Tuesday 18 May 2010

Wanasiasa waaswa kutopenyeza sumu vikundi vya ushirika

Na Hashim Mlenge
BAADHI ya wanasiasa nchini wameshauriwa kusimamia maedneleo nchini badala ya kutumia muda mwingi kulumbana kisiasa.

Wameelezwa kuwa suala la maendeleo lazima lipewe umuhimu wa kwanza katika mijadala ya kisiasa na viongozi hao wahakikishe kuwa wanawaunga mkono wananchi kufikia maendeeo yao.
 
Wito huo umetolewa na Katibu wa Umoja wa Vijana wa (CCM) Wilaya ya Magharibi, Abubakar Ali Hamdani, wakati akizungumza na gazeti hili hivi karibuni huko Fuoni Wilaya ya Maghabi Unguja.
 
Alisema wamechipuka baadhi ya wanasiasa wanaoingilia kati vikundi vya maendeleo kwa kuwatwisha mzigo wa propaganda za kisiasa, hali inayowafanya wasisimamievizuri maendeleo yao ya kila siku.
 
ikuwa kumekuwapo na baadhi ya wanasiasa kuingiliana kati vikundi vya maendeleo vinavyoanzishwa na wananchi halia mabyo huwafanya kuingiza siasa zao ambazo zinaeza kupelekea kuivunjika kwa umoja uo.
 
Alifahamisha kuwa hali hiyo ikizidi kutawala katika nyoyo za watu ni wazi kuwa inaweza kuvunja umoja baina ya wanavikundi vya ushirika na kutawanyika.

Katibu huyo alisisitiza kuwa si haki wala si ruhusa viongozi wa kisiasa kutumia muda wao kuingilia kati jitihada za wananchi za kutafuta maendeleo ambazo zimelekezwa zaidi kwenye njia ya ujitegemea.
 
“Sioni busara yoyote kwa wanasiasa kuzinadi siasa zao katika vkundi vya ushirka, hali ambayo huweza kuleta migongano baina ya wananchi kwa sababu vikundi hivyo havikuanzishwa kisiasa bai wa nia ya kiuchumi.
 
“Nndani ya Vikundi hakuna wanasiasa wa vyama tofauti, hivyo, tusijaribu kuzitangaza siasa zetu katika vikundi hivyo kwani tunaweza kusababisha matukio mabaya vikundini humo”.
 
Hivyo, alisema kuwa ni wajibu wa viongozi hao kuwa pamoja na wanavikundi ili kuunga mkono jitihada za kuwaletea maendeleo na kuondokana na umasikini.
 
Hatua ya Katibu huyo inaokana imetokana na kuzuka kwa baadhi ya wanasiasa wanaojaribu kuingilia kati jitihada zilizofanywana wananchi wa jimbo la Fuoni ya kuanzisha kwa kamati ya Wanafunzi ya kuwaendeleza kielimu.

No comments:

Post a Comment