Sunday 27 February 2011

BASKELI YA HAMIS Ma - SMS YATUA KWASHAMUHUNA

 Baiskeli ya 'Hamis Ma-SMS' yatua kwa Shamuhuna

Na Juma Khamis

ZAWADI ya baiskeli katika shindano 'Hamis Ma-SMS' linalochezeshwa na kampuninya simu Zantel, imekwenda kwa Waziri wa Ardhi, Makaazi, Maji na Nishati wa Zanzibar Ali Juma Shamuhuna.

Shamuhana alikabidhiwa zawadi yake iliyopokelewa kwa niaba yake, katika hafla ya kuwakabidhi zawadi washindi katika viwanja vya Malindi mjini Zanzibar.

Washindi wengine wa baiskeli ni Nassor Ali, Suleiman Salum, Salum Hamza na Mkubwa Haji, huku Hamida Ali Mwinyigogo akijinyakulia vespa.

Utoaji zawadi hizo, ulikwenda sambamba na hafla ya kuwazawadia washindi wa mbio za baiskeli zilizoandaliwa na kampuni hiyo.

Katika mashindano hayo ya kilomita 120, Juma Lukona aliibuka katika nafasi ya kwanza kwa kutumia muda wa saa 2:37:55, akifuatiwa na Ali Juma aliyeendesha kwa saa 2:39:00 na nafasi ya tatu ikachukuliwa na Khamis Juma aliyetumia saa 2:46:00.

Mashindano hayo yaliyoanzia viwanja vya Malindi kupitia Mshelishelini- Kiwengwa- Matemwe-Mkokotoni-Donge, na kumalizikia Malindi yalishirikisha washindani 20, wakiwemo wanane wa ngazi ya taifa.

No comments:

Post a Comment