Sunday 27 February 2011

Mamlaka yaonya waharibifu miundombinu ya maji

Mamlaka yaonya waharibifu miundombinu ya maji

Na Ahmada Ali, MCC

MAMLAKA ya Maji Zanzibar (ZAWA) imesema haitomvumilia mtu yoyote atakaebainika kuharibu miundo mbinu ya maji na kuitia hasara Mamlaka hiyo.

Hayo yalielezwa na Afisa Uhusiano wa Mamlaka hiyo Zahor Suleiman Khatib, alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi katika ofisi ya Mamlaka hiyo.

Alisema kumekuwa na uharibifi wa makusudi unaofanywa na baadhi ya wananchi ambao huharibu miundombinu ya maji jambo ambalo linarejesha nyuma maendeleo.

Khatib, alifahamisha kuwa Mamlaka hiyo, imekuwa ikijitahidi kulipatia ufumbuzi tatizo la ukosefu wa maji tatizo hayo lakini bado imekuwa sugu kwa upande wao kutokana na baadhi ya wananchi kufanya uharibifu makusudi.

Hata hivyo, alisema ukosefu wa huduma ya maji katika mitaa mingi imekuwa ni tatizo linalosababishwa na mabomba ya zamani ambayo yameziba.

Afisa huyo amewataka wananchi hususan wa Makadara kushirikiana na Mamlaka hiyo kutoa taarifa kuhusu watu wanaowafikiria au kuwatambua kushiriki kwenye hujuma za miundombinu ya maji.

No comments:

Post a Comment