Monday 6 December 2010

WANANCHI WATAKA MFANO WA ZANZIBAR EXPLORE UIGWE.

Wananchi wataka mfano wa Zanzibar Explore uigwe



Na Aboud Mahmoud


Jumatatu 6 Disemba 2010

KAMPUNI mbali mbali nchini zimetakiwa kuiga mfano wa Kampuni ya Zanzibar Explore kutokana na jitihada zake inazozichukua katika kuwaunganisha wanajamii na kutoa misada mbali mbali.

Ushauri huo umetolewa na wananchi mbali mbali wakati walipokuwa wakizungumza na mwandishi wa habari hizi mara baada ya kumalizika kwa kongamano la siku ya UKIMWI duniani lililofanyika katika ukumbi wa hoteli ya Serena Inn.

Wananchi hao walisema kuwa kampuni hiyo inayoongozwa na Maryam Olsen imekuwa mstari wa mbele katika kusaidia nyanja mbali mbali kwa wanajamii wa Kizanzibari.

"Naipongeza sana kampuni ya Zanzibar Explore imekuwa mstari wa mbele kusaidia huduma mbali mbali za kijamii,hii ni dalili nzuri kwa sisi wananchi wa Zanzibar,"alisema Suleiman Mauly kutoka Drug Free Zanzibar

Aidha wananchi hao walioshiriki katika kongamano hilo walisema kuwa kuna haja kubwa ya kampuni mbali mbali binafsi kufuata nyayo za kampuni hiyo kuwa kuwa bega kwa bega na jamii.

"Ningependa kutoa ushauri wangu kwa kampuni nyengine kujitokeza na kuiga mfano wa Zanzibar Explore kutokana na kuisaidia jamii katika mambo mbali mbali,"alisema Fatma Thomas kutoka ZAPHA+ .

Nae Salim Ahmed alisema kuwa Zanzibar Explore imekuwa mstari wa mbele katika kutoa msaada wa huduma za kijamii ikiwemo katika watu wanaoumwa na ugonjwa wa akili,wanaoishi na virusi vya ukimwi pamoja na watu wanaoacha kutumia madawa ya kulevya.

Zanzibar Explore ni moja ya taasisi isiyokuwa ya Kiserikali ambayo imejikita zaidi katika utoaji wa huduma za jamii katika nyanja mbali mbali katika visiwa vua Unguja.

No comments:

Post a Comment