Monday 18 July 2011

WAJASIRIAMALI WA ZANZIBAR WAJIFUNZA MATUMIZI YA NGOZI MWANZA.

Wajasiriamali wa Zanzibar wajifunza matumizi ya ngozi Mwanza

Na Ali Mohamed, Maelezo
WIZARA ya Kazi, Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi na Ushirika imesema itaendelea kuwajengea uwezo wa elimu wanaushirika na wajasiriamali wengine kama mbinu ya kuwapa mafunzo ya kuwajengea uwezo wa kuzalisha bidhaa bora na kukuza fursa za ajira.
Akitoa maelekezo kwa wajasriamali waliokuwa wakijiandaa kwenda Mwanza kwa mafunzo ya ujasiamali, Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Asha Ali Abdulla alisema serikali itafikia lengo hilo kwa watu wengi zaidi,
Alisema katika kipindi ambacho ni cha ushindani wa kibishara na huduma wajasiriamali Zanzibar lazima wabadilike na kutegeneza bidhaa zitakazomudu ushindani katikamasoko ya kibiashara nchini,
“Nia ya seriki ni kuwatoa wajasiriamali katika hali waliopo na kuwapeleka mbele kwa kuwaendeleza na kuwawezesha kutengeneza bidhaa zenye ubora kwa kutumia soko la ndani, alisema Asha.
Wajasiriamali wanaohudhuria mafunzo ya matumizi ya ngozi kutengeneza viatu aina ya kubadhi kutoka Pemba na Unguja kuwa makini katika mafunzo hayo na kuchukua elimu ili watakaporudi nyumbani wawe walimu kwa wenzao.
Ziara hiyo imegharamiwa na serikali kupitia Wizara Kazi na Uwezeshaji kwa kushirikiana na Wawakilishi wa Majimbo ya Kikwajuni na Wawi Pemba.
Nae Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Ali Juma alisema inashangaza kuona bidhaa nyingi zinazotokana na sanaa za mikono katika Mji wa Zanzibar hazitoki Zanzibar.
Alisema bidhaa nyingi na sanaa zinatoka nje ya Zanzibar hivyo hazioneshi utamaduni halisi wa Zanzibar na aliwataka wajasiriamali kuwa wabunifu zaidi ili kuleta ushindani kibiashara.

No comments:

Post a Comment