Saturday 11 December 2010

BOMBOM YASHINDWA KUIRIPIA MIGOMBANI.

Bombom yashindwa kuiripua Migombani

Na Aboud Mahmoud
Jumapili 12 Disemba 2010

TIMU ya soka ya Migombani ya Zanzibar, imetoka kidedea kwa kuifunga timu ya Bombom ya mjini Dar es Salaam goli 1-0 katika mashindano ya muungano kwa timu za vijana wa daraja la central.

Katika mtanange huo uliochezwa kwenye uwanja wa Mao Tsetung bao la washindi lilipachikwa nyavuni na Omar Juma mnamo dakika ya 50.

Vijana wa Bombom walijaribu kwa kila hali kutafuta bao la kusawazisha na pengine la ushindi, lakini mabomu yao yalishindwa kufyatuka.

Aidha katika kiputehicho, Migombani ilipata pigo bada ya mchezaji wake Ali Salum kufurushwa kwa kadi nyekundu katika dakika ya 76 kutokana na mchezo wa rafu.

Michuano hiyo inashirikisha timu za vijana kutoka Tanzania Bara na wale wa Zanzibar.

No comments:

Post a Comment