Wednesday 5 May 2010

Kampuni ya C-Weed yawapa sare watoto 95 Kidoti

Na Halima Abdalla
ZAIDI ya watoto 95 waliocha masomo katika skuli ya Kidoti, wamepatoa misada ya sare na vifaa mbali mbali kutoka kampuni ya C-Weed Corporation.

Wanafunzi hao waliacha skuli kutokana na kutokuwa na huduma muhimu kwa ajili ya masomo yao pamoja na kuishi kwenye mazingira magumu.

Kampuni hiyo imetoa msaada wa sare kwa wanafunzi 95 zenye thamani ya shilingi 712,000 kwa ajili ya kuwasaidia watoto hao wanaoishi mazingira magumu na waweze kurejea skuli.

Akizungumza katika ghafla ya makibidhiano yaliyofanyika Shehia ya Kidoti, Wilaya ya Kaskazini ‘A’, mshauri wa Kampuni ya Mwani C-Weed Corporation, Makame Nassor Salum, alisema msaada huo ni utekelezaji wa sera ya kampuni yake.

Alisema fedha hizo zimetokana na kutoa shilingi tano kwa kila kilo moja ya mwani wanaoununua kutoka kwa wakulima ili kusaidia jamii.

“Sera ya kampuni yetu ni kutumia kutoa shilingi tano ya kila kilo ya mwani tunaoununua kutoka kwa wakulima na fedha hiyo hutumika kuisaidia jamii”,alisema Salum.

Alisema fedha hizo ni muhimu katika kusaidia na kuharakisha harakati za maendeleo vijijini, huku akibainisha kuwa utekelezaji wa sera hiyo ni kwa vijiji vyote wanavyonunua mwani Unguja na Pemba.

Sambamba na hayo, alisema kwa mwaka huu kampuni hiyo imepandisha bei ya mwani mara tatu na ikilinganisha na kampuni nyengine zinazouza bei ya shilingi 180.
 
Nae Mkuu wa Wilaya ya Kaskazini ‘A’,Riziki Juma Simai ,alishukuruku Kapuni ya C-Weed Corporation kwa kuweka shilingi tano kwa kusaidia jamii na kuziomba Kampuni nyengine kuiga mfano huo.

Alisema Kampuni nyengine hazina utamaduni huo hivyo kampuni hii inahitaji kupewa pongezi na kujali maendeleo ya vijiji.

Aidha aliwashauri wakulima hao wa mwani kujitahidi kuzalisha mwani ili soko liweze kukua na kuimarika.

No comments:

Post a Comment