Tuesday 25 May 2010

Bandari yafungua tenda ujezi wa mnara mwana wa mwana

Na Ramadhan Makame
MKURUGENZI wa Ufundi Shirika la Bandari, Abdi Omar Maalim amesema Shirika hilo litachagua kampuni yenye uwezo zaidi katika ujenzi wa mnara wa Mwana wa Mwana.

Mkurugenzi huyo alisema hayo jana katika hafla fupi ya ufunguzi wa zamani za ujenzi wa mnara huo zilizotumwa na makampuni ya ujenzi.

Alisema shirika hilo lingependa kuona mnara huo unafanyiwa matengenezo na kuwa kwenye hali bora zaidi ya ulivyo hivi sasa.

Aliyakahikishia makapuni yaliyoomba zabuni ya ujenzi huyo kuwa uadilifu wa hali ya juu utakuwepo kwenye mchakato wa kuipata kampuni hiyo.
 
“Tunaomba mtuamini kuwa kazi hii itafanywa kwa imani na kampuni zitakazoshindwa zisichoke kuomba kazi nyengine ikitokea kwenyeshirika letu”,alisema Mkurugenzi huyo.
 
Alifahamisha kuwa ili mnara huo ujengwe vizuri ni lazima kampuni bora kati ya zilizojitokeza ichaguliwe katika ujenzi wake.

Mkurugenzi Maalim, alisema mnara wa Mwana wa Mwana ni miongoni mwa minara muhimu sasa katika kuviongoza vyombo vya usafiri wa baharini.
 
“Huu ni mnara muhimu sana katika kuviongoza vyombo vya baharini, ujenzi wake lazima upate kampuni iliyo imara”,alisema.
 
Alisema baada ya ufunguzi wa zabuni hizo, zitapelekwa kwenye kamati ya uongozi wa shirika na kujadiliwa kabla ya kuelezwa kampuni ipo iliyoshinda zabuni.

Kampuni sita yalitokeza kuomba zambani ya ujenzi wa manara wa kuongozea vyombo vya baharini uliopo Tumbatu,kati ya kampuni hizo kampuni nne ndizo zilizorejesha zabuni hiyo kwa wakati.

Kampuni zilizojesha ombi la ujenzi wa huo ni Jamaa Constructions Compay ambayo imeomba zaidi ya shilingi milioni 75.5 za ujenzi wa mnara huo kwa wiki 14.
 
Kwa upande wa kampuni ya Salem Constructions Limited, imeeleza kuwa itaifanya kazi hiyo kwa wiki 10 kwa shilingi milioni 119.

Aidha kampuni ya Azim Constructions imetaka milioni 138 na ujenzi utachukua muda wa wiki 16.

Huku kampuni ya mwisho ya Zeccon Limited ikihitaji milioni 108.9 za ujenzi utakaochukua wiki 22.



No comments:

Post a Comment