Monday 30 August 2010

MUFTI KUZIKWA LEO.

Mufti kuzikwa leo

Na Mwandishi wetu

MUFTI Mkuu wa Zanzibar, marehemu Sheikh Harith bin Khelef, anatarajiwa kuzikwa leo kijijini kwao Muyuni, Mkoa wa Kusini Unguja.

Taarifa zilizotolewa na Afisi ya Mufti Mkuu wa Zanzibar, zimeeleza kwamba, kabla ya mazishi Mufti atasaliwa saa tatu asubuhi Masjid Mushawwar, Muembeshauri Mjini Zanzibar na kuondoka hapo kuelekea Muyuni kwa mazishi yatayofanyika saa nne asubuhi.

Maiti ya Mufti huyo iliwasili Zanzibar jana jioni, ikitokea India, ambako marehemu alifariki akiwa matibabuni.

Uwanja wa ndege wa kimataifa wa Mwalimu Nyerere Mjini Dar es Salaam, mapokezi ya maiti ya Mufti, yaliongozwa na Rais Mstaafu wa awamu ya pili wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Alhaj Ali Hassan Mwinyi, Kaimu Katibu Mkuu, Wizara ya Nchi Afisi ya Rais Katiba na Utawala Bora, Abdulghani Himid Msoma, pamoja na wanafamilia na watendaji wa Ofisi ya Mufti wakiongozwa na Katibu wa Mufti, Sheikh Fadhil Soraga.

Marehemu Sheikh Harith alifariki dunia Alkhamis, huko Chenay, akiwa amelazwa hospitali kwa ajili ya matibabu kwa karibu wiki tatu.

No comments:

Post a Comment