Wednesday 1 December 2010

MAKAMO WA RAIS WA KENYA, KILONZO MUSYOKA AMPONGEZA RAIS WA ZANZIBAR.

Alhamisi 2, Disemba, 2010
Naye Rajab Mkasaba anaripoti kutoka Tripoli Libya, Makamu wa Rais wa Kenya, Kalonzo Musyoka amempongeza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza Mapinduzi, Dk. Ali Mohamed Shein kwa kuchaguliwa kuwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi.

Pongezi hizo amezitoa alipokuwa na mazungumzo na Dk.Shein mjini Tripoli, Libya ambako viongozi hao wote walihudhuria katika mkutano wa tatu wa Mashirikiano kati ya Umoja wa Afrika na Jumuiya ya Ulaya.

Katika mazungumzo hayo Musyoka alitoa pongezi kwa Zanzibar kwa kuendesha uchaguzi kwa amani na utulivu na kuweza kujijengea sifa kubwa ndani na nje ya nchi na kueleza kuwa Kenya itaendeleza uhusiano na Zanzibar ambao upo kwa muda mrefu.

Nae Dk. Shein alitoa shukurani kwa Rais Kibaki kutokana na salamu za pongezi alizomtumia kutokana na kuchagiliwa kwake kuwa Rais wa Zanzibar na kumueleza Musyoka kumfikishia kiongozi huyo salamu za shukurani kutoka kwake.

No comments:

Post a Comment