Friday 30 April 2010

Mradi wa usambazaji waya wa umeme watiwa saini Ikulu

Na Mwanajuma Abdi

TAASISI ya Millennium Challenge Account ya Tanzania (MCA-T) imetilia saini mkataba wa ujenzi wa mradi wa utengezaji wa utandazaji waya wa pili wa kusafirisha umeme kutoka Tanzania Bara hadi Zanzibar na kampuni ya VISCAS ya Japan utaogharimu dola za Marekani 28,210,400.

Sherehe hizo zilifanyika jana, Ikulu mjini hapa, ambapo Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Amani Abeid Karume na Balozi wa Marekani nchini Tanzania, Alfonso E. Lenhardt walishuhudia.

Waziri Kiongozi wa SMZ, Shamsi Vuai Nahodha aliwaongoza Mawaziri na watendaji wengine wa SMZ, katika kushuhudia hafla hiyo adhimu kwa wananchi wa Zanzibar.

Wengine waliohudhuria ni Mkurugenzi Mkaazi wa MCC, viongozi wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, pamoja na Maofisa wa MCC, MCA-T, TANESCO, ZECO na wawakilishi kutoka kampuni ya ESB International ya Ireland.

Mradi huo unafadhiliwa na Serikali ya Marekani na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar pia nayo inachangia dola milioni 3.1, katika kufanikisha mradi huo kukamilika kwa wakati uliopangwa.

Mkurugenzi Mtendaji wa MCA-T, Bernard Mchomvu alisaini kwa niaba ya Tanzania na Tetsuji Ohno ameiwakilisha Kampuni ya VISCAS- Japan, ambao utatumia dola za Marekani 28,210,400 hadi kukamilika kwake Disemba 2012.

Akizungumza mara ya utiaji wa Saini huo, Mkurugenzi Mtendaji wa Tanzania wa Millennium Challenge Account, Bernard Mchomvu, alisema mradi huo ni muhimu katika kukuza uchumi na kupambana na umasikini nchini.

Aliongeza kusema kwamba MCA-T imekuwa ikifanya kazi pamoja na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar na Serikali ya Tanzania katika kusimamia miradi ya Shirika la Changamoto la Millenia (MCC) inayofadhiliwa na Serikali ya Marekani, ambapo jumla ya Dola za Marekani 698.1 zimetolewa na Serikali ya Marekani kusaidia miradi mbali mbali ya maendeleo ikiwemo miundombinu ya barabara, usafirishaji wa maji safi na ujenzi wa waya wa pili wa umeme kwa ajili ya kuwaletea wananchi maendeleo na kukuza uchumi wa nchi ili kuweza kupambana na umasikini.

Nae Mwakilishi wa Kampuni ya VISCAS, Tetsuji Ohno alieleza utiaji wa saini wa mkataba huo umefungua hostoria mpya kwa kampuni yake katika Bara la Afrika kwa nchi ya Tanzania, Zanzibar kushinda zabuni ya ujenzi wa kuweka waya wa pili utaokuwa na megawati 100, ambao utakuwa na nguvu zaidi katika upatikanaji wa huduma hiyo ya uhakika Zanzibar.

Alieleza mradi huo utasaidia kuimarisha mfumo mzuri wa biashara, sambamba na kukuza uchumi na kujenga mustakabali mzuri wa maendeleo ya baadae kwa nchi na wananchi kwa ujumla.

Nae Balozi wa Marekani nchini Tanzania, Alfonso E. Lenhardt aliongeza kusema kwamba, sherehe za utiaji wa saini huo ni kuongezea nguvu huduma ya umeme utaosafirishwa kutoka Tanzania Bara hadi Unguja kwa kufikia megawait 100 na utagharimu Dola za Marekani milioni 28.

Alifahamisha kuwa, mradi huo ni muendelezo wa miradi mbali mbali inayofadhiliwa na Serikali ya Marekani kupitia kwa Shirika lake la Changamoto (MCC), tokea mwaka 2008 ilipasainiwa kufanya kazi nchini, ambapo jumla ya Dola za Marekani milioni 698.1 imeshasaidia kwa nchi ya Tanzania.

Alifafanua kuwa, Taasisi MCC imesaidia katika uwekaji wa miuondombinu ya maji, barabara, afya na umemem ili kuwa na nguvu zaidi katika matumizi katika skuli na biashara, ambayo hayo yote yanafanyika kwa ajili ya kukuza uchumi.

Aidha alitoa salamu za watu wa Marekani na Rais wao Obama kuwa wanajivunia kusaidia mradi huo wa umeme Zanzibar katika kuongezea nguvu zaidi.

Alisema kuongezewa nguvu kwa waya wa umeme utasaidia kuweka sera nzuri za mazingira ya watu binafsi kuwekeza nchini.

No comments:

Post a Comment