Sunday 27 February 2011

Uchafu wasababisha mama ntilie kupigwa 'stop' Malindi

Uchafu wasababisha mama ntilie kupigwa 'stop' Malindi

Na Madina Issa

WAFANYABIASHARA ya chakula katika eneo la Malindi wametakiwa wasitishe mara moja utoaji wa huduma katika eneo hilo na kutafuta sehemu nyengine.

Mkuu wa Idara ya Afya na huduma za jamii katika Baraza la Manispaa Rajab Salum Rajab, alitoa agizo hilo aliopokuwa akizungumza na wafanyabiashara hao huko ofisini kwake.

Alisema biashara ya chakula katika eneo hilo lazima isite kutokana uchafu uliopo ambao unaweza kusababisha kuathirika afya za walaji wa chakula.

Mmoja wa wafanyabiashara hao Halima Ali Faki, aliwaomba Manispaa wawapatie sehemu za kukaa ili waendeleze biashara zao na kujikwamua kimaisha.

Pia alikiri eneo walilokuwepo haliridhishi kwa kuuza biashara zao za chakula lakini wapo hapo kwa ajili ya kujipatia riziki zao za halali na kujisaidia kusomesha watoto wao.

Sambamba na hayo wameiomba Manispaa iwastahamilie kwa kutowaondosha kwani hapo ndipo wanapopata riziki zao na kusema wataliweka eneo hilo safi zaidi.

No comments:

Post a Comment