Wednesday 25 August 2010

WAZANZIBARI KUMTUNZA DK. KARUME

Wazanzibari kumtunza Dk. Karume



Issa Mohammed

MKUU wa Mkoa mjini Magharibi Abdalla Mwinyi Khamis amesema kuwa wananchi wa Zanzibar watamtunuku Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Aman Abeid Karume nishani ya Uongozi Mahiri.

Akizungumza na waandishi wa habari afisini kwake Vuga mjini hapa, Mkuu huyo alisema hatua hiyo inatokana na kiongozi huyo kuiongoza vyema Zanzibar katika kipindi cha miaka 10.

Alisema nishani hiyo atakatotunzwa Dk.Karume itakuwa ya dhahabu ambapo itakabidhiwa kabla ya kumalizika kipindi cha uongozi wake.

Alifahamisha kuwa wazo la kutunukiwa nishati kiongozi huyo limetokana na yeye na kwamba limeungwa mkono na wananchi kadhaa wakiwemo viongozi wa vyama vya siasa.

Alisema baadhi ya wananchi wamechangia kiasi cha fedha za kununua dhahabu ya kutayarishia nishati hiyo ambapo hadi sasa kiasi cha shilingi milioni tano zimekusanywa kwa ajili hiyo.

Mkuu wa mkoa aliwataja baadhi ya waliochangia fedha hizo kuwa ni Chama cha Mapinduzi kilichotoa shilingi milioni mbili na chama cha wananchi CUF kilichotoa shilingi milioni mbili.

Aidha alisema maskani ya Dk. Mohammed Gharib Bilal imechangia shilingi milioni moja na kwamba wananchi kadhaa wameahidi kuchangia fedha kwa ajili yakifanikisha utayarishaji wa Nishati hiyo.

Mkuu wa mkoa amewataka wananchi wengine kuchangia mpango huo kwa kupitia afisi za wakuu wa wilaya za Unguja na Pemba.

No comments:

Post a Comment