Monday 6 December 2010

JENGO LA UWANJA WA NDEGE KUAZA JANUARI.

Jengo la abiria uwanja wa ndege kuanza Januari


Na Mwanajuma Abdi


Jumatatu 6 Disemba 2010


JENGO la kisasa la abiria katika Uwanja wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume, utaanza Januari mwakani ambao utagharimu dola za Marekani milioni 70.4 hadi kukamilika kwake.

Mkurugenzi wa Anga, Malik Mohamed Hanif, alisema hayo alipokuwa akizungumza na gazeti hili, mjini hapa amesema ujenzi huo utaanza mapema mwezi ujao na utachukuwa miaka mitatu hadi kukamilika kwake, ambao utagharimu Dola za Marekani milioni 70.4.

Alisema jengo hilo litajengwa na kampuni ya Beijing Enginering Construction Group (BECG) ya China ambayo imeshinda zabuni ya ujenzi huo.

Alieleza hatua za awali za matayarisho zimeshafanyika za kupima udongo na hivi sasa kazi inayoendelea ni kuingiza vifaa vya ujenzi nchini ili kazi hiyo iweze kuanza mwezi ujao.

Aidha alifahamisha kuwa, ujenzi huo pia utahusisha barabara katika eneo la jengo hilo sambamba na kuweka maeneo maalum ya maegesho ya vyombo vya moto, ili kuweka haiba nzuri ya muonekano wake.

Ujenzi wa jengo jipya la kisasa la abiria linajengwa na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar baada ya kupata fedha za mkopo nafuu kutoka China.

Hata hivyo kujengwa kwa jengo hilo litasaidia kuondoshea kero abiria wanaosafiri na wananchi mbali mbali wanakwenda kuwapokea wageni wao au kuwasindikiza katika uwanja huo.

No comments:

Post a Comment