Sunday 27 February 2011

Cossovo yatinga nusu fainali

 Cossovo yatinga nusu fainali

Na Ismail Mwinyi


TIMU ya Cossovo, imefanikiwa kuingia nusu fainali ya michuano ya ‘Chombo Cup’, kwa kuichapa Love Bite magoli 2-1, katika mchezo wa robo fainali uliochezwa kwenye kiwanja cha Magomeni Jeshini.

Cossovo ilianza kulitia dosari lango la wapinzani wao kwa goli lililofungwa na Haroun Rashid katika dakika ya 20, kabla Amour Vuai kuongeza la pili mnamo dakika ya 54.

Jitihada za Love Bite kukomboa magoli hayo ziliishia kupata bao moja tu la kujifariji, lililotiwa nyavuni na Masoud Mwalim katika dakika ya 67.

Timu za Natural na Ruff Ryder zilitarajiwa kupambana jana katika mchezo mwengine wa robo fainali.

No comments:

Post a Comment