Sunday 19 December 2010

MFUKO WA BARABARA KUTUMIA 4.609BN /- MATENGENEZO BARABARA KADHA.

Mfuko wa barabara kutumia 4.609bn/- matengenezo barabara kadha
Jumatatu, 20 Disemba 2010

FUKO wa Barabara nchini unakusudia kutumia shilingi bilioini 4.609 kuzifanyia matengenezo bara bara kadhaa Unguja na Pemba.

Fedha hizo ni sehemu ya michango ya wananchi inayotokana na kodi ya mfuko wa barabara inayokuswanya kutokana na huduma ya barabara ambapo mwaka 2010/2011 mfuko huo umekusanya shilingi bilioni 0.842 sawa na asilimia 15 ya makusanyo yote.

Mkurugenzi wa Mfuko huo, Abdi Khamis alimwambia Waziri wa Nchi Afisi ya Rais Fedha, Uchumi na Mipango, Omar Yussuf Mzee kwamba fedha zitazotumika kwa ujenzi wa barabara hizo ni sawa na asilimia 85 ya makusanyo yote ambayo yalifikia shilingi bilioni 5.451 mwaka 2010/2011.

Barabara zitakazohusika na mpango huo, ni ya mzunguko Mwanakwerekwe na kuendelea hadi eneo la nyumba mbili.

Barabara nyengine alioitaja ni ya Bungi Miembe Mingi kutokana na kuwepo kasoro ya kiwango cha barabara hiyo na kuweza kusababisha ajali za mara kwa mara.

Bara bara nyengine inayoingiakwenye mpango huo ni ya Mwembe njugu kuelekea Kibanda Hatari, Sokoni kwa Mchina hadi Mwanakwerekwe, Mpendae hadi Nyumba mbili, Kidongechekundu hadi Jang’ombe, Mwembemadema hadi Kikwajuni na Koba hadi Kajengwa.

Kwa upande wa Pemba, Mkurugenzi huyo alizitaja barabara zitakazojengwa ni ya Wete Weni, Ole hadi Konde, Chakechake hadi Wesha, Mbuguani hadi Tironi na Wesha hadi Mkumbuu.

Nyengine Kipapo hadi Mgelema, Chake Chake hadi Mjini na mitaa mbali mbali, kwa maelezo yake, maandalizi ya barabara za Mji wa Zanzibar, alisema yamefikia hatua nzuri baada ya kutumiwa kampuni mbali mbali kufanya kazi bhizo.

Kwa mujibu wa Mkurugenzi huyo, hadi Novemba mfuko huo unaidai serikali shilingi 757,870,674.60 .

Hata hivyo, Mkurugenzi huyo alikosoa mfumo unaotumika kuendeshea mfuko kwa kuendelea kuwekwa chini ya Wizara ya Miundo mbinu.

No comments:

Post a Comment