Tuesday 27 April 2010

Mtoto wa kambo aunguzwa maji ya moto

Na Jumbe Ismailly, Singida
POLISI Mkoani Singida inamshikilia mwanamke kwa tuhuma za kwa kumwagia maji ya moto na kusababisha kumuunguza sehemu mbali mbali za mwili wake kwa kilichodaiwa kuwa hapendi kuishi naye.

Kwa mujibu wa kamanda wa polisi wa Mkoa wa Singida, Celina Kaluba, mwanamke huyo ni Maria Eliasi (30) mkaazi wa mtaa wa Sokoine, mjini Singida alimuunguza Amina Mustafa mwenye miaka 2 na miezi kumi.

Hata hivyo, kamanda huyo alisema tukio hilo lilitokea tarehe 21 mwezi huu saa nne asubuhi katika mtaa wa kituo cha zamani cha magari, kata ya Majengo.

“Ajali hiyo ilisababisha mtoto huyo kuungua vibaya”, alisisitiza Kaluba.

Kwa mujibu wa msemaji huyo wa jeshi chanzo cha tukio hilo ni kutokumpenda mtoto ambaye alikuwa akiishi pamoja naye.

Hata hivyo kamanda Kaluba hakusita alifafanua kuwa mtuhumiwa huyo amekamatwa na wakati mtoto huyo aliyelazwa katika Hospitali ya Mkoa wa Singida hali yake ni mbaya.

No comments:

Post a Comment