Wednesday 23 February 2011

CHOMBO CUP YAINGIA ROBO FAINALI

 Chombo Cup yaingia robo fainali

Na Ismail Mwinyi


KATIKA mashindano ya kuwania ‘Chombo Cup’ yanayoendelea kwenye uwanja wa Magomeni jeshini, timu ya Mbendembe imejipatia ushindi wa bure baada ya Monaco kushindwa kutia mguu uwanjani.

Kutokana na hali hiyo, Mbendembe imefuzu kuingia robo fainali na kuvaana na Msimbazi katika mchezo wa kusaka nusu fainali.

Mchezo huo ndio utakaofungua pazia la robo fainali itakayochezwa leo saa 10:30 jioni uwanjani hapo.

Timu itakayoibuka bingwa wa ngarambe hizo, itazawadiwa mbuzi na mipira mitatu, huku itakayoshika nafasi ya pili ikifarijiwa kwa zawadi ya mipira mitatu.

Michuano hiyo imeandaliwa na kufadhiliwa na Mbunge wa jimbo la Magomeni Amour Chombo.

No comments:

Post a Comment