Friday 10 December 2010

KAMATI KUU KUUKATA MZIZI WA FITINA WA UMEYA ZANZIBAR.I

Kamati Kuu kuukata mzizi wa fitna wa Umeya Z'bar


Na Mwantanga Ame
Alhamisi 9 Disemba 2010

HATIMA ya nani atabebeshwa jukumu la kuwania kiti cha Umeya wa mji wa Zanzibar na Wenyeviti wa Halmashauri za Wilaya, itajulikana leo baada ya Kamati Kuu ya CCM kupitisha baraka zake.

Kwa mujibu wa taarifakutoka ndani ya CCM zinaeleza kuwa Kamati hiyo itakuwa na kikao chake leo jijini Dar es Salaam, ambapo pamoja na mambo mengine itayapitia majina ya wanaCCM waliojitokeza kuwania nafasi ya kwa miji mbali mbali Ukiwemo wa Zanzibar.

Kikao cha Kamati Maalum ya Zanzibar, ilikaa wiki iliyopita ambapo ilipitisha majina ya wanaCCM wawili waliojitokeza kuwania nafasi hiyo kwa Mji wa Zanzibar, huku pia majina ya waliojitokeza kuwania nafasi za Uenyekiti wa Halmshauri za Wilaya.

Majina yaliopitishwa na kikao hicho kuwania Umeya wa Zanzibar ni pamoja na Meya aliyemaliza muda wake, Mahboub Juma Issa ambaye atakabiliwa na kibarua kizito cha kutetea kiti hicho, baada ya kujitokeza kada mwenzake anayekinyatia kiti hicho kutoka katika Jimbo moja.

Mpinzani wa Mahboub ambaye ni Diwani wa Kikwajuni, ni Diwani wa Miembeni Abdurahman Khatib, ambao wote wanatoka jimbo moja la Kikwajuni.

Katibu wa Idara ya Uenezi Siasa na Itikadi Zanzibar, Vuai Ali Vuai, alithibitisha kuwapo kwa kikao cha Kamati Kuuu leo ambacho kitajadili majina ya wanaCCM hao.

Hata huvyo Vuai alisema taarifa zaidi za kikao hicho anayezifahamu Naibu Katibu Mkuu Visiwani Zanzibar, Saleh Ramadhan Ferouz ambaye nae alipozungumza na Zanzibar Leo, alithibitisha kuwapo kwa kikao hicho.

Hata hivyo Ferouz alisema taarifa zaidi za kikao cha leo anazo msemaji wa kikao hicho ambaye ni katibu Mkuu wa CCM, Yussuf Makamba.

Meya huyo aliyemaliza muda wake anaonekana kuzunguka huku na kule huku taarifa za wapambe zikieleza kuwa yuko katika kampeni kali kwa Wajumbe wa NEC, huku Mgombea mwenzake naye akikanyaga maeneo hayo hayo ya kuomba ridhaa kwa wajumbe hao kupitisha jina lake.

Hapo awali Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Mjini Magharib, kupitia msemaji wake Maulid Issa, kilieleza kuwa kwa upande wa Naibu Meya, nafasi hizo tayari zimepata wagombea watano waliojitokeza.

Majina ambayo yanayosubiri baraka hizo Katibu huyo alisema ni la Diwani wa Wadi ya Mlandege, Khamis Mbarouk Khamis, Mussa Haji Idrisa wa Wadi ya Mwembemakumbi na Shara Ame Ahmeid wa viti Maalum Wanawake.

Hadi sasa ni Chama cha CUF, kimekuwa kimpya huku kikiwa na Madiwani katika Majimbo ya Mjini likiwemo wa Wadi za Jimbo la Mji Mkongwe, ikiwemo ya mchangani na Mtoni,

Aidha, uchaguzi kwa Halmashauri ya Wilaya ya Magharibi, nao umeshafanyika na aliyepishwa nafas ya Mwenyekiti ni Masoud Abrahman alieshika nafasi ya kwanza na kumshinda Shaka Hamdu amekuwa wa pilina Omar Ali Khamis ni watatu.

Nafasi za Umakamu, watasubiri matokeo ya vikao hivyo ni pamoja na Amina Ali Mohammed, Aziza Abdalla na Msimu Seif.

No comments:

Post a Comment