Tuesday 7 December 2010

NEC ZANZIBAR YAJADILI WANAOWANIA UMEYA

NEC Zanzibar yajadili wanaowania Umeya



Na Mwandishi wetu
Jumanne 7, Disemba 2010
MAKAMU Mwenyekiti wa CCM Zanzibar, Amani Abeid Karume jana alikiongoza kikao cha Kamati Maalum ya Halmashauri Kuu ya Taifa Zanzibar, kilichofanyika afisi kuu Kisiwandui.

Kwa mujibu wa taarifa kwa vyombo vya habari iliyotolewa na Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar, Saleh Ramadhan Ferouz, kikao hicho pamoja na mambo mengine kilipokea na kujadili majina ya wana CCM waliojitokeza kuomba kuteuliwa kugombea nafasi ya Meya wa Manispaa ya Zanzibar kwa mwaka 2010-2015.

Katika kinyang’anyiro hicho, ni wanachama wawili tu ndio waliojitokeza kuomba kuwania nafasi hiyo, ambao ni Mahbubu Juma Issa na Khatib Abdulrahman Khatib.

Kikao hicho kimetoa mapendekezo yake kwa Kamati Kuu ya CCM juu ya wana CCM hao waliojitokeza kugombra nafasi hiyo kwa hatua zinazoendelea.

No comments:

Post a Comment