoka chama cha CCM.

Aidha Tume hiyo imemteua Arafa Mohammed Said kutoka CUF, kuingia katika Baraza la Manispaa la Zaznibar.

Kwa upande wa wilaya ya Magharibi, walioteuliwa kuingia kwenye Halmashauri kutoka CCM, Halima Salum Abdulla, Aziza Abdulla Amour, Asha Khamis Juma, Fatma Ramadhan Masorwa huku Hidaya Ali Hamad akiteuliwa kuingia kwenye halmashauri hiyo akitokea chama cha CUF.

Waliochaguliwa kuingia Halmashauri ya Wilaya ya Kati ambao wote ni kutoka CCM ni Zakia Mussa Chum, Maua Mohammed Ali na Maryam Khamis Hamad.

Walioteliwa kuingia katika halmashauri ya wilaya ya Kusini ambao wote kutoka CCM, Salama Ali Hamad, Nali Makame Haji na Riziki Abdulla Abdulla.

Katika Wilaya ya Kaskazini A, waliochaguliwa kuingia katika halmashauri hiyo ambao wote ni kutoka CCM ni Kiembe Vuai Jecha, Hidaya Ali Ali, Nali Makame Ngwali na Mwamvua Juma Hussein.

Katika Wilaya ya Kaskazini B, walioteuliwa kuingia katika halmashauri ya wilaya hiyo ambao wote ni kutoka CCM ni pamoja na Mtumwa Abdulla Saleh, Habiba Juma Said na Zakia Makungu Marished.

No comments:

Post a Comment