Monday 23 August 2010

DK. SHEIN AHUTUBIA WAGOMBEA PEMBA NA KUSEMA .KUNA KILA SABABU YA CCM ITASHINDA.

DK. SHENI AHUTUBIA WAGOMBEA PEMBA NA KUSEMA


Kuna kila sababu CCM itashinda

Na Bakar Mussa, Pemba

MGOMBEA Urais wa Zanzibar kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk. Ali Mohammed Sheni amesema chama hicho kimejipanga vizuri na kuna kila sababu ya kuibuka na ushindi mkubwa katika uchaguzi mkuu wa Oktoba mwaka huu.

Dk. Sheni amesema CCM kina wanachama wengi pamoja na wagombea makini wenye uwezo mkubwa wa kuinadi Ilani ya Uchaguzi ya chama hicho na kukipatia ushindi mkubwa.

Dk, Shein, alieleza hayo huko katika ukumbi wa hoteli ya Mbuyu Mkavu Vitongoji nje, Mkoa wa Kusini Unguja wakati alipokuwa akizungumza na wanachama wa CCM wa Mikoa miwili ya Pemba, ambao walijitokeza kugombea nafasi mbali mbali za Uongozi katika Majimbo yao.

“CCM, tumejipanga kwa hilo kwani Wanachma tunao na wagombea tunao wazuri wa kuinadi Ilani yetu ya Uchaguzi ‘ alisema Dk, Shein.

Dk. Sheni hata hivyo, amewataka wanachama wa CCM kuelewa kuwa kazi kubwa inayowakabili kwa sasa ni kujenga mazingira bora yatakayopelekea azma hiyo ya ushindi inafikiwa.

Alisema kuwa ushindi kwa CCM, upo wazi kwani ni chama chenye Sera sahihi na Ilani madhubuti jambo ambalo wananchi waliowengi ,wanaimani nacho hivyo wagombea wazidishe hamu ya kushirikiana na WanaCCM wengine kwa kuendeleza Ushindi utakao kifanya kiendelee kuongoza nchi.

Aliwataka wanachama hao ambao walijitokeza katika kinyang’anyiro hicho kushirikiana na na kusaidiana pamoja kwa nia moja tu ya Ushindi kwa Chama Cha Mapinduzi, kwani waliomba watu wengi lakini kwa utaratibu wa kidemokrasia ndani ya CCM anaetakiwa kusimama ni mmoja.

“CCM, inajivunia kwa kufanya mambo yake kwa mpango bila ya kuiga kutoka kwa Chama chengine kwa vile ndie mwalimu wa Siasa wa mageuzi ya vyama vingi Tanzania", alieleza.

Alisema kutokana na ubora huo CCM, itafanya kampeni zake kwa ustaarabu kwani wanayo kila sababu ya kufanya hivyo, kwani watakayo yaeleza ni yale ambayo yalinadiwa na na CCM, katika Uchaguzi mkuu uliopita ambayo yametekelezwa kwa asilimia kubwa.

“Tuliyo yaahidi kwa wananchi wakati tukiinadi ilani yetu ya Uchaguzi wa mwaka 2005-2010, tumeyatekeleza , sasa kwanini wananchi wasiendelee kutupa ridhaa wakatuchagua tena kuongoza nchi.”alisema Mgombea huyo.

Alifahamisha kuwa ni wakati wakufanya kamapeni za kistaarabu uliomkubwa ,kwani mazingira ya kufanya hivyo yapo na yameletwa na wanccm wenyewe kwa kuleta umoja , amani na mshikamano kwa wananchi.

Aliwataka wananchi wa Zanzibar kuhakikisha wanailinda Katiba ya nchi na ile ya CCM, kwani ndio inayohubiri amani, umoja na mshikamano jambo ambalo Zanzibar inajivunia kwa kuwa na maendeleo makubwa katika sekta mbali mbali.

Dk. Shein amempongeza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Aman Abeid Karume, na Katibu Mkuu wa CUF Maalim Sief Sharif Hamad, kwa kuamua kuwaunganisha pamoja wazanzibar kua kitu kimoja, na kuleta mazingira mazuri ya kisiasa kwa Zanzibar.

Alisema anaimani kwa ubora wa Ilani na Sera madhubuti za CCM wananchi waliowengi watamchagua kua rais wa Zanzibar na ataangonza kwa mjibu wa katiba ya nchi na kamwe hatomdhulumu mtu wa aina yoyote.

Aliwataka wagombea watakapokua katika kampeni zao kuyanadi na kuyaeleza yale aliomo katika Ilani ya ya Uchaguzi kwanza na ndio waeleze memgine waliojipangaia ya kuwaletea wananchi maendeleo katika Mjimbo yao na kutosahau kuwaombea kura wenzao.

Mgombea huyo wa urais kwa tiketi ya CCM ,aliongeza kwa kusema kua katika uongozi wake pindi akipewa ridhaa atahakikisha mambo manne anayasimamia kwa nguvu zake zote ikiwa ni pamoja na kuwataka wananchi kuyalinda na kuyadumisha Mapindzui ya Zanzibar ya mwaka 1964,kwani ndio dira ya wanzanibari yalioleta uswa na kuwepo kwa Serikali hii.

Alilitaja jambo la pili kua kuulinda na kuuendeleza na kuuheshimu muungango wa Jamhuri ya watu wa Zanzibar na Jamhuri ya Tanganyika uliozaa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa maslahi ya nchi mbili hizo.

Aliendelea kusema kuwa atahakikisha umoja , amani na utulivu wa watanzania kwa kuishi vizuri bila ya matatizo kwa kuelewa kua wote ni wamoja.

Dk Shein alifafanua kua jambo la nne ni kusimamia na kuelta maendeleo kwa wananchi wote bila ya ubaguzi.

Hivyo malengo ya CCM kikatiba ni kuendelea kushika hatamu kwa ngazi zote kwa Tanzania nzima pia na hilo litapatikana iwapo wagombea wataitaangaza vyema Ilani ya uchaguzi ya CCM na huivyo Tanzania yenye neeema itapatikana.

No comments:

Post a Comment