Monday 6 December 2010

SHEKH SHARIF ATAKA WAKATWE WANAOJINUFAISHA KWA JINA LAKE.

Sheikh Sharif ataka wakamatwe wanaojinufaisha kwa jina lake


Na Kunze Mswanyama, Dar


Jumatatu 6 Disemba 2010

WAKAAZI wa Jiji la Dar es Salaam, wameaswa kutowasikiliza watu wanatumia jina na nembo ya Sheikh Sharif Zaharani Foundation, ili kuwahadaa wananchi.

Sheikh Sharrif alitoa tahadhari hiyo kwenye mkutano wake na waandishi wa habari huko afisi kwake jijini Dar es Salaam.

Alisema tayari kuna taarifa za kubakwa wasichana wawili na mtu ambaye alitumia jina na nembo yake Sheikh Sharrif Foundation na sambamba na kuwepo kwa taarifa za utapeli.

Alisema wapo watu wanaotumia nembo na jina lake kwa maslahi binafsi wakidai kuwa nao wanaouwezo wa kuwahudumia watu kiroho.

Sheikh huyo ambaye ana umri wa miaka tisa, alisema watu hao pia wanajitambulisha kuwa wao ni masharifu kumbe siyo bali ni matapeli wa mjini wanaotumia uongo wa dini ili kujipatia mali kwa njia ya udanganyifu.

Sheikh Sharrif aliwataka wananchi kutosita kuwachukulia hatua za kisheria matepeli hao kwa kuwafikisha katika vituo vya polisi kwani wapo kwa ajili ya kuwaibia watu.

“Wale wote waliokwisha fanyiwa matendo hayo watoe taarifa katika kituo chochote cha polisi kilicho karibu nao, ili kurahisisha kukamatwa kwao na sheria kuchukua mkondo wake”, alisema.

Wakati huo huo, serikali ipongezwa kwa hatua yake ya kuruhusu matumizi na usajili wa waganga wa tiba mbadala baada ya waganga hao kufungiwa kufuatia wimbi la mauaji ya watu wenye ulemavu wa ngozi.

Akitia pongezi hizo, mgunduzi wa dawa ya figo, Danny Kyauka, alisema wakati wote walipokuwa wamefungiwa leseni zao, walikuwa wakitoa huduma kwa kujifichaficha.

Dokta Danny, alisema kuruhusiwa kwa leseni zao kutawafanya kuendelea kutoa huduma hizo bila ya kificho, sambamba na kuwapatia huma za matibau wnaanchi wenye watatizo mbali mbali.

No comments:

Post a Comment