Monday 31 May 2010

Mbunge Sanya, Jussa watamba Mji Mkongwe


  • Fatma Ferej, Najma, Nabahan waangukia kisogo

  • Msanii Abdulla Isaa atafuta mchawi
Na Aboud Mahmoud


MWAKILISI wa jimbo wa la Mji Mkongwe kwa tiketi ya Chama cha Wananchi CUF, Fatma Abdulhabib Ferej ameangushwa katika kinyang’anyiro cha kura ya maoni ya CUF.

Fatma ambae amepata kura 183 ameangushwa na Mbunge wa kuteuliwa na Rais, Ismail Jussa Ladhu aliyepata 334 ambapo nafasi ya tatu ikishikiliwa na Abdullah Uhuru aliepata kura 93 na Othman Hamad, kura 2.

Katika uchaguzi huo, uliofanyika katika ukumbi wa Wakf wa Wangazija Kiponda mjini Unguja, umempitisha tena Mbunge wa jimbo hilo, Ibrahim Mohammed Sanya kwa kupata kura 327.

Sanya amemuangusha msanii maarufu wa muziki wa taarab, Zanzibar, Abdullah Issa Khamis aliyepata kura 115 huku Amina Abdullah, amepata kura 119 na Ali Majid, akaangukia kura 54.

Katika hatua nyengine, uchaguzi huo wa kura za maoni kwa tiket ya CUF katika jimbo la Mji Mkongwe uliwachagua wagombea udiwani ambapo katika wadi ya Mkunazini, Diwani anaeshikilia nafasi hiyo Nassor Amin amepata kura 174 na kumuangusha Ramadhan Adnan aliepata kura 152.

Katika wadi ya Mchangani mgombea nafasi hiyo hakua na mpinzani naye ni Amir Said Bashut ambae amepata kura 317.

Uchaguzi huo ambao wengi walikuwa wakiutizamia kuwa na vishindo uliendeshwa kwa amani na utulivu huku kila mgombea akikubaliana na matokeo.

Aidha uchaguzi huo ulikuwa kivutio kikubwa kwa kuvuta hisiaa za wananchi wengi wa jimbo hilo kutokana na kila mmoja kujinadi kuzikamata nafasi hizo.

Baadhi ya Wawakilishi kupitia chama hichowalioangushwa katika nafasi hiyo ni pamoja na Naibu Spika na Kiongozi wa juu wa jumuiya ya Wanawake ya CUF, Aziza Nabahan Suleiman.

Mwengine alieangushwa ni pamoja na mwandishi wa habari wa na mtangazaji wa zamani, Najma Khalfan Juma ambao wote walipata alama ya nne katika uchaguzi huo, huku Zakia Omar, akishikilia nafasi ya pili.

No comments:

Post a Comment