Friday 30 April 2010

Makunduchi sekondari kuadhimisha miaka 100

Na Ali Mohamed, Maelezo
SKULI ya Sekondari Makunduchi inatarajia kufanya sherehe za kuadhimisha miaka 100 ya kuanzishwa kwake pamoja na miaka 20 ya urafiki na skuli ya Stone Comprehension ya Uingereza.

Akizungumza na wanakamati ya skuli hiyo na wanafunzi, Katibu wa kamati hiyo, Haji Simba Hassan amesema sherehe hizo zitafanyika mapema Julai, 2010.

Alisema maadhimisho hayo ni sehemu muhimu ya kukumbuka historia refu ya skuli hiyo na mafanikio yaliyopatikana katika kipindi cha mikaa 100.

Mwenyekiti huyo aliwataka watu waliosoma skuli hiyo kushiriki kikamilifu katika sherehe hizo ili ziweze kupata ufanisi mkubwa.

Aidha, katika maelezo yake, Katibu huyo hakuainisha nani ataongoza maadhimisho hayo ya kihistoria.
 
Wakati huo huo, Katibu Haji Simba Hassan, alisema skuli hiyo ina mpango wa kuyatengeneza upya mabanda ya skuli yaliyochakaa kwa kujengea mazingira mazuri wanafunzi.

Alisema katika mpango huo wa ujenzi, zaidi ya shilingi milioni 100 zinatarajiwa kutumika ambapo amewataka wote waliosoma katika skuli hiyo kuchangia kwa hali na mali.

Skuli ya Sekondari Makunduchi ni miongoni mwa skuli za muda mrefu kujengwa katika Mkoa wa Kusini ambapo watu wengi wakiwemo viongozi wa ngazi za juu serikalini walisoma skuli hiyo.

No comments:

Post a Comment