Friday 30 April 2010

Dk. Karume mgeni rasmi kilele cha Mei day

Na Ramadhan Makame
WAFANYAKAZI wa Zanzibar, kesho wanaungana na wafanyakazi wenzao kusherehekea siku ya wafanyakazi duniani Mei mosi.

Kwa mujibu wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Zanzibar (ZATUC), limeeleza kuwa sherehe hizo zinatarajiwa kufanyika hoteli ya Bwawani iliyopo mjini hapa.

Shirikisho hilo, lilieleza kuwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Amani Abeid Karume atakuwa mgeni rasmi katika sherehe za leo.

Sherehe hizo zitaanza kwa maandamano ya wafanyakazi wa taasisi mbali mbali yatakayoanzia viwanja vya Malindi na kuelekea hoteli ya Bwawani.

Siku ya wafanyakazi duniani huwapa fursa wafanyakazi kujitathmini kwa kuangalia utendaji wao kwa maendeleo yao na taifa.

Ujumbe wa mwaka huu wa sherehe za wafanyakazi, ‘uchaguzi mkuu usaidie kuboresha maslahi na ushirikishwaji wa wafanyakazi’.

No comments:

Post a Comment