Monday 30 August 2010

KIFICHO KUFUNGUA ITIFAKI YA KIMATAIFA

Kificho kufungua itikafu ya kimataifa



Na Mwajuma Juma

SPIKA wa Baraza la Wawakilishi aliyemaliza muda Pandu Ameir Kificho leo anatarajiwa kuifungua Itikafu ya Kimataifa itakayofanyika huko katika Msikiti wa Said Washoto Welezo Wilaya ya Magharibi Unguja.

wenyekiti wa Kamati ya Kimataifa ya Itikafu Khatib Twahir, alilieleza hayo alipokuwa akizungumza na muandishi wa hizi huko Welezo wilayani ya Magharibi.

Alisema Itikafu hiyo itakuwa ya siku tisa au kumi itaaza majira ya saa 10:45 za jioni ambapo itajumuisha waumini wa dini ya kiislamu zaidi ya 500, kutoka nchini mbali mbali za ndani na nje ya nchi.

Mwenyekiti huyo alisema tayari baadhi ya wawakilishi kutoka nchi zitakazoshiriki Itikafu hiyo wameshawasili ambapo wengine waltarajiwa kuingia mchana wa jana.

Twahir alizitaja baadhi ya waumini waliokwisha wasili ni kutoka nchi za Burundi, Uganda, Zambia na Pemba, ambapo nchi zilizotarajiwa kuwasili jana ni Kenya, Malawi na Tanzania Bara.

Alifahamisha kwamba katika Itikafu hiyo zilitarajiwa kuwasili nchi 10 lakini kwa sasa hivi zitashiriki nchi nane baada ya Oman na Emirates kushindwa kuwasilishwa washiriki wao.

Itikafu ya Kimataifa hufanyika kila mwaka ifikapo mwezi 20 wa Ramadhan, ambapo katika kikao hicho waumini kupata fursa ya kusoma hadithi, qurani na kutoa mawaidha.

Aidha pia kufanyika mashindano ya kuhifadhi qurani na hadithi za Mtume Muhammad (S.A.W) kwa vijana waliochini ya umri wa miaka 16.

Mwenyekiti huyo alisema Itikafu ya mwaka huu kiasi cha shilingi milioni 20 zinatarajiwa kutumika.

No comments:

Post a Comment