Wednesday 25 August 2010

JWTZ KUSAFISHA HOSPITAL MJI WA ZANZIBAR

JWTZ kusafisha hospitali, mji wa Zanzibar


Na Mwantanga Ame (ZJMMC)

JESHI la Waananchi Tanzania, (JWTZ), litazifanyia usafi Hospitali za Zanzibar pamoja na maeneo mbali mbali ya kijamii katika Mji wa Zanzibar.

Jeshi hilo la wananchi litachukua hatua hiyo ikiwa ni miongoni mwa shamrashamra za maadhimisho ya miaka 46 tangu kuanzishwa kwake.

Jeshi la Wananchi wa Tanzania lilianzishwa rasmi Septemba 1, 1964, baada ya vijana 1,000 kutoka Jeshi la Ukombozi Zanzibar (JLU) na Kings African Rifles (KAR) kutoka Tanzania bara kumaliza mafunzo yao ya pamoja.

Taarifa ya Jeshi hilo iliyotolewa jana kwa vyombo vya habari hapa imeeleza kuwa kazi hizo zinatarajiwa kuanza leo katika maeneo mbali mbali ya Mji wa Zanzibar na Kisiwani Pemba.

Baadhi ya maeneo ambayo yatafanyiwa usafi kwa mujibu wa tarifa hiyo ni pamoja na Hospitali Kuu ya Rufaa ya Mnazi Mmoja, Bustani ya Jamhuri, Maruhubi Miembe mingi na Kinazini.

Eneo jengine ambalo wanajeshi watafanya kazi ya usafi ni pamoja na la Uwanja wa Ndege, Bustani ya migombani, Hospitali ya Wazee Welezo Beit Ras Chuo cha Ualimu na sehemu nyengine.

Aidha zoezi hilo pia litaihusisha hospitali ya Kivunge pamoja na Hospitali za SMZ iliopo Chake Chake na Vitongoji, kazi kama hizo pia zinatarajiw akufanyika katika maeneo kadhaa ya Tanzania bara.

No comments:

Post a Comment