Monday 23 August 2010

MANISPA KUBURUZWA MAHAKAMANI

Manispaa kuburuzwa mahakamani

Mohamed Gharib, ZJMMC

WAFANYABIASHARA ndogo ndogo wa soko la Mwanakwerekwe wamekusudia kuliburuza mahakamani Baraza la Manispaa la Zanzibar kutokana na hatua ya kuzivunja meza zao za biashara.

Katibu wa kamati ya wafanyabiashara hao Mkubwa Khamis Hamad alisema washamefungua kesi katika kituo cha Polisi Mwanakwerekwe, na wanachosubiri kuelezwa hatua nyengine za jeshi hilo.

Mkubwa alisema malalamiko waliyoyawasilisha kwenye jalada hilo walilolifungua polisi ni kuvunjiwa meza mpya 13 ambapo kila moja meza hiyo ina gharama ya shilingi 130,000.

Alisema mbali ya meza hizo pia baraza hilo limevunja meza ndogo ndogo zipatazo 70 ambapo wamechukua hatua hiyo kinyume na utaratibu.

Katibu huyo alifahamisha kuwa pia eneo hilo ambalo meza zao zimevunjwa waliliwekea kifusi gari nane huku kila gari moja ikigharimu shilingi 130,00.

"Waliingia kuja kuvunja kupitia lango kubwa la soko na baada ya kufika hapa walimuamuru mlinzi wetu aondoke na kuzivunja meza zetu",alisema katibu hiyo.

Mkubwa alisema kuvunjiwa meza zao hizo ni kinyume na misingi ya sheria kwani kwenye eneo hilo wao wamepewa na kihalali na Halmashauri ya Wilaya ya Magharibi.

No comments:

Post a Comment