Sunday 19 December 2010

VITONGOJI WAAHIDIWA UFUMBUZI WA MGOGORO WA ARDHI.

Vitongoji waahidiwa ufumbuzi mgogoro wa ardhi

Na Suleiman Rashid Omar Pemba
Jumatatu 20 Disemba 2010.

WAZIRI wa Nchi Afisi ya Makamu wa pili wa Rais Mohamed Aboud Mohamed amewataka wananchi wa Vitongoji, kisiwani Pemba kuendeklea kuvumilia wakati Serikali inalitafutia ufuimbuzi tatizo la kuchukuliwa ardhi yao.

Waziri Aboud ameyasema hayo nyakati tofauti alipozumgumza na wananchi wa eneo hilo, alipoyakagua maeneo yanayolalamikiwa na wananchi hao.

Alimesema Serikali ipo pamoja na wananchi hao na ameahidi kulifuatilia suala hilo kwa kina hadi pale suluhisho la kweli litakapopatikana na kusisitiza kwamba Serikali inalisimamia ili kila mmoja apatiwe haki yake bila kudhulumiwa.

Aidha, aliwataka wananchi hao kupanga mipango mizuri ya kutumia ardhi kwa vile ardhi katika visiwa hivi ni chache na idadi ya wakaazi inaongezeka siku hadi siku, hivyo ni vyema ikatumika kwa njia bora ili kila mwananchi afaidike nayo.

Kwa upande mwengine, Waziri Aboud amewataka viongozi wa Wilaya ya Chake Chake kusimamia maeneo yote yanayolalamikiwa na kuhakikisha kuwa hayajengwi hadi pale taratibu zitakapokamilika ikiwa pamoja na wadai kulipwa fidia.

Naye, Mwakilishi wa jimbo la Wawi, Maalim Nassor Juma amewataka wananchi hao kuwa wavumilivu na yeye akiwa ni kiongozi wao atalifuatilia suala hilo katika ngazi zote hadi pale ufumbuzi utakapofikiwa.

No comments:

Post a Comment