Friday 10 December 2010

Dk. SHEIN KUFANYA ZIARA YA KUWASHUKURU WANA CCM.

Dk. Shein kufanya ziara ya kuwashukuru wanaCCM



Na Mwandishi Wetu
Ijumaa 11 Disemba 2010
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Ali Muhamed Shein, anatarajia kuanza ziara ya kichama katika Wilaya za Mikoa Mitano ya Zanzibar.

Taarifa kwa vyombo vya habari iliyosainiwa na Katibu wa Kamati Maalum ya NEC Itikadi na Uenezi, Vuai Ali Vuai imeeleza kuwa kwenye ziara hiyo Dk. Shein atazungumza na viongozi wa CCM wa ngazi mbali mbali.

Alisema lengo la ziara hiyo pamoja na mambo mengine, ni kutoa shukurani na kwa wanaCCM kwa kikiwezesha Chama hicho kuibuka na ushindi kwenye uchaguzi mkuu uliopita.

Alisema Dk. Shein ataanza rasmi ziara hiyo Disemba 11 mwaka huu katika Mkoa wa Kusuni Unguja, ambapo majira ya asubuhi ataanza ziara hiyo Wilaya ya Kusini na baade kutembelea Wilaya ya Kati.

Katibu Vuai alisema Disemba 12, Dk. Shein ataendelea na ziara yake Mkoa wa Kaskazini Unguja ambapo taanzia Wilaya ya Kaskazini ‘B’ asubuhi na jioni kumaliza Wilaya ya Kaskazini ‘A’.

Ziara hiyo kwa kisiwa cha Unguja itamalizika Disemba 13, kwa kuzitembelea Wilaya za Magharibi na Wilaya ya Mjini.

Baada ya kuzimaliza wilaya za Unguja, Dk. Shein atakuwa atawasili kisiwani Pemba Disemba 14, ambapo Disemba 15 ataanza ziara katika wilaya ya Micheweni na Wete na kumaliza ziara hiyo Disemba 16 kwa Wilaya za Mkoani na Chake-Chake katika Mkoa wa Kusuni Pemba.

No comments:

Post a Comment