Saturday 11 December 2010

JINA LA MGOMBEA UMEYA WA ZANZUBAR CCM LEO.

Jina la mgombea Umeya wa Z'bar CCM leo
Na Mwantanga Ame
Jumapili 12 Disemba 2010

BAADA ya Kamati Kuu CCM, kuyarejesha majina mawili ya wanaowania nafasi ya Umeya wa Mji wa Zanzibar, ngoma nzito kwa Meya aliyemaliza muda wake Mahboub Juma Issa, kwani kazi ya ziada itamlazimu kuchukua kuvuka kigingi cha kuitetea nafasi hiyo.

Kazi hiyo itamkumba Meya huyo kwenye kikao kinachotarajiwa kutoa maamuzi ya nani atakuwa Meya wa Mji wa Zanzibar, baada ya jina la mpinzani atakaechuana nae nalo kurejeshwa na Kamati hiyo.

Kikao kitachotoa jina la mgombea wa Umeya wa Zanzibar kinatarajiwa kufanyika leo katika Afisi ya Chama Mkoa wa Mjini huko Amani Mjini Zanzibar, ambapo pia kitachagua mgombea Naibu Meya kati ya wagombea watatu.

Hapo awali Kikao cha Kamati Kuu ya Chama Cha Mapinduzi, kilichofanyika juzi Mjini Dar es Salaam kwa ajili ya kupitisha majina ya wagombea, ambapo kiliyarejesha majina yote mawili likiwemo la mpinzani wake Khatib Abrahman Diwani wa Miembeni.

Kurudi kwa majina hayo mawili tayari baadhi ya watabiri wanadai kuwa kazi kubwa itamkuta Meya, Mahboub leo hii ili kuona anafanikiwa kubakia katika kiti hicho kwa miaka mitano ijayo.

Mahboub, tayari ameshakaa katika kiti cha Umeya wa Zanzibar katika kipindi cha miaka mitano iliyopita akiwa ni Diwani wa wadi ya Kisimamajongoo aliyetokea Jimbo la Kikwajuni.

Abrahman ni Diwani mpya wadi ya Miembeni anaewania nafasi hiyo kwa mara ya kwanza ambaye alishika nafasi hiyo baada ya kushinda uchaguzi wa marudio katika Waji hiyo kwa Jimbo la Kikwajuni.

Kutokana na upya wa Diwani huyo tayari baadhi ya watabiri wa mambo ya kisiasa waliliambia gazeti hili kuwa Meya huyo aliemaliza muda wake atakuwa na kazi kubwa kutokana na changamoto iliyojitokeza kuona wagombea hao kutoka katika Jimbo moja.

Walisema bila ya kutaka kutajwa majina yao kutokana na ukaribu wa Mgombea huyo wanasiasa hao walisema hawafahamu ni kwanini iwe wagombea hao kutoka Jimbo moja kutaka kuwania nafasi hiyo ingawa ni Demokrasia.

Walifahamisha kuwa wasingemuona Meya huyo kuwa na kibarua kikubwa pale ingetokezea kwa CCM kuweka jina moja ama Wagombea hao kutokea katika Majimbo tofauti kati ya manane yalioshikwa na Chama hicho.

Sababu nyengine ambayo waliieleza ushindani wanautarajiwa kuwa mkali kwa wagombea hao kutokana na kuwapo kwa sura nyingi mpya, ndani ya Baraza hilo na sio zile ambazo alizofanya nazo kazi katika Baraza lililopita hapo awali.

Kutokana na hali hiyo wafuatiliaji hao wa mambo ya siasa walifahamisha kuwa wanachokitabiri kuwapo kwa ushindani mkali kwa wagombea hao baada ya majina yao kufikishwa katika Baraza la Madiwani wa Chama Cha Mapinduzi.

Tayari wagombea hao ili wameanza kufanya kampeni zao kwa wajumbe wa baraza hilo pamoja na viongozi wa Chama ili kuona kila mmoja anafanikiwa katika uchaguzi huo.

Akizungumza na Zanzibar Leo, Mahboub alisema ana imani kubwa ya kuweza kubakia katika nfasi yake hiyo kwa vile wagombea wote ni kuwa wanatoka katika Jimbo moja.

Alisema amepokea uteuzi wa jina lake kurudi na mpinzani wake kwani kitachoenda katika kikao hicho ni mchuano wa wagombea wanaotoka katika Jimbo moja na atakuwa tayari kupokea matokeo ya aina yoyote.

Alisema lengo lake bado kuwa aina yoyote ya matokeo yatabakia kuwa na mgombea wa CCM katika Baraza la Madiwani ili kuweza kushirikiana na wanachama wa CCM waliomo katika Baraza hilo waweze kufanya kazi zao vizuri na kwa ushirikiano.

No comments:

Post a Comment