Monday 29 November 2010

DK. SHEIN AHUDHURIA MKUTANO WA EU LIBYA.

Dk.Shein ahudhuria mkutano wa EU Libya


Na Mwandishi wetu

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Ali Mohamed Shein, ameondoka nchini jana kuelekea Libya kushiriki mkutano wa tatu wa EU kwa Afrika.

Taarifa zilizopatikana zinaeleza kwamba katika mkutano huo, Dk. Shein anamwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Jakaya Mrisho Kikwete.

Katika mkutano huo wa siku mbili, Dk.Shein amefuatana na ujumbe wa viongozi mbali mbali kutoka Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na Serikali ya Tanzania.

Katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Zanzibar, Dk.Shein aliagwa na viongozi mbali mbali.

Dk. Shein na ujumbe wake wanawatarajiwa kurejea nchini Novemba mosi.

No comments:

Post a Comment